Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Dooh sema mjomba unaonekana we ni short tempered kinyama unamind hadi vitu vidogo! Sikutegemea kama huu mjadala ungekuturn this furious!
kapanicl vibaya, hata sikuwaza kumbe yuko hivi,
 
Aiseee hivi ni kwanini mkishashikiwa pabaya huwa mnakimbilia kusema kuwa siyo wote wanaoamini dini wala uwepo wa Mungu? Na huwa mnakimbilia kwenye mwamvuli wa sheria na tamaduni kwani kila mtu anafuata hizo tamaduni?

Sasa kama wewe hauwaheshimu mashoga kwanini unanilazimisha mimi niwaheshimu watu wasioamini Mungu katika kundi la watu wengi wanaoamini Mungu? Je vipi dunia nzima tukasema tusimuamini Mungu hali itakuwaje?

Halafu pia kwanini ulazimishe kila mtu aamini sayansi what is sayansi? Wakati hata sayansi nayo kuna vitu havijawa proven kwa asilimia mia moja kama ambavyo atheists wanaamini kuna vitu kuhusu deity havijawa proven kwa asilimia mia moja?

Hifadhi nguvu na amani yako kwa matumizi.mengine ya msingi.

Kwanza huu ni uzi wa mapichapicha...wanaotaka kutujazia magazeti ni kupita kama hauoni mtu.

Nani hapa hana dhambi au madhaifu yoyote hadi aanze kuhukumu wengine?

Cha ajabu watu wanataka kushambuliana jukwaani tena mtandaoni ambapo hata hamfahamiani?

Sehemu ambayo mtu anaamua awe kitu chochote anachotaka yeye.

Hata uraiani mtu hauwezi kuhusika na maisha ya kila mtu...kuna wavuta bangi, walevi, wezi, waongo, wazinzi, wadangaji.orodha ni ndefu. Sasa ukianza kuhangaika na hao watu si utazeeka kabla ya muda?

Hao wasioelewa achana nao, tupia picha kwanza

IMG_20211203_232828_854.jpg
 
Basi mkuu inatosha. Pumzika sasa uzi uchukue mkondo kwingine. Kulitaka kupoa kidogo lakini sasa umekuja unakwoti kila mtu na kuchochea moto upya. Mjadala huu utaendelea mpaka lini? Acha sasa ili watu waendelee na mambo mengine. Hukuwepo na watetezi wako wamekupigania sana. Let's move on to other important things. Jifunze kusikiliza na mashauri ya watu wengine na siyo wewe kujifanya wewe ndiyo wewe tu. Inatosha sasa. Acha watu waendelee na mambo mengine...
Hadi kaifikie hii comment ni asubuhi
 
Kanaanziaga kusoma juu kalipoishia.
Na kanasomaga comment moja moja na kanatoa response ,,hakana utaratibu wa kusoma zote.
Ndivyo kalivyo siku zote,siyo kwenye mada hii tu.
Ulivonijaa umbea mie, huwa sitaki kupitwa.
Heri nikose kula, ila sio umbea, tena kuna bonge la story, nataka nianzisje uzi wake,

Umbea wa moto mjini hapa.
 
Hey ladies, mkuwe basi jamani. Yaani uzi mzima mmeuharibu kwa kuleta mada zenu za ushoga embu hayo mambo yenu mkayazungumzie huko PM.

Huu uzi ulikuwa mzuri mmeanza kuuharibu kwa kuingiza mada zenu za ajabuajabu, muwe na aibu basi.
Hey cc, hili jambo hapa sio sehemu yake, ila baadhi ndo walitaka haya, tulishatoa muongozo mbona.
 
Leo nimekatetea maana walikuwa wanajadili mada nyingine kabisa.
Mbona kakienda hovyo huwa nakapa za uso, na watakaonivamia nao nawatwanga hivyohivyo.
Yeaaaah nakupenda nikikosea unanikanya, na nikiwa sawa unaniweka sawia, ubarikiwe,
 
najuaga kuchukia mie bas? kwangu burudani tyuuh, naishi navyotaka, sio wanavyotaka.
Sawa lakini kama kila mtu angeishi anavyotaka, jamii ingeparaganyika. Maelewano katika jamii yanamtaka kila mwanajamii kuacha kufanya baadhi ya vitu kama vinawakera wengine - hasa kama vitu hivyo havimwongezei wala kumpunguzia cho chote. Hiki ndicho kiini cha dhana ya "kuishi vyema na watu". Kama kila siku wewe ndiyo kiini cha purukushani na migongano katika jamii, pengine ni wakati wa kurekebisha baadhi ya mambo hasa kama hayakunyimi raha na utashi wako.

Ila kama burudani tyuuh ni muhimu zaidi kuliko utangamano na maelewano na watu basi endelea tu mkuu. Mpaka wakuroge yaani
 
Sawa lakini kama kila mtu angeishi anavyotaka, jamii ingeparaganyika. Maelewano katika jamii yanamtaka kila mwanajamii kuacha kufanya baadhi ya vitu kama vinawakera wengine - hasa kama vitu hivyo havimwongezei wala kumpunguzia cho chote. Hiki ndicho kiini cha dhana ya "kuishi vyema na watu". Kama kila siku wewe ndiyo kiini cha purukushani na migongano katika jamii, pengine ni wakati wa kurekebisha baadhi ya mambo hasa kama hayakunyimi raha na utashi wako.

Ila kama burudani tyuuh ni muhimu zaidi kuliko utangamano na maelewano na watu basi endelea tu mkuu. Mpaka wakuroge yaani
wao wanavofanya mambo yao mie nawakatazaga? Si kwa uhuru wao? Na wao waache kufatilia wenzao, kila mtu ashinde match zake bhana wee,

Najua sana unakerekwa na hii mada asingekua mommah kuwapa za uso, hata wee ungeshambulia

Kajua kuwakomesha na unafiki, wamebaki kuhaha hawajui washike wapi.
 
Back
Top Bottom