Serikali kuanzisha mfumo wa kidigitali kukusanya kodi kwenye matangazo ya mitandao ya kijamii

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Jul 24, 2021
576
1,626
IMG_0531.jpeg

Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango wakati anawasilisha Bajeti ya 2023/2024 amesema kutokana na ukuaji wa teknolojia, biashara nyingi zinafanyika mtandani na hivyo matangazo yanayofanywa kukuza bishara hizo kwenye mitandao ya kijamii kama Instagram, Facebook, Twitter na blogs mbalimbali imekua maradufu.

Kutokana na hayo, Serikali kwa kushirikiana na Sekta binafsi, inatarajia kuanzisha mfumo wa kidijitali wa kufuatilia na kuhakikisha kodi husika za Serikali zinalipwa kwa wakati. Hii itajumuisha matangazo ya Biashara ambayo huwekwa na watu maarufu (digital influencers) na biashara za mtandaoni zinazofanyika nchini.
 
Waziri wa fedha na mipango, wakati wa kuwasilisha bajeti ya 2023-2024 amesema kutokana na ukuaji wa
teknolojia, Dunia inashuhudia mabadiliko makubwa katika tasnia ya matangazo ya kibiashara (Advertisment) ambapo sasa matangazo mengi yamekua yakifanyika kupitia mitandao (online advertisement) hasa mitandao ya
kijamii kama vile Instagram, Facebook, twiter na Blogs mbalimbali.

Kwa kushirikiana na Sekta binafsi, Serikali inatarajia kuanzisha mfumo wa kidijitali wa kufuatilia na kuhakikisha kodi husika za Serikali zinalipwa kwa wakati. Hii itajumuisha matangazo ya Biashara ambayo huwekwa na watu maarufu (digital influencers) na biashara za mtandaoni zinazofanyika nchini.
 
Bora iwe hivyo maana utapeli umekuwa mwingi sana, mtu anatangaza uhuni mtandaoni na ukioneshwa kilichotangazwa na bei ni vitu viwili tofauti.

naunga mkono hoja, watu wanakuwa na nidhamu na mitandao ya kijamii hususani kutumia mitandao kufanya utapeli wa Bei, bidhaa na huduma.

sasa tutakuwa tunaona matangazo yenye ubora mitandaoni maana uliweka tangazo la ovyo utakosa wateja na tangazo utalipia.


Kwa hili nitakuwa mchoyo wa fadhila na shukrani Kama nisipompengeza Rais Samia na Waziri Nchemba
 
Najaribu kujiuliza serikali italitekelezaje hili?

Mfano YouTube, Instagram, TikTok nk ziko sourced nje ya Tanzania..

Tutalazimika kupata kibali kutoka serikalini ili kuwa na account YouTube, Instagram, TikTok nk?

Mfano Mimi naweza kuweka Tangazo langu kwenye YouTube account inayomilikiwa na mtu aliye nje ya nchi mfano; Kenya, USA nk. Utawezaje kutoza Kodi Tangazo Hilo?

I don't get it...
 
Tamaa zimewazidi Kodi mnazokusanya haziwatoshi mnajaribu kubana kila sehemu...mikataba ya kuwanufaisha watanzania mnaboronga.....kwa nini msiache vijana watafute riziki Bila vikwazo.
 
Najaribu kujiuliza serikali italitekelezaje hili?

Mfano YouTube, Instagram, TikTok nk ziko sourced nje ya Tanzania..

Tutalazimika kupata kibali kutoka serikalini ili kuwa na account YouTube, Instagram, TikTok nk?

Mfano Mimi naweza kuweka Tangazo langu kwenye YouTube account inayomilikiwa na mtu aliye nje ya nchi mfano; Kenya, USA nk. Utawezaje kutoza Kodi Tangazo Hilo?

I don't get it...
Nchi ya hovyo Sana hii.
 
Najaribu kujiuliza serikali italitekelezaje hili?

Mfano YouTube, Instagram, TikTok nk ziko sourced nje ya Tanzania..

Tutalazimika kupata kibali kutoka serikalini ili kuwa na account YouTube, Instagram, TikTok nk?

Mfano Mimi naweza kuweka Tangazo langu kwenye YouTube account inayomilikiwa na mtu aliye nje ya nchi mfano; Kenya, USA nk. Utawezaje kutoza Kodi Tangazo Hilo?

I don't get it...
Nchi ya hovyo Sana hii.
 
Safi wakati hawa wasanii wanaojifanya wapo busy na sanaa uku nchi inaangamizwa na waarabu
 
Back
Top Bottom