Serikali Kujenga Flyover Saba katika jiji la Dar es Salaam

Serikali Kujenga Flyover Saba katika jiji la Dar es Salaam

wamekudanganya kitu gani wewe???
e2493d84a97c62375c64c7b18c5b5c49.jpg
 
Miradi ya hivi ni ndoto za alinacha. Bado wanaamini kuna watu wako usingizini kiasi hicho?
 
Unaweza ukatoka chozi kabisa foleni ya Tazara, viongozi wetu hawajawahi na hawaijui foleni ya Tazara ndio maana huu mradi umechelewa kutekelezwa..
Foleni linakukuta uko sokota unakuja tazara, au matumbi au vingunguti, lazima utoe chozi na ukichepuka tu polisi hao. Ni shida, viongozi hawajui kero za foleni kwa kweli.
 
Hivi Tanzania ni Dar es salaam Pekee? Kazi ipo.
 
Wale wana magari mara 1000 ya tz, sasa wasingekua na flyover nadhani nchi nzima wangekuwa wanatembelea baiskeli nadhani. Toa hiyo minyoo huko kichwani aisee.., daah..
Hio barabara ya juu inamsaidia nn mchimba madini kule manyara .elimu Bora ndo mkmbozi
 
Kwani watanzania tumesema tunataka kupita juu sisi tunataka
Maji Safi, salama na ya unakuja 24/7
Umeme wa uhakika 24/7
Elimu Bora na sio hii ngonjera tunazofundishwa sahivi
Ajira
Mazingira mazuri ya kujiajiri nasio hizo barabara za juu maana sisi za chini zinatutosha mkiweza ziweka katika good condition
......habari za Kinyerezi 1,2 na 3 hujawahi kusikia ? Steigler Georges ?
 
46% ya watanzania hawana vyoo

63% ya watanzania hawana maji safi na salama
.

34% ya watanzania wanatumia chini ya 2000 kula, kusafiri, etc
 
Ni kweli, mimi mwenyewe ni mnufaika wa matunda ya mipango ya 1933, mfani mwinge ni hiz Kinyerezi gas power plants, gesi iligunduliwa miaka ya 70 lakini leo tunakula matunda. Mipango mingine ni hii ya Stiegler's gorge, mipango yake ilianza tangu enzi za Nyerere lakini kwa uwezo wa muweza tunaweza tukala matunda ndani ya miaka 10.., tusikate tamaa...
Ni kweli kabisa
Mola azidi kutubariki
 
Naomba viongozi watumie akili kidogo!! Watoto wanasoma kwa shida wanashinda njaa mpaka kupata vidonda tumbo.walimu wao wanalia hawalipwi stahili zao nao wanapepesuka kwa njaa mashuleni! Matokeo yake elimu imeporomoka sana na inazidi kuwa ya hovyo...viongozi wanakimbilia sifa za fly overs na madege yanayotuletea hasara kubwa. Nilini tutaamka na kutoka kwenye shithole asee! Nchi gani iliendelea bila kuinua elimu? Watoto wetu wanauwezo duni mmno siyo tuu sayansi bali hata kupambanua mambo. Poor us
 
Mwaka huu serikali itakamilisha upembuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi wa barabara saba za juu (flyover) ktk jiji la Dar es Salaam. Barabara hizo zitajengwa ktk maeneo ya Chang’ombe, Uhasibu, Mwenge, Morocco, Kamata, Magomeni na Tabata. -@TZ_MsemajiMkuu wa Serikali, Dk Abbasi.
DVfzC6_X0AAVtth.jpg:large
Just thinking loud.Hivi baada ya wizara zote kuhamia dodoma congestion city centre haitapungua?
 
Back
Top Bottom