Mimi ni yule mmoja, kati ya wale kumi,
Uliowaponya ukoma, kwako nimerudi
Wale tisa sijui,
Ila mimi nimekuja kusema Asante
Najiuliza, Nikulipe nini, kwa yote ulionitendea mimi,
Baba ni mengi, siwezi lipa hata kwa senti
Natafuta namna nzuri ya kukushukuru ninakosa,
Natafuta maneno mazuri ya kukushukuru ninakosa.
Ee Baba,
Nikulipe nini, nikulipe nini?
Uliyonitendea ni mengi,
Siwezi kuhesabu
Ila nina neno moja,
ASANTE (x5)
Nachojuaga, huwa unaongezaga
Kama ukimpa mtu kitu alafu akakushukuru
Nachojuaga, huwa unaongeza, zaidi.
Sikushukuru tu kwa haya uliyotenda,
Ila, Hata kwa yale ambayo hujayatenda
Huku nikiamini, Shukrani ni sauti ya imani
Fedha (Haitoshi kukushukuru)
Dhahabu (Haitoshi kukushukuru)
Ee Baba
Nikulipe nini, nikulipe nini
Ulionitendea ni mengi,
Siwezi kuhesabu
Ila nina neno moja,
ASANTE (x2).
Shukrani imebebwa kwenye neno moja,
ASANTE (×4)
View attachment 2054922