Serikali iache kunyanyasa watumishi, Mfumo wa PEPMIS hauna uhusiano na mshahara wa Mtumishi alioufanyia kazi mwezi mzima

kichongeochuma

JF-Expert Member
Jan 21, 2024
315
567
Nashindwa kuelewa hawa viongozi huwa wana tumia akili gani katika maamuzi yao.

Msidhani kila mtu anaishi mtumba hapo dodoma muwe mnafanya tafiti za kina kabla ya kuleta hiyo mifumo yenu kwanza.

Mfumo wenu unahitaji angalau 3G au H+ Internet speed ili angalau ufanye vizuri wakati huo kuna watumishi wapo vijijini huko ambako hadi leo wanapata internet yenye kasi ya GPRS na EDGE (hilo nina uhakika nalo na ushahidi ninao).

Msitumie ubabe kwenye hili mtatesa watumishi sana, mfumo bado una shida na si rafiki kwa mazingira yetu mnalazimisha nchi kuingia kwenye teknolojia ambazo ki msingi si rafiki kwa kwa aina ya watu na miundo mbinu kifupi hamjawaandaa watumiaji wala miundo mbinu.

Mtumishi ataesimamishiwa mshahara wake alio utumikia mwezi mzima kutokana na majukumu yake kwa mujibu wa makataba wake wa kazi kwa kisa hajajiunga na PEPMIS anione PM kwa masaada wa kisheria.
 
Ndiyo madhara hayo ya kuwa na watu wenye elimu ya kukariri madesa.
Hii nchi ina shida kubwa sana hasa uwezo wa baadhi ya viongozi kuchambua mambo kwa kina, nahisi watu wenye uwezo wa kuchambua mambo kwa kina wananyimwa nafasi au huenda hawapo hiko juu maana jambo kama hili lili hitaji maandalizi makubwa sana ya kimiundombinu kwanza, kuandaa wahusika watakao tumia huo mfumo maana kuna watu hawajawahi kutumia wala kununua hizo smartphone maana sio takwa la mkataba wa kazi na pia kutokana na aina ya mazingira wanayo fanyia kazi sasa unamsimamishiaje mshahara mtu huyo wakati majukumu yake ya kiutendaji yaliyopo kwenye mkataba wake wa kazi kayatekeleza na anasubiri ujira wake.?
 
Inawezekana Hilo ni tangazo Tu la ku speed up watumishi kujisajili, na pia Kwa kutumia tamko Hilo ni rahisi kujua areas of difficulties, ili kupata alternative ways za kusolve.

Naamini haitawakatia watumishi Kwa kosa lililo nje ya uwezo wao, especially waliopo katika remote areas.
 
Nashindwa kuelewa hawa viongozi huwa wana tumia akili gani katika maamuzi yao.

Msidhani kila mtu anaishi mtumba hapo dodoma muwe mnafanya tafiti za kina kabla ya kuleta hiyo mifumo yenu kwanza...
Huyu mbawene sjui kala maharagwe ya wapi.

Katika siku alizoongea pumba ni leo.

Na soon ataondoshwa kwenye hyo wizara.

Vinginevyo ataleta taharuki na kusababisha hata mgomo.

Mama mtoe huyu waziri haraka sana
 
Kuna haja ya jf kuleta jukwaa la watumishi, mtoa mada kaandika kana kwamba wote humu tunajua pepumiss maan yake ndio Nini
emoji848.png


Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile ap
 
Walimu pamoja na kuwa na vishkwambi bado wanashindwa kujisajili kwenye huu mfumo?

Hila huu ni uonevu mkubwa tanzania tunashida ya matumizi ya hii mifumo na huu mfumo umekuwa ukiwasumbua sana watumishi sio haki kuwanyima mshahara eti kisa hawajajisajili
 
Walimu pamoja na kuwa na vishkwambi bado wanashindwa kujisajili kwenye huu mfumo?

Hila huu ni uonevu mkubwa tanzania tunashida ya matumizi ya hii mifumo na huu mfumo umekuwa ukiwasumbua sana watumishi sio haki kuwanyima mshahara eti kisa hawajajisajili
Hivyo vidude kwanza wana vilalamikia sana ni vibovu vingi havishiki mtandao vibakufa hovyo tu
 
Back
Top Bottom