Serikali ya Afrika Kusini yaomba rasmi hati ya kukamatwa kwa Putin

Messenger RNA

JF-Expert Member
Jul 24, 2022
1,105
3,026

Putin

Getty ImagesCopyright: Getty Images
Serikali ya Afrika Kusini imetuma maombi rasmi kwa mahakama kutoa hati ya kukamatwa kwa Rais wa Urusi Vladimir Putin iwapo atawasili nchini humo.
Chama kikuu cha upinzani nchini Afrika Kusini, Democratic Alliance, kinasema kuwa haya ni makubaliano ya matakwa yake: chama hicho hapo awali kiliwasilisha ombi kwa mahakama kulazimisha serikali kutekeleza agizo la kukamatwa kwa Putin lililotolewa mwezi Machi na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) huko The Hague.
Afrika Kusini inawajibika rasmi kufuata matakwa ya ICC, na Putin alialikwa kwenye mkutano wa BRICS utakaofanyika Agosti mjini Johannesburg, lakini uongozi wa nchi hiyo haukuficha ukweli kwamba haikuwa na nia ya kumkamata rais wa Urusi.
Hata hivyo, serikali ya Afrika Kusini haikupata njia yoyote ya kisheria ya kutotekeleza kibali hicho. Viongozi wa Afrika Kusini wamesema kwa uwazi katika siku za hivi karibuni kwamba walimwomba Putin asiende, na siku ya Jumatano aliamua kutokwenda, ingawa si lazima kutokana na hofu ya kukamatwa.
BBC SWAHILI
 

View attachment 2695969
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Serikali ya Afrika Kusini imetuma maombi rasmi kwa mahakama kutoa hati ya kukamatwa kwa Rais wa Urusi Vladimir Putin iwapo atawasili nchini humo.
Chama kikuu cha upinzani nchini Afrika Kusini, Democratic Alliance, kinasema kuwa haya ni makubaliano ya matakwa yake: chama hicho hapo awali kiliwasilisha ombi kwa mahakama kulazimisha serikali kutekeleza agizo la kukamatwa kwa Putin lililotolewa mwezi Machi na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) huko The Hague.
Afrika Kusini inawajibika rasmi kufuata matakwa ya ICC, na Putin alialikwa kwenye mkutano wa BRICS utakaofanyika Agosti mjini Johannesburg, lakini uongozi wa nchi hiyo haukuficha ukweli kwamba haikuwa na nia ya kumkamata rais wa Urusi.
Hata hivyo, serikali ya Afrika Kusini haikupata njia yoyote ya kisheria ya kutotekeleza kibali hicho. Viongozi wa Afrika Kusini wamesema kwa uwazi katika siku za hivi karibuni kwamba walimwomba Putin asiende, na siku ya Jumatano aliamua kutokwenda, ingawa si lazima kutokana na hofu ya kukamatwa.
BBC SWAHILI
Huyu mzee kwa sasa anaishi kwenye mahandaki kama kenge.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Ukisoma juju hivi utadhani serikari ya Africa kusini ndo imeomba waranti hiyo... kumbe ni ngonjera za wapinzani akina Malema ndio wanahimiza kuhusiana na waranti hiyo...
 
Anaishi kama digidigi mzee wa watu,maana akitoka nje ya nchi tu yupo kwenye mikono salama.
Endeleeni kujitia moyo...kumsimanga mtu ambye hajui hata kuna species kama hizi zina-exist.
Kudai katiba tu tumeshindwa...kusoma mikataba tu yawaarabu hatuwezi mpaka tunawekewa vipengele vinavyotutia aibu ....

Then mko na wishful thinking na hisia kwa mtu ambaye hata akifa leo ghafla..dunia nzima inatambua na itatambua kuondoka kwake whether negatively or positively...

Waafrika tulilogwa au??
 
Back
Top Bottom