Teh mkuu wewe ndiyo ulinisingizia kuwa mimi natetea ushoga au umesahau sasa kati ya mimi na wewe nani mnaa? Wewe umenipa maandiko kutoka kwenye biblia nami nimekupa andiko kutoka kwenye biblia ila cha ajabu nikikupa mimi unapinga ila ukinipa wewe unataka nikubali as if ninayokupa mimi natunga mwenyewe!
Kuna comment kule juu nilikuuliza shoga akitubu anaenda mbinguni au haendi ukanijibu anaenda na ukakubali kwamba hata naye anasamehewa kama wengine hadi ukaingiza sijui habari za TPDF na kunitaka nikemee ushoga! Sasa kwanini tuzunguke sana ikiwa shoga naye akitubu ataenda mbinguni kama ambavyo mzinzi naye akitubu ataenda?
Mimi nilikupa maandiko haya:
Luka 6: 42
Au, utawezaje kumwambia ndugu yako, Ndugu yangu, niache nikitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako, nawe huiangalii boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe, ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi kilichomo katika jicho la ndugu yako.
1 Wakorintho 6: 9 - 10
9 Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,
10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi.
1 Wakorintho 6: 18 - 20
18 Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.
19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;
20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.
Mwanzo ulikuwa unarukaruka ila baada ya kulipata hilo andiko moja ndiyo umeamua ushikilie hapo hapo ukifikiri kwamba hilo andiko ndiyo litafunika hayo maandiko mengine yote! Unafikiri hilo andiko la ufunuo ulilokazania ndiyo linapinga hayo maandiko mengine yote?
Hakuna sehemu biblia inasema adhabu ya moto itatofautiana kulingana na dhambi alizotenda mtu! Labda unioneshe ni wapi biblia inasema kuna levels za ukali wa moto wa jehanam kulingana na ukubwa wa dhambi nioneshe!
Mkuu wewe ndiyo hujui kuchambua biblia ndiyo maana ukatoa mifano kama eti sijui kwanini Lutu alipokuwa anakunywa pombe na kufanya mapenzi na wanawe ule moto wa Sodoma na Gomora haukuja kuwaunguza na wao duuh! Haki nilicheka na kushangaa sana siku ile!
Na inaonesha hata Mungu mwenyewe bado hujamjua vizuri namna anavyofanya kazi zake achilia mbali hayo maandiko yake! Sema kwa vile nimekaa kimya kuhusu hayo mkuu wangu basi ndiyo ukajiona unajua kuchambua hayo maandiko kuliko hata wale waliyoyaandika mwee na kuwaona wengine hawajui kitu!
Kwahiyo mimi kukalia kimya baadhi ya mambo ambayo naona kabisa hauyajui na umepuyanga haikufanyi uwe sahihi katika hayo yote unayoandika! Ila wewe naona umekazana kusema tu nimeshindwa sijui wewe ndiyo mshindi sasa sijui ni mashindano gani hayo ambayo umeshinda dooh pathetic!
Na naona unafikiri kwamba mimi kufunga huu mjadala basi ndiyo nimeshindwa kuendelea kukuelewesha au eti nimekubaliana na wewe kwa kila ulichoandika! Maana naona unanilazimisha kweli nikubaliane na wewe tofauti na mimi ninayekuelewesha taratibu na kukuacha ujitafakari ili ukitaka uyachukue usipotaka uyaache kiroho safi tu!
Niliamua kufunga mjadala ili niokoe muda wangu na nguvu zangu maana nimeshaona hapa hatutafika mwisho wala kufikia suluhisho halafu sifaidiki na chochote! Mimi ninapoquote wengine wala sijakutaja wewe ila umejihisi tu mimi nimeamua kukuacha ubaki na imani yako na mimi nibaki na imani yangu ila kama utataka kuendelea kujitunuku huo ushindi hewa basi endelea tu mkuu the floor is all yours mie huo utoto siuwezi so nimeshamalizana na wewe kuhusu habari za ushoga na hayo maandiko usiyojua tafsiri yake!