Serikali Kujenga Flyover Saba katika jiji la Dar es Salaam

Serikali Kujenga Flyover Saba katika jiji la Dar es Salaam

Wakijenga flyover saba Dar es Salaam watabomoa hadi ikulu ya magogoni kupisha upanuzi wa hizo flyover.
Vijumba vyetu vitabomolewa tutishi chini ya flyover.
Naomba WB wasiwakopeshe tu maana tutakoma.
 
Mwaka huu serikali itakamilisha upembuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi wa barabara saba za juu (flyover) ktk jiji la Dar es Salaam. Barabara hizo zitajengwa ktk maeneo ya Chang’ombe, Uhasibu, Mwenge, Morocco, Kamata, Magomeni na Tabata. -@TZ_MsemajiMkuu wa Serikali, Dk Abbasi.
DVfzC6_X0AAVtth.jpg:large
Kwenye hoyo picha yako nioneshe Mwenge, Tabata, Chang'ombe, Morocco zilipo. Mnajenga MADARAJA sio flyover!!
 
Wewe unadhani ni nini vile??? mfano pale Tazara
Yaan sijui wanataka lijengwe vipi ndio liwe flyover kwa uelewa wao, maana flyover ni daraja la kuvusha magari, sasa kuita flyover ni daraja as if ni daraja la mto ruvu sidhani kama ni sahihi
 
Kama sio kitu cha kujivunia mbona awamu zilizopita hazikuwapo? Tuambie cha kujivunia katika awamu zilizopita zaidi ya kukua kwa RUSHWA, UBADHIRIFU UFISADI, WIZI ,ZIARA ZA NJE ZISIZO KUWA NA TIJA NK
 
Let’s accept the fact we are shit holes! Huwez kuziiita zile vitu flyover yale ni madaraja ya juu!
 
Panda daladala ya kupita hizo junction, au kama una gari pita mida ya rush hour, nakuhakikishia foleni utakayokumbanna nayo utarudi kuomba radhi
Kwani hizo barabara za juu ndo mkmbozi wa foleni maana kuna uzi ulishaletwa huku ukionyesha foleni kwenye mataifa makubwa kama China
 
Ktk juctions zote, Tazara ndio baba lao kwa kusababisha foleni, pale wamepatia kuanza napo ingawa bado foleni itakuwapo.
Balaa lingine ni pale Ubungo, yaani usiombe ukatane na lifoleni la pale, masaa matatu yanaweza kukatika hujavuka pale, hasara ilioje???!!! Bila hizi flyover tusahau maendeleo yoyote hapa jijini Dar na nchini kwa ujumla. Maana hizi ni kama chemba zilizoziba na kublock maendeleo..!!!
 
Daraja la Kigamboni lilipangwa kujegwa tangu 1933
Na sisi tumepata bahati ya kula matunda yake
Kukata tamaa ni mwiko!
Tunayaweza maana hatuna tena uwoga ndani yetu
SKY IS NOT A LIMIT
Ni kweli, mimi mwenyewe ni mnufaika wa matunda ya mipango ya 1933, mfani mwinge ni hiz Kinyerezi gas power plants, gesi iligunduliwa miaka ya 70 lakini leo tunakula matunda. Mipango mingine ni hii ya Stiegler's gorge, mipango yake ilianza tangu enzi za Nyerere lakini kwa uwezo wa muweza tunaweza tukala matunda ndani ya miaka 10.., tusikate tamaa...
 
Yaan sijui wanataka lijengwe vipi ndio liwe flyover kwa uelewa wao, maana flyover ni daraja la kuvusha magari, sasa kuita flyover ni daraja as if ni daraja la mto ruvu sidhani kama ni sahihi
Nadhani kuna tofauti kati ya flyover na bridge.....labda wajuzi wa lugha watujuze
 
Kwenye hoyo picha yako nioneshe Mwenge, Tabata, Chang'ombe, Morocco zilipo. Mnajenga MADARAJA sio flyover!!
Flyover ni barabara za juu na madaraja ni bridge.....labda wajuzi wa lugha watujuze zaidi??
 
Kwani hizo barabara za juu ndo mkmbozi wa foleni maana kuna uzi ulishaletwa huku ukionyesha foleni kwenye mataifa makubwa kama China
Wale wana magari mara 1000 ya tz, sasa wasingekua na flyover nadhani nchi nzima wangekuwa wanatembelea baiskeli nadhani. Toa hiyo minyoo huko kichwani aisee.., daah..
 
Back
Top Bottom