Vyuma vyangu 5 vya series vikali kuwahi kuvitazama tangu nipate kujua tofauti ya series na movies:
1. BREAKING BAD 👑
Hii kama kungekuwa na mashindano ya series kali kwenye Galaxies, Milk Way Galaxy tukiipeleka hii kazi,
WE ARE NOT IN DANGER, WE ARE THE DANGER, tunanyakua tuzo mapema kabisa.
2. SHERLOCK
Nani kama Sherlock Holmes!?
Hii mali ni kisanga sana mzee, fanya uhalifu uwezavyo, tukimkodi Sherlock Holmes hautoboi, lazima tukuweke nyuma ya NONDO.
3. RICK AND MORTY
Oyaaa weeeeh, tulia hivyo hivyo. Maana najua utashtuka!
Usiseme cartoon ni mbanga za kitoto, maana nitakuona ni mshamba zaidi ya Bartimaeous!
Rick Sanchez, best scientist in the galaxy, huyu mzee ni mwanafalsafa konki, kila akiongea anatema facts!
Wazee wa kataa ndoa mtaipenda hii kazi, humu ndani Rick Sanchez anakuambia
Weddings are basically funerals with cakes!
Unapenda Sci-fi? Unapenda comedy?
Changamka tafuta hiki chuma uenjoy wewe!!!!
4. BAND OF BROTHERS
Unajifanya unapenda sana kazi za majeshi na bado haujakiona hiki chuma!? Aaaah, basi weh Zuchu tu!
Humu ndani zinapigwa shaba mpaka Zambia wanaona wivu!!!
Kutana na E-Coy, kombania iliyobeba matumaini ya kikosi cha jeshi la Marekani katika WW II.
Wale wazee wenzangu wa NO REFORM NO ELECTION, kabla hatujaingia barabarani chukueni huu ujumbe kutoka kwenye Band of Brothers:
The only hope you have is to accept the fact that you're already dead. The sooner you accept that, the sooner you'll be able to function as a soldier is supposed to function: without mercy, without compassion, without remorse. All war depends upon it.
5. TRUE DETECTIVE
Eeeh bwana, hiki chuma nimekiweka hapa namba 5 kwasababu nimetazama season 1 tu, hivyo hii sababu inafanya hiki chuma kiwe cha mwisho kwenye rank zangu za vyuma vitano(5) matata nilivyowahi kuvitazama.
Ingekuwa series zote zinaishia season 1, basi niseme hakuna kigongo cha kuchuana na kigongo hiki.