We acha tu...
Mtu wa karibu sana (42yrs) hapa alikuwa anasumbuliwa na tumbo. Linauma. Linatulia. Mara anahara. Mara tumbo limejaa gesi...amekuja kwenda hospitali amekuwa diagnosed na terminal liver cancer. Yaani kansa imeshaenea kwenye ini mpaka figo na uti wa mgongo na pancreas. Madaktari hawana la kufanya. Wamemwambia akitoboa miezi mitatu ni bahati...na ndiyo tu kaanza PhD yake ya Economics na ana mtoto wa miezi mitano. Just like that maisha yamebadilika.
Uzuri ni kwamba anamfahamu Yesu na uwezo wake; na ameshasema kuwa hawezi kufa. Ijumaa hii kuna maombi maalum kwa ajili yake kanisani...
Ndo maisha yetu. Leo upo unajiona mzima kabisa na ujana wako. Kesho lo lote laweza kutokea. Hata sijui wasio na tumaini katika Yesu wanaishije katika dunia hii ya shida...
Tuombe sana Mungu Atuongoze - katika nyanja zote za safari yetu katika kasayari haka kazuri

