Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Nilijua nikiongea naye nitampa shetani nafasi.
Naona naye ameokoka kaka wa watu.. akaishia kuniangalia tu,,,
Mimi nikishachomoka tu ni miendo,, hata pembeni siangalii.


Wote tumeshukia mlango mmoja,, huu wa upande wa dereva pembeni ambao huwa unafunguliwa kwenye vituo vya mwendokasi.
Sasa pale Mbezi ukishukia ule mlango lazima uruke..
Tumeongozana wote, ananiangalia..
Akaruka, nikaruka
Nilivyoshuka hapo mimi ni mwendo hata nyuma huwa sigeuki Tena.
Ngoja ninyamaze
 
Leo nimetoka posta nimepanda na kaka mmoja kwenye mwendokasi
Huwa nasimama kwenye maungio yale,
Yeye kapandia Jiji.
Kaja kusimama mbele yangu tukawa tunaangaliana..nilikuwa nimeinama alipopanda akanigonga nikashtuka,nikamuangalia nikakuta HB hatari.

Mzuri jamani,amevaa vizuri suti yake,halafu ananukia.

Mwee safari nimeiona fupi,
Naye kasimama palepale hadi mwisho,
Hajasogea hata mbele yake.
Tumeishia kugongana gari ikiyumba..
Mara ahamishie mkono niliposhikilia,
Na mimi hata sikuutoa.
Ila kumuangalia nilikuwa siwezi,nikawa naibia,,nimevaa cap.

Nikasema hapa lazima nimshinde shetani,,wakati wa kushuka ntashuka haraka yasije Kutokea mengine.

Naye kumbe akawa anashukia Mbezi stand.

Aisee gari imesimama,nachukua begi langu pale chini nilikuwa nimeweka
Kaka amesimama tu ananiangalia.
Nilivyomuangalia akageuka kuangalia mlango wa Kutokea.
Nimeishia kutabasamu tu na kuondoka .
Nimeokoka nampenda Yesu.


Wanaume jitahidi muwe mnanukia jamani,
Wakati wa kwenda nilipanda nikakaa mwisho kabisa na wakaka wote,
Aliyekaa pembeni yangu ananuka jasho jamani chaa

Angalau safari yangu ya kurudi imekuwa mubashara.
Note taken,, Tunukie
 
And kazi ikaisha kwa an episode from Big bang theory
IMG_20230320_213830.jpg
 
Back
Top Bottom