Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Nafuatilia kuanzia mwanzo, na mwenye uzi alishaasa yakaisha ila bado yanaendelea na Mshana Jr kaacha mtu ajadiliwe bila yeye kuwepo kujitetea, akiguswa mwingine mmmh anyway ngoja niwe mtazamaji
Dah... Sijaelewa hapa.. Ila kiroho safi kabisa tufanye kama imeisha hii.. Tulimalize kiume kuonesha tofauti
 
Kabisa my dear siyo sifa, halafu hata mimi nikibishana na wanaume wakiishiwa hoja huwa wanaishia kusema "mwanamke hautakiwi kuwa mbishi hivyo" huwa najitahidi kuacha ila nashindwa kwa kweli.

Siwezi kuvumilia mtu ananiambia eti hii ni juisi wakati mimi naona kabisa hii ni pombe (huo ni mfano tu) halafu nikae kimya sasa ndicho wanaume wengi hata wa humu wanachotaka hicho wanataka tukubali kila wanachotuambia eti kwa sababu tu wao ni wanaume na sisi ni wanawake

Kwenye siasa siku hizi nimeacha ndiyo maana hata JF huwa siingii kwenye jukwaa la siasa mimi siasa ilikuwa mwaka juzi hadi mwaka jana instagram kwenye account ya Mange Kimambi kipindi kile na yeye yuko moto na nilikuwa natumia account yangu halisi yaani nilikuwa naona siku yangu haijakamilika bila kuingia instagram kutembelea account yake

Nilikuwa nachambana na watu kwenye comments kama ninavyochambana na watu humu alafu sasa nikapataga boyfriend ambaye tunatofautiana itikadi za kisiasa naye akileta za kuleta kuhusu siasa nilikuwa namchamba hadi ananiambia eti Mange Kimambi kaniharibu niache kumfuatilia nikasema siachi ng'oo ila nashangaa siku hizi hata mtu amsifie au amponde kiongozi gani wala hata sihangaiki siku hizi niko na haya mafurushi ya JF humu yaani nimekuja kugundua haya mambo ni ya muda tu yanakuja yanaisha kuna muda utafika humu nitakuwa nakuja kucomment kama Smart911 halafu natoka, oohh I just can't wait.
 
Niko nawaangalia tu, ila najua siku nikirudi najua nitapigwa LIFE BAN maana kuna watu watakimbia ID zao kimoja hapa...

Naona Mshana Jr anawaunga mkono wakati jana tulikubaliana kuwa hakuna haja ya kuendeleza majibizano maana content ya uzi wake utaharibika...

Wasione nimekaa kimya wakadhani huyu tumempatia...
Dah....
 
Nakumbuka jana tulikubaliana kabisa hakuna haja ya kuendelea majibizano katika uzi wako, ila nimeingia naona bado kuna watu wanaendeleza ujuaji, halafu wengi wao ni mabinti wadogo tu, tena wengine ni kwamba wapo vyuoni bado na wengine ndio wanategemea kuhitimu mwaka huu, wengine ni walimu...

Nimetoa tu angalizo, wasione nimekaa kimya wakadhani siwezi kuna na vivid evisence na hapo ndipo uzi huu utafungwa na mimi kula LIFE BAN na pia kuna watu watakimbia ID zao...

Ongea na wadogo zako hao...
Yaishe mkuu..tusifanye mambo yawe mengi.

Funika kombe
 
Back
Top Bottom