Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #161
SEHEMU YA 121...
“Haijalishi mke wangu, hata ukipita mwaka mzima, jua kuna siku mtoto wetu atakuwa mikononi mwetu,” alisema Richard, japokuwa alikuwa akizungumza kwa kujiamini lakini moyo wake haukuwa na imani hata kidogo.
Wakati akizungumza hayo na mkewe mara akasikia simu yake ikianza kuita. Akaitoa mfukoni mwake na kuiangalia. Namba ilikuwa ngeni, alitamani sana kuipokea lakini kwa kipindi hicho haukuwa muda sahihi wa kuipokea simu hiyo kwani alihitaji kuzungumza na mkewe.
Mpigaji hakukata, ilipokatika, akapiga tena na tena mpaka kuwa kero na hivyo Richard kuipokea na kuipeleka sikioni. Akasikia sauti nzito kutoka upande wa pili, alikuwa mwanaume ambaye alijitambulisha kama polisi na kumpa taarifa kwamba kuna mtu alitaka kuonana naye hapo.
“Nani?” aliuliza.
“Kijana mmoja! Amejitambulisha kwamba yeye ni mganga,” alijibu polisi huyo.
“Nimsaidie nini?”
“Kwamba anataka kuonana na wewe ili uweze kumpata mtoto wako,” alisema polisi, moyo wa Richard ukapiga paa.
“Ni mganga!”
“Ndiyo!”
“Sasa mimi na waganga wapi na wapi?”
“Naomba uje kumsikiliza!”
“Sawa nakuja!”
Richard akakata simu na kumwangalia mke wake. Alikuwa na hasira kali, hakuwaamini waganga na hakuona kama kwenye tatizo kubwa kama hilo mganga angeweza kumsaidia kwa lolote lile.
Akamwambia mke wake kuhusu simu ile iliyokuwa imepigwa, mkewe akamwambia kwamba aende huko kuonana na huyo mtu kwani siku zote binadamu hakutakiwa kukataa wito.
“Ila ni mganga!”
“Najua! Haimaanishi ukienda kumsikiliza tu basi atakuwa amekufanyia dawa. Nenda tu mume wangu,” alisema Bianca kwa sauti ya upole kabisa.
Kwa kuwa alisema mke wake, akachukua ufunguo wa gari na kuelekea huko. Hakuonekana kuwa na raha hata kidogo, moyo wake haukuwahi kumwamini mganga hata kidogo, alikwenda huko kwa ajili ya kumridhisha mke wake tu.
Alipofika, akateremka na kuelekea kaunta ambapo akamkuta Ibrahim ambapo baada ya kumuona Richard tu, akasimama kwa lengo la kuongea naye.
“Twende sehemu tukaongee!”
“Kwani hapa haiwezekani?”
“Ni muhimu sana! Twende tukaongee kaka,” alisema Ibrahim huku akimwangalia Richard.
Itaendelea.
“Haijalishi mke wangu, hata ukipita mwaka mzima, jua kuna siku mtoto wetu atakuwa mikononi mwetu,” alisema Richard, japokuwa alikuwa akizungumza kwa kujiamini lakini moyo wake haukuwa na imani hata kidogo.
Wakati akizungumza hayo na mkewe mara akasikia simu yake ikianza kuita. Akaitoa mfukoni mwake na kuiangalia. Namba ilikuwa ngeni, alitamani sana kuipokea lakini kwa kipindi hicho haukuwa muda sahihi wa kuipokea simu hiyo kwani alihitaji kuzungumza na mkewe.
Mpigaji hakukata, ilipokatika, akapiga tena na tena mpaka kuwa kero na hivyo Richard kuipokea na kuipeleka sikioni. Akasikia sauti nzito kutoka upande wa pili, alikuwa mwanaume ambaye alijitambulisha kama polisi na kumpa taarifa kwamba kuna mtu alitaka kuonana naye hapo.
“Nani?” aliuliza.
“Kijana mmoja! Amejitambulisha kwamba yeye ni mganga,” alijibu polisi huyo.
“Nimsaidie nini?”
“Kwamba anataka kuonana na wewe ili uweze kumpata mtoto wako,” alisema polisi, moyo wa Richard ukapiga paa.
“Ni mganga!”
“Ndiyo!”
“Sasa mimi na waganga wapi na wapi?”
“Naomba uje kumsikiliza!”
“Sawa nakuja!”
Richard akakata simu na kumwangalia mke wake. Alikuwa na hasira kali, hakuwaamini waganga na hakuona kama kwenye tatizo kubwa kama hilo mganga angeweza kumsaidia kwa lolote lile.
Akamwambia mke wake kuhusu simu ile iliyokuwa imepigwa, mkewe akamwambia kwamba aende huko kuonana na huyo mtu kwani siku zote binadamu hakutakiwa kukataa wito.
“Ila ni mganga!”
“Najua! Haimaanishi ukienda kumsikiliza tu basi atakuwa amekufanyia dawa. Nenda tu mume wangu,” alisema Bianca kwa sauti ya upole kabisa.
Kwa kuwa alisema mke wake, akachukua ufunguo wa gari na kuelekea huko. Hakuonekana kuwa na raha hata kidogo, moyo wake haukuwahi kumwamini mganga hata kidogo, alikwenda huko kwa ajili ya kumridhisha mke wake tu.
Alipofika, akateremka na kuelekea kaunta ambapo akamkuta Ibrahim ambapo baada ya kumuona Richard tu, akasimama kwa lengo la kuongea naye.
“Twende sehemu tukaongee!”
“Kwani hapa haiwezekani?”
“Ni muhimu sana! Twende tukaongee kaka,” alisema Ibrahim huku akimwangalia Richard.
Itaendelea.