Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Luka 12:16-21​

Neno: Bibilia Takatifu​

16 Kisha akawaambia mfano, “Shamba la tajiri mmoja lilizaa sana.

17 Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Maana sina mahali pa kuweka mavuno yangu.’

18 Kisha akasema, ‘Nitafanya hivi: nitabomoa maghala yangu na kujenga maghala makubwa zaidi na huko nitaweka mavuno yangu yote na vitu vyangu.

19 Na nitasema moyoni, ‘Hakika nina bahati! Ninayo mali ya kunitosha kwa miaka mingi. Sasa nitapumzika: nile, ninywe na kustarehe.’

20 Lakini Mungu akamwambia, ‘Mjinga wewe! Usiku huu huu utakufa! Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea vitakuwa vya nani?’

21 Hivi ndivyo itakavyokuwa kwa mtu yeyote anayehangaika kujikusanyia utajiri duniani lakini si tajiri mbinguni kwa Mungu.”
Ah hakika
Upo vizuri kwa neno ..

Mathayo 6:19-21​

Mathayo 6:19-21 BHN​

“Msijiwekee hazina hapa duniani ambako nondo na kutu huharibu, na wezi huingia na kuiba.

Jiwekeeni hazina mbinguni ambako nondo na kutu hawawezi kuiharibu, wala wezi hawaingii wakaiba. Maana pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa .
 
Ah hakika
Upo vizuri kwa neno ..

Mathayo 6:19-21​

Mathayo 6:19-21 BHN​

“Msijiwekee hazina hapa duniani ambako nondo na kutu huharibu, na wezi huingia na kuiba.

Jiwekeeni hazina mbinguni ambako nondo na kutu hawawezi kuiharibu, wala wezi hawaingii wakaiba. Maana pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa .

Mhubiri 1:14 BHN​

Nimeyaona yote yanayofanywa duniani; yote ni bure: Ni sawa na kufukuza upepo!


1 Timotheo 6:10 BHN​

Kwa maana kupenda sana fedha ni chanzo cha uovu wote. Watu wengine wametamani sana kupata fedha hata wakatangatanga mbali na imani, na wameivunja mioyo yao kwa huzuni nyingi.
 
Back
Top Bottom