Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Alivyobeba vyombo mara ya mwisho akajiapiza kumuacha.
Imagine,mwanamke amesomba kila kitu hadi vigodoro..mumewe analala chini
Akaondoka zake.

Lahaula hatujakaa sawa mwezi huo umepita mara vyombo vinarudishwa..wanaanza kufunga ving'amyzi upya.
Kwa kweli nilishindwa kujizuia kucheka.

Yaani kaka Hana shida kabisa,ila mwanamke ni kichomi jamani uwiiii...
Ukiwaona kama hawaendani kabisaa..dada macho juu na anataka mambo makubwa ambayo Kwa sasa mumewe hana.
With such a big call; Mtumishi wa Mungu ilikuwaje akachagua mwanamke wa aina hiyo hata kama ke alifake kuwa mwema? Ila Watumishi nao wana mapito jamani, Mungu awasaidie
 
Nakemea na napinga vikali hoja hii Mimi ni mtumishi wa jehova sinaga mambo ya dunia!. Kama ameshindwa kukutongoza asituseme wengine akirogwa aje aanze kusema kimeenda kimerudi!.
Mtumishi wa Jehova
 
Kuna work Mate mmoja bana alilazimisha ndoa wakafunga ya serikali na aliyemuita mumewe...
Ilikua 2016 kaona madam A ameshaolewa B ameshaolewa C ameshaolewa...akamwambia mtu wake nimebaki madam Mimi tu staff akafosi kamlazimisha mwanaume aliekuwa nae kipindi hiko nae alikua mwalimu mwenzie mpaka wakaenda kufunga ya serikali ilimradi tu asibaki madam pekeake ambae hajaolewa Wakafunga. Balaa likaanza ikawa ni visa na vituko tu humo ndani ikafikia pahala likizo kila mmoja anaenda anakojua yeye na hakuna kuulizana wala kumaindi mwenzio likizo ikiisha wanarudi wanaendelea na drama ndoani...
Ikafikia hatua kila mmoja akawa analala chumba chake hali ikawa mbaya zaidi mwanaume akawa analeta wanawake humohumo ndani kwenye chumba chake.
Mbona mwanamke aliomba uhamisho ghafla bila kutaka. mpaka leo wana hiko cheti cha serikali hawajaenda kuvunja ndoa ila kila mmoja anaendelea na mahusiano mengine huko aliko!!
Halafu alikua yule mtu wa show off masaa yote ofisini ni "Mimi me wangu Mimi mme wangu.. mimi na mme wangu Mimi na mme wangu utadhani wengine hawana waume au hawajaoa na kuolewa!!!! Mbaya zaidi sijui tuseme mwanaume hakumpenda au sijui hata tusemeje.
Mtu mmeamua kufunga ndoa nyie kama nyie wawili badae wewe mwanamke ukampeleka mumeo kumtambulisha kwenu wanamtambua ila yeye mwanaume hana hata dalili ya kukupeleka kwao ukiuliza utanipeleka lini unajibiwa acha kiherehere cha kutaka kujulikana hapo mwanaume huyo ana watoto wawili alishazaa na wanawake wawili tofauti huko Nyuma kabla hawajakutana na baadhi ya likizo eti anaendaga huko kusalimia watoto zake anakaa likizo nzima ikiisha anarudi kwako !! Mshahara wote hana habari za kupanga maendeleo nawewe ndiokwanza anaangalia watoto wake wewe unabaki tu kulia nanafsi yako! Alihama bila kupenda mbona!
So sad
🤣🤣🤣🤣
 
Ni mkorofi ana fujo zake lakini tulimuonea huruma kiukweli!! Inafikia wakati mmetoka kazini mnaongozana kwako tu anakaaa weee anaangalia Muvi ikikaribia Usiku ndio anawaza Kurudi kwake kwenye balaa!
Au weekend ilifikia wakati anatoka kwake asubuhiiiii anabadilisha tu vituo akichoka kwa huyu anaenda kwa yule kupiga story kumaliza weekend masaa yaende!!
 
Back
Top Bottom