Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Halafu we unasema dunia iishe tu, kuna watu wana mitihani duniani, tumshukuru Mungu kwa kila jambo.
Na mimi ninayo yangu ila nilioupata ulinipiga penyewe.. nashindwa kuukubali.


Nimemuonea huruma maana nimevuta picha maumivu aliyopata na anayoendelea kupata..
Yaani ajali ni mbaya,,viungo hata vikirudi,haviwezi kuwa the same kama mwanzo.
Mimi almanusura gari liondoke na kichwa Changu hadi leo hakipo sawa.

Sent from my TECNO CG6 using JamiiForums mobile app
 
Halafu we unasema dunia iishe tu, kuna watu wana mitihani duniani, tumshukuru Mungu kwa kila jambo.
We acha tu...

Mtu wa karibu sana (42yrs) hapa alikuwa anasumbuliwa na tumbo. Linauma. Linatulia. Mara anahara. Mara tumbo limejaa gesi...amekuja kwenda hospitali amekuwa diagnosed na terminal liver cancer. Yaani kansa imeshaenea kwenye ini mpaka figo na uti wa mgongo na pancreas. Madaktari hawana la kufanya. Wamemwambia akitoboa miezi mitatu ni bahati...na ndiyo tu kaanza PhD yake ya Economics na ana mtoto wa miezi mitano. Just like that maisha yamebadilika.

Uzuri ni kwamba anamfahamu Yesu na uwezo wake; na ameshasema kuwa hawezi kufa. Ijumaa hii kuna maombi maalum kwa ajili yake kanisani...

Ndo maisha yetu. Leo upo unajiona mzima kabisa na ujana wako. Kesho lo lote laweza kutokea. Hata sijui wasio na tumaini katika Yesu wanaishije katika dunia hii ya shida...

Tuombe sana Mungu Atuongoze - katika nyanja zote za safari yetu katika kasayari haka kazuri
 
Na mimi ninayo yangu ila nilioupata ulinipiga penyewe.. nashindwa kuukubali.


Nimemuonea huruma maana nimevuta picha maumivu aliyopata na anayoendelea kupata..
Yaani ajali ni mbaya,,viungo hata vikirudi,haviwezi kuwa the same kama mwanzo.
Mimi almanusura gari liondoke na kichwa Changu hadi leo hakipo sawa.

Sent from my TECNO CG6 using JamiiForums mobile app
Pole sana.
Unahisi headaches, una TBI?
 
Pole sana.
Unahisi headaches, una TBI?
Lilikwanguaga tu karibu na kichwa😂
Ni miaka 10 sasa umepita,,ila hili eneo nikishika ama nikijigonga linasisimka.

Kurudi kama mwanzo ni mtihani sana.
Namuombea huyo dada Mungu amponye.
Japo ndio hivyo hana kipande cha mkono 🥺..hata kingebaki bado hakiwezi kuwa na nguvu kama mwanzo..hapa narefer kwenye kajimkono kangu linivunjikaga miaka 15 iliyopita.
Hayo niliyapita.

Linalonitesa sasa ni kumbukumbu tu za msiba.
...........
Kwanza usinitoe kwenye reli..
Naomba ile picha
 
Back
Top Bottom