Acha niongee nikiwa na akili timamu ni set dish mahala pake.
Issue sasa hivi ya kutokuwa na uaminifu na hofu kwenye mahusiano mengi inatokana na misingi mibovu ya kiimani, kimaadili ukiachana na yote mengine. Kila kitu kwenye maisha ya mwanadamu kinajengeka kwenye imani na maadili (kwenye maadili tunapata tamaduni )
Niongee kwa ufupi imani ya kweli, inapokosekana si Me au Ke atae kuwa na hofu kwa Mungu, hofu kwa Mungu ikishapotea hakuna uaminifu, mtu hamuogopi Mungu na sio muaminifu kwa Mungu unategema awe na hofu na muaminifu kwa mwanadamu mwenzake?
Tukija kwenye tamaduni, misingi mingi ya kitamaduni imekufa enzi zetu tulipokuwa tunataka kuoa wazee wanafanya vetting kijijini, unaoa unacho kijua na unaolewa na unacho kijua..
Ila sasa hivi nakutana na manzi kidimbwi imenipa mifinyo kesho natangaza ndoa hujui kama jambazi au mchawi