Yeah hiki ndicho nilichotaka kusema mkuu, kwa sisi wakristo dhambi pekee isiyosameheka ambayo ni kubwa na mbaya kuliko zote ni kumkufuru au kumdhihaki Roho Mtakatifu. Keyword ni Roho Mtakatifu haijasema Mungu Baba wala Yesu, na hiyo dhambi haihusishi ushoga.
Kwani mkuu Mungu kuangamiza wanadamu kwa moto ilikuwa ni adhabu ya kwanza kwa wanadamu inayohusisha vifo vya watu wengi? Si kuna gharika ambayo aliangamiza dunia nzima kasoro Noah na nduguze na baadhi ya viumbe wengine je ile ilikuwa ni adhabu ya ushoga pekee?
Kumbuka hata kule Nineveh walizidi maovu na Mungu alitaka kuwaangamiza kabisa ila akamtuma Jonah akawahubirie waache maovu ndipo Mungu alipowasamehe baada ya Jonah kuwahubiria na wao kuacha maovu yao! Sasa niambie je Nineveh nako walitaka kuangamizwa sababu ya ushoga tu?
Na unajua kwamba tukija kwenye uhalisia kiroho dhambi mbaya kuliko zote ni uzinzi? Maana maandiko yanasema kabisa afadhali ya dhambi nyingine mtu anazifanya nje ya mwili wake ila dhambi ya uzinzi mtu anaifanya juu ya mwili wake mwenyewe lakini mbona watu hawaikemei hii dhambi wanaiona kawaida?
Halafu kumbuka maandiko hayo hayo yanamuita mnafiki mtu ambaye anatoa boriti kwenye jicho la mwenzie ilihali hajatoa kibanzi kilichopo kwenye jicho lake mwenyewe! Leo hii eti mzinzi anajiona mtakatifu kuliko shoga na hebu niambie ni watu wangapi leo hii wanasubiri hadi ndoa ndiyo wafanye?