Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Hivi ni kwa nini? juzi juzi hapa kuna classmate wangu nilikutana nae ktk stori ananiambia kaolewa na ana watoto wawili mimi vipi nikamuambia sijaolewa wala sina mtoto akaanza kunisema tatizo nachagua sana imagine ni mwanamke mwenzangu ananisema hivyo. Sijui hii kitu inasababishwa na nini nachukia.

Tulia mama kula maisha...

Mumeo yupo atakuja kwa wakati Mungu aliopanga...
 
Ukiacha watu wakupangie cha kufanya kwenye maisha utajikuta unaingia pabaya, kwenye ndoa hamna kuwahi wala kuchelewa muda ukifika utaingia tu...

Na ukiwa desperate unaweza usiolewe au ukapata mtu ambaye si sahihi ..

Oh yeah ndoa haihitaji haraka ..
Binadamu hawawezi kuacha kuongea kabisa .
Binafsi sina haraka ndo kwanza sina habari wacha tu waongee .
 
Almost kila mtu anakuwa na ndoto, maono, matamanio, matarajio n.k.Na tunaweka na timeline kabisa kwamba hadi muda huu niwe na 1,2,3,4. Sasa wakati unapanga mambo yako, usisahau kuwa Mungu na yeye ana mipango yake tena ambayo tunaamini na kujua kwamba ni myema kuliko ya kwetu. Ikitokea mipango yako haijakamilika kibinadamu lazima ujisikie vibaya; lakini usije ukaishia kuwa mlalamishi na mnyonge kwa sababu hujapata vitu fulani; utaishia kuwa an ingrate. Tatizo letu huwa tunahesabu sana baraka za wengine ambazo tunaziona ni kubwa zaidi; tunasahau kuhesabu baraka zetu ambazo nazo kuna watu wanaziangalia na kuzitamani. Comparison is the thief of joy.

As a result tunajikuta tunakuwa watu wa kulalamika na desperate. Kama ambavyo Mimi mzazi sipendi mtoto ambaye atakuwa hanishukuru, ananilalamikia tu kwa sababu ya kitu fulani ambacho sijaweza kumpatia; definitely hata Mungu anachukizwa na watoto wake wasio na shukraniz bali walalamishi. So utaishia kulalamika tu badala ya kuenjoy baraka ambazo Mungu amekupa. "Praise and be Raised, Complain and Remain.

Ubaya zaidi binadamu huwa haturidhiki; Leo utahitaji kitu fulani desperately, kesho ukishakipata unataka tena kitu kingine ambacho huna. Ingawa kwa wanawake ndoa ndiyo kama lifetime achievement kwetu; Leo utaililia wee, ukishakipata unahamia kwenye tamanio la kuwa na watoto, then mume ana uwezo kiasi gani mbona mume wa mwenzio kamfanyia hiki mkewe/familia, then watoto wanasoma shule gani, watoto wa marafiki zenu wanasoma shule fulani, mara nyumba and the list goes on. So kwenye maisha most likely hakuna siku utakuwa na Kila kitu unachokitaka; ni wewe unaamua kuridhika na kuvienjoy vichache ulivyobarikiwa.

Kubwa zaidi we have to believe and honor God's time. Yeye atakupa hiyo ndoa kwa wakati ambao anaona ni sahihi zaidi kwako. Inawezekana ungekuwa umeshaolewa kwa wakati ambao unautaka wewe; leo ungekuwa mjane au divorcee tayari. Na hata Mungu akiamua kutokukupa ndoa kabisa; shukuru tu; ni wangapi ambao ndoa zao zimekuwa sababu za vifo vyao? Naamini wangejua yaliyopo mbele yao, wangeamua tu kubaki kuwa single. Tujifunze kuwa watu wa shukrani aisee

Kuna a certain sermon by Joel Osteen kuhusu kuwa na positive perspective. Alisema wengi wetu tunaona maisha yetu like a boring routine; unaamka Kila siku, unakwenda kazini/biashara then unarudi nyumbani. Kila siku inakuwa hivyo kiasi kwamba tunachukulia kama ni kitu cha kawaida tu, nothing exciting. Lakini kumbe hiyo boring routine ni baraka kubwa sana; wangapi wanalala na hawaamki tena, au wakaamka wakakuta baadhi ya viungo havifanyi kazi; wangapi wanatafuta kazi/biashara ambayo kwako imeshakuwa boring? So kumbe ukiamua kuwa mtu wa shukrani; una vitu vingi sana vya kukufanya ushukuru. Kuna vitu tunavi-overlook sana, lakini ni vitu vya msingi mno, ni baraka kubwa mno kwetu;

1. Umebarikiwa upendo wa familia yako, ndugu marafiki. Una wazazi, kaka, dada, bibi n.k. Ni kama kitu Cha kawaida tu kila siku; ila siku akiondoka huyo ndugu ndiyo utagundua kuwa umepoteza baraka kubwa kiasi gani. Mimi binafsi nikisikia mtu anaita "baba" na baba yake akamuitikia; natamani nimwambie ni kiasi gani amebarikiwa kwa sababu ni baraka ambayo mimi sina tena. Kuna moments za furaha sana unabarikiwa nazo, lakini unaishia kuwa na simanzi like I wish baba angekuwepo hapa.Though I'm grateful niliienjoy baraka yangu to the fullest.

2. Afya. Ukiwa na afya njema then uone watu wanaoumwa serious; utajiona wewe ndiyo mbarikiwa dunia nzima. Ukipata changamoto ya kiafya; haki unaweza kumwambia Mungu chukua vyote niachie tu afya yangu.
Kuwa mzima, unapumua vizuri; ni baraka tosha kabisa, unapaswa kushukuru.

3. Peace of mind. Kuna watu Wana almost Kila tunachokitamani lakini hawana amani ya moyo. Kuwa na amani ya moyo aisee ni baraka kubwa sana, and no amount of money can buy that.

So ukiamua kuwa positive kila kitu utakiona kwa upande chanya sana. So unaweza tu kuchukulia kuwa huu muda ambao hujaolewa ndiyo muda mzuri wa wewe ku-add value kwenye maisha yako. Tangu ukiwa mdogo una ndoto na maono yako binafsi, ndiyo muda wa kuyatimiza sasa. Ukishaolewa mambo yanabadilika kwa kiasi fulani; mnaanza kutembea kwenye maono ya mume sasa na sio ya kwako (kwa % kubwa). So kuna vitu au ndoto zako ambazo zitamezwa na maono ya mume.

Pia una wakati mzuri wa kufanya chaguo sahihi la mume; kiakili unakuwa umekomaa sana. Mimi binafsi naamini ningeolewa in my early 20s ningekuwa divorcee sasa hivi. Kuna vitu vingi vya msingi ambavyo ningevi-overlook na vingekuja kunitesa sana; what matters to me at that time ni kwamba tunapendana. Lakini sasa hivi ndiyo naona; love alone is not enough; kuna vitu vingi sana vya kuviangalia. With age vigezo vyangu (vya msingi) vilikuwa vinaongezeka kwa kweli; kwa sababu akili yangu ilikuwa imekomaa kuchanganua mambo; unayaangalia mahusiano kwa jicho la kesho na kesho kutwa na sio leo hii ya tunayosema tunapendana.

Ni sawa kutamani au kuomba vitu fulani ambavyo hatuna; but tusijistress sana juu ya tusivyonayo hadi tukakufuru. Tuwe watu wa shukrani. Sio Kila tunamwendea tu Mungu kumuomba, hakuna siku tunamwendea kwa shukrani na sifa.

C.c Carleen upitage na huku

Sent using Jamii Forums mobile app

Umemaliza...

Barikiwa sana..
 
Mimi ni mvivu sana kutembea.
Kwahiyo sijulikani sana...ila hata nikitoka, Kwa wanaonijua sidhani kama wanaweza kuuliza maana nipo siriazi mno


Kazi unayo

Anha sawa
Mimi natembea ila si sana halafu mimi rahisi kuongea na watu hivyo ukinianza tu lazima nikujibu hahaha .. I enjoy mingling muda mwingine .
Ukauzu naufanya mtaani huku napoishi ila ukinikuta nje huko naongea huyo
 
Aisee inakera muda mwingine ukute sasa hata huchagua watu kihivyo .. upo zako tu unasubiri aje anayefaa tu .

Ni fikra tu za watu ,Halafu wao wanahisi wanaume ni waoji kumbe si wote .. wengine Ni wapitaji tu .

Wanawake inabidi tutiane moyo ila inakuwa otherwise kama ishu hii ya lulu na Mange aise sio fair kabisa

Kuchagua lazima uchague sio kila mwanaume anafaa kuwa baba wa familia...
 
Ukiacha watu wakupangie cha kufanya kwenye maisha utajikuta unaingia pabaya, kwenye ndoa hamna kuwahi wala kuchelewa muda ukifika utaingia tu...

Na ukiwa desperate unaweza usiolewe au ukapata mtu ambaye si sahihi ..
Kuna work Mate mmoja bana alilazimisha ndoa wakafunga ya serikali na aliyemuita mumewe...
Ilikua 2016 kaona madam A ameshaolewa B ameshaolewa C ameshaolewa...akamwambia mtu wake nimebaki madam Mimi tu staff akafosi kamlazimisha mwanaume aliekuwa nae kipindi hiko nae alikua mwalimu mwenzie mpaka wakaenda kufunga ya serikali ilimradi tu asibaki madam pekeake ambae hajaolewa Wakafunga. Balaa likaanza ikawa ni visa na vituko tu humo ndani ikafikia pahala likizo kila mmoja anaenda anakojua yeye na hakuna kuulizana wala kumaindi mwenzio likizo ikiisha wanarudi wanaendelea na drama ndoani...
Ikafikia hatua kila mmoja akawa analala chumba chake hali ikawa mbaya zaidi mwanaume akawa analeta wanawake humohumo ndani kwenye chumba chake.
Mbona mwanamke aliomba uhamisho ghafla bila kutaka. mpaka leo wana hiko cheti cha serikali hawajaenda kuvunja ndoa ila kila mmoja anaendelea na mahusiano mengine huko aliko!!
Halafu alikua yule mtu wa show off masaa yote ofisini ni "Mimi me wangu Mimi mme wangu.. mimi na mme wangu Mimi na mme wangu utadhani wengine hawana waume au hawajaoa na kuolewa!!!! Mbaya zaidi sijui tuseme mwanaume hakumpenda au sijui hata tusemeje.
Mtu mmeamua kufunga ndoa nyie kama nyie wawili badae wewe mwanamke ukampeleka mumeo kumtambulisha kwenu wanamtambua ila yeye mwanaume hana hata dalili ya kukupeleka kwao ukiuliza utanipeleka lini unajibiwa acha kiherehere cha kutaka kujulikana hapo mwanaume huyo ana watoto wawili alishazaa na wanawake wawili tofauti huko Nyuma kabla hawajakutana na baadhi ya likizo eti anaendaga huko kusalimia watoto zake anakaa likizo nzima ikiisha anarudi kwako !! Mshahara wote hana habari za kupanga maendeleo nawewe ndiokwanza anaangalia watoto wake wewe unabaki tu kulia nanafsi yako! Alihama bila kupenda mbona!
 
Kuna work Mate mmoja bana alilazimisha ndoa wakafunga ya serikali na aliyemuita mumewe...
Ilikua 2016 kaona madam A ameshaolewa B ameshaolewa C ameshaolewa... alafosi kamlazimisha mwanaume aliekuwa nae kipindi hiko nae alikua mwalimu mwenzie mpaka wakaenda kufunga ya serikali ilimradi tu asibaki madam pekeake ambae hajaolewa Wakafunga. Balaa likaanza ikawa ni visa na vituko tu humo ndani ikafikia pahala likizo kila mmoja anaenda anakojua yeye na hakuna kuulizana wala kumaindi mwenzio likizo ikiisha wanarudi wanaendelea na drama ndoani...
Ikafikia hatua kila mmoja akawa analala chumba chake hali ikawa mbaya zaidi mwanaume akawa analeta wanawake humohumo ndani kwenye chumba chake.
Mbona mwanamke aliomba uhamisho ghafla bila kutaka. mpaka leo wana hiko cheti cha serikali hawajaenda kuvunja ndoa ila kila mmoja anaendelea na mahusiano mengine huko aliko!!
Halafu alikua yule mtu wa show off masaa yote ofisini ni "Mimi me wangu Mimi mme wangu.. mimi na mme wangu Mimi na mme wangu utadhani wengine hawana waume au hawajaoa na kuolewa!!!! Alihama bila kupenda mbona!
Maskini pole zake madam. Ndoa sio jambo la kukurupuka wala kulazimisha inatakiwa itokee wote mmeridhiana kuingia huko.
 
Maskini pole zake madam. Ndoa sio jambo la kukurupuka wala kulazimisha inatakiwa itokee wote mmeridhiana kuingia huko.
Alivyokuwa muongeaji sasa!!!! Ni Yule wa kuwananga wenzie yani aibu ilikua yake mbona sasahivi tangu ahame ameshatutambulisha wanaume kama watatu hivi mwezi huu unatambulishwa huyu mwezie ujao yule.... kiukweli ndoa sio mchezo sio suala la kukurupukia ndoa zina mengi mno!
 
Yaani kila kitu kina faida na hasara.
Mtu akiwahi ndoa anakuwa na faida ya kuzaa mapema lakini wengi wao akili inakuwa bado haijakomaa kuweza kubeba ndoa.

Wanandoa wanaochelewa kuoana watapata watoto late lakini wengi wao akili zinakuwa zimeshakomaa..Kuna namna wanajitambua.
Kabisa na usiolewe sababu fulani kaolewa au nawaona wenzangu angalia nafsi yako pia Omba Mungu akupe kulingana na hitaji la moyo wako bila hivo hutoboi
 
Back
Top Bottom