Sasa ni dhahiri kesi ya Mbowe imekaa vibaya. Mashahidi 24 na vielelezo 19 vya serikali si mchezo. Ni mkao wa kunyolewa

Mlimamrefu

Member
Aug 1, 2021
27
93
Kwa mashtaka yaliyosomwa leo tarehe 23 Agosti 2021 ni wazi serikali imejipanga ipasavyo kwa kesi hii ya Mbowe ya ugaidi.

Serikali kuwa mashahidi 24 na vielelezo 19 siyo mchezo. Sasa tunafahamu kwa nini IGP alilizungumzia hii kesi kwa kujiamini sana na kueleza kuwa Mbowe kama ni mkristo mkweli atawaeleza ukweli wafuasi wake. Yote kwa yote, mahakama ndicho chombo cha juu cha kutoa hukumu.

Kupitia hukumu hiyo tutajua ukweli wa jambo hili. Kwa hatua iliyofikia kesi hii, ni vyema sasa tuiache mahakama ifanye kazi yake. Mabango na kauli za kisiasa kutoka Chadema sasa siyo mahali pake. Bahati nzuri katiba za vyama vyote vya siasa vinasisitiza juu ya kutambua utawala wa kisheria ambapo masuala ya mahakamani yanaachwa kwa mahakama kuamua na siyo kuyaleta kwenye majukwaa ya kisiasa.

Tutaishangaza dunia ikiwa bado chama fulani kitaendelea na kuweka mashinikizo nje ya mahakama. Pamoja na kwamba shinikizo zenyewe hazina hata nguvu ya kufungua soda na haziwezi kubadili lolote kuhusu mwenendo wa hii kesi, bado ni bora tukaachana na kuonesha shinikizo hizo ambazo kwangu naziona ni za kitoto na zinazidi tu kuwadhalilisha wanaoziweka.

Court decisions are based on what the law says and what the evidence proves. There is no place in the courts for suspicion, bias or favouritism. Tuachane na hizo empty rhetoric
 
The last issue to answer is how many witnesses are required to prove a fact in a criminal trial? As rightly put by the learned State Attorney and to our minds rightly so, there is no particular number of witnesses required by law to prove any fact. What is important is the credibility of the witness. The provision of section 143 of the Evidence Act tells it all.

It reads: 11 "Subject to the provisions of any other written law, no particular number of witnesses shall in any case be required for the proof of any fact.

in law, there is no specific number of witnesses required to adduce evidence. She referred to the case of YOHANNES MSINGWA (1990)TLR150.
 
Kwa akili zako mleta uzi unafikiri kujaza mashahidi na vielelezo ndio kunaprove guilty kwa condermed person hiyo ni michezo ya kimahakama tu ila kama hakuna strong arguments kuprove huo ushubwada wao ni kazi bure kwa watu wenye akili kubwa wanajua hizo ni hujuma za kisiasa kuhusu katiba mpya
 
Mbowe lazima ale mvua. Lema mjanja alikimbia madeni na kesi ya ugaidi. Kwa sababu lema alikuwa jambazi so anajua kabisa kama kitu kimekaa vibaya.
Kwa nini iwe lazima? Unao ushahidi walau kwamba Lema ana madeni na ni jambazi?

Jamii forum imekuwa Facebook sasa.
 
Ku

Kuna mtu alishangilia kifo cha magufuli akachinja na mbuzi wakala na wapambe wake
Nasikia nae kafa usiku wa kuamkia leo,
Sasa najiuliza mbona hata muda haujaenda kwa nini afe sasa wakati alihisi ana mkataba na mungu?
Na ni wale wanazi wa chadema.
Nani huyo
 
Matusi kutukanana mitandaoni na kutiana moyo kwenye ujinga, ni ujinga!

Sheria sio kwa makabwela peka yake, na magereza kwa wavunja sheria zisiishie kwa walala hoi,

Sheria zifanye kazi yake na mtu akibainika kafanya kosa hata kama ni nani, atiwe ndani
 
Kwa mashtaka yaliyosomwa leo tarehe 23 Agosti 2021 ni wazi serikali imejipanga ipasavyo kwa kesi hii ya Mbowe ya ugaidi.

Serikali kuwa mashahidi 24 na vielelezo 19 siyo mchezo. Sasa tunafahamu kwa nini IGP alilizungumzia hii kesi kwa kujiamini sana na kueleza kuwa Mbowe kama ni mkristo mkweli atawaeleza ukweli wafuasi wake. Yote kwa yote, mahakama ndicho chombo cha juu cha kutoa hukumu.

Kupitia hukumu hiyo tutajua ukweli wa jambo hili. Kwa hatua iliyofikia kesi hii, ni vyema sasa tuiache mahakama ifanye kazi yake. Mabango na kauli za kisiasa kutoka Chadema sasa siyo mahali pake. Bahati nzuri katiba za vyama vyote vya siasa vinasisitiza juu ya kutambua utawala wa kisheria ambapo masuala ya mahakamani yanaachwa kwa mahakama kuamua na siyo kuyaleta kwenye majukwaa ya kisiasa.

Tutaishangaza dunia ikiwa bado chama fulani kitaendelea na kuweka mashinikizo nje ya mahakama. Pamoja na kwamba shinikizo zenyewe hazina hata nguvu ya kufungua soda na haziwezi kubadili lolote kuhusu mwenendo wa hii kesi, bado ni bora tukaachana na kuonesha shinikizo hizo ambazo kwangu naziona ni za kitoto na zinazidi tu kuwadhalilisha wanaoziweka.

Court decisions are based on what the law says and what the evidence proves. There is no place in the courts for suspicion, bias or favouritism. Tuachane na hizo empty rhetoric
Mwigulu alijiapiza kumfunga Lwakatare , tena alitengeneza hadi video Studio , leo muulize ule uchafu wake ulikoishia , ndio ije kuwa huu ugaidi wa laki 6 ?
 
Back
Top Bottom