anaejua dawa ya Ulcers hata ya kienyeji yaani kwa mwezi haipiti mara mbili lazima nikachomwe sindano
Pole kwa unayopitia,hope utakuwa sawa..
Mimi nimeumwa sana nilifika hatua nikaingizwa mpira wa camera mara nne...
Walichukua kinyama tumboni wakakituma maabara Nairobi na baadae nilianza tiba ila sikupona pia.
Nilikua sina raha ya maisha,pesa napata ila siwezi kula ninachokipenda...
Ni Mungu tu ndio anajua niliyopitia siwez hata simulia,kila dawa nilitumia
Nili blend makabichi..
Nili blend viazi mbatata..
Nili blend bamia
Habat soda
Dawa za kienyeji
Helgo kit zaidi ya mara 8
Madawa ya kisuna. .
Kifupi nimekunywa madawa mengi sana.
Ila kuna msamaria humu humu jf aliniambia atanipa dawa kama nikipona nitamlipa, nisipopona bhasi(ila alianza kunidai hata sijamaliza dozi

).
Ilikua ni ghali ila naamini ndio iliponya japo baada ya kupima nilionekana niko sawa ila kuna vyakula nilikua bado naogopa kula. Mfano dagaa,maharage,pilau,limao,ndimu,machungwa,nanasi n.k
Nashukuru Mungu sasa hivi nimepona nakula kila kitu, japo kuna vingine sili nimevichukia kabisaa...
Cha msingi hata bia sasa nakunywa.
Kwa kweli nilijaribu kugundua ameweka nini kwenye ile dawa niliambulia ni asali ya nyuki ndogo na mdalasini,vingine sikuweza kufaham na aligoma kunifundisha,kama angelinifundisha hakika kila anayeumwa nami ningemfundisha bure mana najua khali wanazopitia.
By the way hio asali na mdalasini imesaidia kuwapa nafuu baadhi ya watu ambao nimekua najua wanaumwa vidonda vya tumbo lakin hawakupona kabisa kama mimi.
Ushauri wangu jaribu kutumia na wewe japo inavuruga tumbo,ukianza na kijiko kidogo cha chai nusu saa kabla ama baada ya kula mara tatu kwa siku na kila ukipata nafuu ongeza kijiko cha pili hivyo hivyo mpaka vifike vijiko vitatu kabla ama baada ya kula kwa mda wa mwezi mmoja..
Pia uendele kutotumia vyakula hatarishi then utatujuza khali yako...
I wish you quick recovery.