Hivi vifaa vya moto ni hatari sana.
Kuna gesi tulikaa nayo wiki 1 mtungi mkubwa 30 kgs ukakatika😂
Niliwaambia jamani hii gesi inavuja,, ilikuwa inanuka mno, wakasema kawaida..Ni Mungu tu alitunusuru haikulipuka maana harufu yake ilikuwa inasambaa jikoni kote hadi sebuleni.
Heater almanusura ichome nyumba.
Mtoto aliwasha akaitupia kwenye nguo.
Mama yake yupo nje anafua,machale yakamcheza akamuangalie mtotol kuja kustuka baadaye wanaona Moshi unatoka chumbani.
Mimi zangu kuni na mkaa.
Nikiwa na haraka natumia Kuni.