Nathani wana jamvi la muhimu ni kumshauri Diamond kama kweli alijikwaa akafanya lolote la kuwakwaza aliekuwa nao zamani,ni suala kurudi tu na kukaa na kuyamaliza,kwani wanaokupandisha ndo wanao kushusha hao hao vijana ndo walikua wanambeba na kumshangilia bwana Almas,unakumbuka alipo kuja kwenye msiba wa kanumba gari lake lilikua linasukumwa na leo anazonewa,sasa kikazi na kimaisha si vizuri ni ishara ya kuanza kupoteza mashabiki,tukumbuke hata huko nje wamemjua kwa kuwa Watanzania ndo wamempa promo,la muhimu bwana Nasibu jirudi kwa mashabiki wako kama kweli ulifanya dharau yeyote basi wewe ni binadamu kaa chini maliza,sisi wenye akili tunataka wewe na kiba mfanikiwe tupate burudani,malizeni haya.