Umebonga points sana chalii wa kwangu. Achana na hizo nguchiro zije kupata watoto. Halafu watoto wao wanajisiwe tangu wakiwa wadogo. Ufike umri wajikute wana addiction tayari tuone kama watawanyonga.
Wanafiki sana hawa watopolo. Yaani ni wanafiki wa kiwango cha lami. Wao ni wasafi kinoma hawana dhambi.
Kama ambavyo kuna watu wameumbwa abnormal (wenye ulemavu wa namna mbalimbali) pia wapo ambao wana hormonal imbalance katika viwango vya hali ya juu. Dawa sio kuwatukana eti na kujifanya wakali kwao. Tuwaombee na tuongee nao kistaarabu tu maana vitu vingine ni nature triggered.
Hivi katika hali ya kawaida wewe mwanaume utakubali kuwekwa nyama na mwanaume mwenzio? Sasa kama unaona ni kitu strange kwanini unadhani ni wewe tu unaona hivyo. Kwanini usiwaze nini kilitokea mpaka huyu mmoja akaanza hiyo mambo? Au wewe ni unique kinoma yani kwamba unazi senses za kutosha sana than others.
Acheni upumbavu. Kemeeni dhambi lakini kwa namna ambayo inajenga. Ukimtenga mdhanbi umemsaidia nini? Nyie masela nimewadharau kinima kubabake walay
Hakika ubarikiwe sana una maneno ya busara na hekima mno.
Unajua napenda kuwa mkweli siku zote, ushoga unasambazawa na mabasha, tena wengi wao wapo ktk ndoa zile takatifu.
Nina siri na ninajua mengi ila ngoja hili niliweke hapa.
Wakati naingia chuo 1St yr, nlibahatika kupata friends wawili wote n ke, urafiki wetu uko hadi sasa, namaanisha n real friends, sasa ktk m1 wapo kumbe alikua na rafiki gay ambaye walisoma wote o level, kwa sasa yuko chuo TIA Dar, sasa ktk urafiki wetu siku 1 rafk angu huyu akanambia tutoke, obvious mie sio mtu wa kutoka, nkamkatalia nkamuambiaje tukutane chuo tyuuh.
Basi nlivofka chuo naye alivokuja pale nkaona kaongozana na huyo mtu, by the way nlvomuona tyuuh nkajua uhalisia wake, tukapiga story pale na kucheka na nn, then tukatawanyika,
Baadae yule gay alinitafuta kwa cm ili niwe rafik ake wa karibu skuona vibaya, bas ktk kujuana kiundani nkaja kugundua yupo ktk mahusiano na mwanaume m1 ambaye n mfanya kazi wa bank 1 kubwa pale posta, pia ni mume wa mtu na baba wa watoto wawili wote wa kiume. Na ndoa ya kanisani na mkewe ni mwalimu wa sec maeneo ya tabata. Huyo mwanaume kampangia apartments huyu gay yaan km n mchepuko au nyumba ndogo.
Yule gay nkawa nazungumza nae iv je mke wake akijua wee ndo unaeharibu ndoa yake, tena sio mwanamke n mwanaume atajisikaje? Na atakufikiriaje wee? Nkawa naendelea kumuhoji huogopi kurogwa? Kuundiwa majambazi je? Kudhalilishwa? Majibu yake yalinifanya niwe mpole ila nkawa sichoki kuzungmza nae, maana n mtata afu ana zile nyodo za shombo ni mwenyeji wa Tanga, nilimuambia wazi kua gay sio tatzo na sikulaumu, ila mtu uliyenae sio sahihi kwako, mbna vijana na watu wasiioa wako wengi? Huko chuoni kwenu hakna wavulan wa wee kua nao? Km hakna kwanini usitulizane kwani usipokua ktk mahusiano utapungukiwa kipi? Lakini majibu yake sasa kilanga kiliniisha.
Kiukweli nilijisikia vibaya sana tena mno, nkamuuliza wee una dada? Akanijibu yes nkamuuliza wameolewa? Akanjjibu yes, nkamuuliza utajisikiaje shemej ako anamfanyia dada ako km binti wa watu anavofanyiwa kupitia wee? Alichonijibu sasa nilkua hoi, yaan nlichoka, bas sku zikawa zinaenda, sku hyo akaniita kwake nimtembelee, nlivoenda nkamkuta yupo na huyu mwanaume wapo sebulen wanatazama TV,
Nkaishia kusalimiana nao na baadae nkaondoka muda huo huo,
Kumbe huku nyuma yule mwanaume ana muuliza taarifa zangu yule gay wake, wakaelezana wenyewe mpaka walipotosheka, sasa kumbe yule mwanaume alichukua cm ya gay wake na kuchukua no yangu,
Siku hiyo nipo home jioni cm inaita kuchek no ngeni, huwa sipokei no ngeni nakataa na kutuma text kuuliza "we nani" bas akanijibu nkamuambia anitafute baadae,
Kweli ile baadae akanitafuta akajieleza wee, mie namsikiliza tyuuh, mara akaomba tuonane, nkamuuliza wapi anajibu mie kitambaa cheupe club sijui pub iko tabata, nkamgomea nkamuambia ukitaka njoo chuo sku gan nkamuambia, kweli ile siku alifika ndo nlimuona vizuri sasa, yaan akaanza kusema madhaifu ya gay yule, kumbe namjua nia yake mie niingie mtegoni nkawa namchora tyuuh, nkamdadisi sasa km kweli yule gay ana mapungufu hayo, kwanini bado yuko nae, na anamsaliti mke wake, majibu yake hadi nilijihisi homa.
Yaan akaanza kusingizia eti kuwa mkewe hakua muaminifu ktk ndoa, akaamua atafte mchepuko (ke) ili kupoza machungu, lakini huyo mchepuko alichofanya afadhari ya mkewe. sasa akaona wanawake nao ni wale wale, heri ageukie kwa gay, ilifikia hatua huyo gay analala nae ktk kitanda ki1 anacholala na mkewe, pindi akiwepo safarini au likizo mkoani, mie nikamuhoji baada ya yeye kuona mchepuko haujasaidia, kwanini asingetulia na mkewe waijenge familia yao. Akaanza kufunguka kuwa kuwa yeye ana hisia na gays (bottoms) ila kuoa amefanya kuepusha vidole vya jamii na kuwaridhisha wazazi/ndugu zake. nilichoka hapo hoi, nkaendelea kumuhoji kwanini sasa ameoa? Ili hali hana hisia na wanawake, asingisizie sjui hizo sababu wala hazina mashiko, kuoa na kuolewa sio lazima, sasa kwanini anamtesa kihisia binti wa watu akati yeye hana hisia nae? Akabaki anajitetea visivyo eleweka, nkaamua kumuambia ukweli wazi wazi.
Nkamuambia ni heri aachane na huyo mkewe kuliko kumtesa kihisia,(alikiri hana hisia na wanawake) japo ukweli anaujua yeye, nkamuambia kuhusu watoto tafuteni namna ya kuwalea pasipo kuathiri ukuaji na malezi bora kwao. Kwani mkewe atakapojua kua haya anayoyafanya itakua madhara zaidi ya kuachana unless awe ameridhika na hilo au hatalichukulia uzito. Nkaendelea kumuambia kuwa nje ya huyu Gay na mchepuko, km mkewe hakua muaminifu ni heri angechagua njia bora kwake, kuachana au kusamehe, kuliko kuongezea matatizo ktk familia yake. Yule mwanaume alinitazama na hakuamini km mie ndo nazungumza nae, nkamuhoji ushawahi kua na mahusiano na gay kabla ya kuoa akanijibu yes wakati akiwa advance na chuo pia. Nimkambana tena wee hapo inaonekana unao gays wengi na pia ni Malaya, kwani km sio hivyo usingenitaka mie, akaanza kusema oooh mie gay yeyote akipita mbele yangu ninae akikaa hovyo napita nae, nlichoka nilitamani nilie kwa uchungu, jinsi gan mwanamke au binti wa watu atakavyoletewa magonjwa




. Nlijawa na huruma na hofu juu yake, baada ya mazungumzo hayo tukaachana,
Hadi leo bado wako ktk mahusiano, ila ndoa ya huyo mwanaume inasua sua natamani hata nimteteee huyu mwanamke ila naanzia wapi na nitaonekanaje kwa huyu mwanaume na gay wake. Mwanaume ndo amezama ktk kina kirefu cha mapenzi kwa gay, hasikii wala haoni. Hata marafki zangu hawa (ke) nlipowashirikisha walinikanya nisiingilie hayo mambo hayanihusu,niwaache wao wenyewe wapambane.
Nawaonea huruma sana wanawake walio olewa maana mambo km haya kwa waume zao hawawezi gundua wala kujua kamwe, wanabaki kuteseka gizani.
Haya hivi kwa mfano gays wote aliotembea nao huyu mwanaume wauwawe, huyu mwanaume hata tafuta gay mwingine au hata kumrubuni yeyote kumuanzisha?ukizingatia pesa na ushawishi anao.
Nimejaribu kuwaonesha jinsi ushoga ulivyo mpana,nina visa na matukio mengi ila nimeweka hili,ili wanaume na wanawake muangalie mnapambana na kitu au jambo la ukubwa upi.
.........