Serikali imeshindwa kabisa kudhibiti madereva wao, wanajiona wao wapo juu ya Sheria za barabarani Nchini

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
Ni siku chache tu zimepita tangu itokee ajali ambayo haikuwa na madhara makubwa kati ya basi la mwendokasi na defender ya Polisi.

Picha za tukio hilo zilisambaa mitandaoni na ilivyoonesha wazi kabisa kuwa mwenye kos ani yule aliyekuwa akiendesha ile gari ya Polisi kwa kuwa aliingilia njia ya mwendokasi.

Sijui nini kiliendelea, lakini huo ni mfano wa matukio mengi ambayo yanahusisha magari ya Serikali au taasisi za Usalama ambayo yakiwa barabarani ni kama vile yenyewe yana upekee wa kwake.

Licha ya Serikali kusema mara kadhaa huko nyuma kuhusu madereva wa taasisi hizo kujifanya wao ndio wanajua kila kitu na wao ndio wababe, ni kama hakuna cha maana kilichofanyika kuhusu kubadilisha hali hiyo.

Tukio la jana 14/09/2022 lililoondoa maisha ya watu kadhaa akiwemo Mkurugenzi wa Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora, wapumzike kwa amani ndugu zetu hao, imeripotiwa kuwa dereva wa gari la kiongozi huyo aligomea kusikiliza kile kilichosemwa na askari wa usalama barababarani.

Nimeona wanasema alikatazwa kuingia barabarani kwa kuwa muda huo ulikuwa ni maalum kwa magari makubwa, yeye akabisha kwa madai ana haraka na wanataka kuwahi.

Hivi Serikali imeshindwa kufanya maamuzi magumu kuhusu madereva wao kuwa na tabia ya kutoheshimu sheria za barabarani?

Rais Samia na viongozi wengine wote hili kweli limewashinda au ndio ile kesi ya nyani unampelekea…..

Kuna wakati nawaza au labda madereva wanapata jeuri kwa kuwa wanasapotiwa matendo yao na haohao viongozi wao wanaowabeba?
 
Kwanini Boss alishindwa kumzuia dereva wake afuate maelekezo ya trafiki?
ST, SU, SM, PT, JW, ZT, UT, MT et. al. wako excepted na sheria za usalama barabarani; wao haziwahusu kabisa.
 
Tangu lini dereva wa gari la serikali akaendesha gari bila amri ya boss wake? Ukiona gari la serikali linakimbia hovyo ujue dereva kapokea maelekezo
 
Tangu lini dereva wa gari la serikali akaendesha gari bila amri ya boss wake?ukiona gari la serikali linakimbia hovyo ujue dereva kapokea maelekezo
Kweli, nahisi hilo nalo neno la msingi.
 
Wakianza kufa wao ndo akili inawakaa sawa.

Utaona huko Mbeya vijiko vishafika na kazi imeanza.

Ila hakuna madereva wanaoendesha vibaya kama wa serikali.
 
Kwanini Boss alishindwa kumzuia dereva wake afuate maelekezo ya trafiki?
Yani kutokana na sehemu ile kua ya hatari wameweka utaratibu magari yapite kwa zamu, hivyo waliruhusu magari madogo kisha makubwa, huyu Mkurugenzi alipaki pembeni akanunua viazi, alipomaliza zamu ya gari ndogo ikawa imeisha, ndipo walipo mzuia lkn kwa madaraka yake akagoma kiwa yeye hawezi subiri, wakamruhusu, ndipo alipokutana na hiyo mashine, kulia kjna gari kushoto gari, akakaaa katikati na kupigwa kwa kubanwa katikakati
 
Ni siku chache tu zimepita tangu itokee ajali ambayo haikuwa na madhara makubwa kati ya basi la mwendokasi na defender ya Polis...
Tatizo ni hao viongozi. Kiongozi akisha kalia hzo chuma anaona barabara yake hana wa kumzuia sheria zinatuhusu sisi wao hapana haziwa husu.

Zipo ajali nyingi police, na magari mengi ya serikali ndo chanzo. Hao madereva ukute kapewa amri endesha gari usisimame sasa hapo tunamlaumu dereva tu. Mm naona tuanze na hawa viongozi
 
Hao jamaa wanakwambia kwamba mwendo wa serikali ni masaa 2 au 3 aiseee ukicheki kipande ni cha 350km...
 
Ni siku chache tu zimepita tangu itokee ajali ambayo haikuwa na madhara makubwa kati ya basi la mwendokasi na defender ya Polisi.

Picha za tukio hilo zilisambaa mitandaoni na ilivyoonesha wazi kabisa kuwa mwenye kos ani yule aliyekuwa akiendesha ile gari ya Polisi kwa kuwa aliingilia njia ya mwendokasi.

Sijui nini kiliendelea, lakini huo ni mfano wa matukio mengi ambayo yanahusisha magari ya Serikali au taasisi za Usalama ambayo yakiwa barabarani ni kama vile yenyewe yana upekee wa kwake.

Licha ya Serikali kusema mara kadhaa huko nyuma kuhusu madereva wa taasisi hizo kujifanya wao ndio wanajua kila kitu na wao ndio wababe, ni kama hakuna cha maana kilichofanyika kuhusu kubadilisha hali hiyo.

Tukio la jana 14/09/2022 lililoondoa maisha ya watu kadhaa akiwemo Mkurugenzi wa Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora, wapumzike kwa amani ndugu zetu hao, imeripotiwa kuwa dereva wa gari la kiongozi huyo aligomea kusikiliza kile kilichosemwa na askari wa usalama barababarani.

Nimeona wanasema alikatazwa kuingia barabarani kwa kuwa muda huo ulikuwa ni maalum kwa magari makubwa, yeye akabisha kwa madai ana haraka na wanataka kuwahi.

Hivi Serikali imeshindwa kufanya maamuzi magumu kuhusu madereva wao kuwa na tabia ya kutoheshimu sheria za barabarani?

Rais Samia na viongozi wengine wote hili kweli limewashinda au ndio ile kesi ya nyani unampelekea…..

Kuna wakati nawaza au labda madereva wanapata jeuri kwa kuwa wanasapotiwa matendo yao na haohao viongozi wao wanaowabeba?
Madereva wa serikali na taasisi zake zote wanajiona wako juu ya sheria, ukiangalia asubuhi magari ya viongozi wa taasisi nyeti za serikali zote zina vimulimuli wanavunja sheria zote za barabaranibinafsi sijaona umuhimu wao wa kutaka wapishwe. Magereza na JWTZ wote hao ndio wanaongoza kuvunja sheria. Ningeshauri magari ya JWTZ yafuate sheria au wadamke asubuhi sana ili wawahi huko wanakoenda kwani barabara za uma ni kwa ajili ya wananchi wote wafuatao sheria ili watimiza majukumu yao ya kila siku, tungekuwa na vita ndio wangepewa kipaumbele
 
Back
Top Bottom