Series (Special thread)

Nyie mnaijua Treadstone Nyie
Moja kati ya series bora kabisa mimi kuwahi kuangalia.

Series iliyobeba watu wa mataifa mengi tofauti tofauti.

Director alinimaliza alipo amua kutembea na matukio ya miaka tofauti pamoja mwanzo mwisho, nilizoea kuona unaenda na tukio likiisha unaamishwa miaka ila hapa yalitembea pamoja.

Hasara yake ni pale walipo hairisha kutoa season 2, daah niliumia sana iyo kitu ilihitaji mwendelezo.
 
Nimesoma synopsis yote Wikipedia, naona kama nimeiona tayari
 
Series: Gangland
Year: 2021 -
Genres: Action, Crime, Drama
Language: French
Country: France
Rates: 7.1/10, Tv-Ma

Ufaransa na wao wana jambo lao hili hapa, Mzigo mtamu sana. Stori yake ni Mwamba yeye ana timu yake ya wezi lakini hawaibii watu wao ni wizi wa Mamilioni ya pesa.

Deal lao la mwisho kupiga ilikua ni kuiba Gold, Na ni Ma Pro kweli kweli. Sasa ana Kajomba kake kabinti, Kumbe kana michezo ya chini chini kudokoa dokoa vitu na timu yake flani.

Sasa kuna siku wakadokoa ambavyo havitakiwi kudokolewa, Yaani walibeba Cocaine alafu waka Plan iuzwe msala ukaanzia hapo. Sitaki kuongea mengi, Ila kwa ufupi jamaa kutokea kufanya mission za kuiba vitu inageuka now kua Mission ya kumuokoa Mjomba.

Mzigo una Eps 06 tu za maana sana.
 
Wakuuu natamani kupata series kali kma money heist wenye kunijuza tafadhali
 
Hi kali aise ndo nimeimaliza saivi.

Japo lian nazingua sana aise
 
Narudisha shukrani kwa yule alienishauri kuiangalia SEE.

Ubarikiwe sana.

Kwa wale mnaoendelea na season 2, pale ilipofikia ni mwisho?
Maana sitaki niishie kwenye utamu, nataka nikiangalia nimalize moja kwa moja.

Uvumilivu wa kulaza viporo huwa sina kabisa.

Mfano mzuri tu ni namna 24 ilivyonifanya nikeshe 2 days in a row.
 
Mzigo mzuri huo na season 3 itaendelea mwakani tuombe tu covid -19 isishambulie tena kama kipindi cha nyuma maana iyo season 1 ilitoka 2019 lakini covid ilivyokuwa kali wakapotezea kushoot kwa muda ndio season 2 ikatoka mwaka huu
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…