Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Roho ngumu ya kijerumani - IRINGA >> mbeya
IMG_20211209_173655_347.jpg
 
Walokole wengi (hata wale feki) huwa wanajiona kama wana hatimiliki na Mungu; na wana ka authority fulani hivi na Neno lake. Ila ukiangalia maneno na matendo yao sasa mpaka unatikisa kichwa.

Kila mtu na ashike sana alichonacho hasa nyakati hizi ambapo watu hawaogopi kitu tena; mpaka dhambi za kinyama zinatendeka mchana peupe; huku zikitetewa na kuungwa mkono waziwazi.

Dunia nzima sasa imejifunga kibwebwe kueneza na kusambaza ushoga. Huwezi kuangalia muvi kwa amani bila kukutana na ushoga. Mpaka katuni za watoto. Na kama unataka uharibu career yako jaribu tu kuusema ushoga vibaya. Utafukuzwa kazi na kuandamwa sana. Mpaka imekuwa kama sifa fulani hivi mtu akijitangaza kuwa ni shoga (ku- come out). Huyo ndo ataitwa shujaa na mwenye courage. Shujaa wa nini? Courage ipi? Wanajua wenyewe!

Kwa nini dunia nzima inapiga kampeni ku promote ushoga? Kuna kitu gani ambacho ni so special kuhusu ushoga? Wapo baadhi ya watu wanaofungamanisha kampeni hizi na mfumo mzima wa kumwondoa binadamu na kumtenga mbali kabisa na Mungu lengo likiwa ni kuweka mazingira mazuri ya New World Order - serikali moja ambayo kiongozi wake mkuu atakuwa ni yule mpinga kristo aliyetabiriwa kuwa atatokea siku za mwisho kabla ya Masihi kurudi. Eti huyo mpinga Kristo naye atakuwa shoga! Kwamba, japo dhambi zote ni machukizo kwa Mungu na mshahara wake ni mauti, hakuna dhambi yenye kudhalilisha utu na kumfikisha binadamu katika utengano kamili na Mungu wake kama ushoga. Ndiyo maana dunia imewekeza sana katika dhambi hii na waalimu wa unabii wanasema kuwa haijawahi kutokea dunia nzima kuungana katika kupromote dhambi kuu waziwazi namna hii kama tunavyoshuhudia leo.

Mnaweza kukesha hapa mkibishana na kutukanana lakini wenye dunia yao wanajua kinachoendelea ndiyo maana wamewekeza mabilioni ya dola kwenye ajenda hii. Na kama ilivyokuwa kwenye suala la demokrasia (vyama vingi), inaaminika kuwa ushoga nao utalazimishwa tu kama ajenda ya jumla kwa mataifa yote duniani. Usiporuhusu ushoga unanyimwa misaada ya kiuchumi na wakubwa wa dunia. Ushoga sasa ni suala la haki za msingi za kibinadamu!

Basi kila mtu na ashike sana alichonacho!
Duuh Mungu aepushie mbali asee
 
Back
Top Bottom