Basi bana kuna day miaka hiyo nilienda zahanati moja hivi ya serikali, nikajimaliza kwa Dokta then akanipa karatasi ya kwenda nayo maabara.
Kipimo alichoandika hakisomeki wala sikukielewa ko sikushughulika nacho sana, kufika nikaenda kabidhi ile kadi kusubiri kuitwa. Yule attendant akauliza umetoka kwa Dr. Room na 3 nikamwambia ndio, yule dada akajiongelesha ' ana nini huyo leo mbona karibia watu wote anawaleta huku?
Nikashtuka kidogo ila sikuongea nikarudi kukaa kwa viti, basi nikakaa karibu na mdada wa saizi yangu akili ikaniambia muulize kaandikiwa kipimo gani.
Kuuliza akanijibu kipimo sawa na nilichoandikiwa tena akaongeza 'unajua ni kipimo cha HIV hiki? Nikamwambia hata sijui, basi nikagoogle chap nikaona ni bla bla za HIV.


Nikamuaga yule dada nikamwambia siwezi poteza muda wangu hapa maana nilivyojimaliza kwa DR na hiki kipimo sioni koneksheni yoyote



nikasepaa.