Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
01
“Jamani leo natangaza rasmi….” alisikika jamaa mmoja akiwaambia wenzake.
“Tangaza…” wenzake walisema huku wakicheka.
“Kuanzia leo kwa hapa chuo, hakuna demu mkali kama yule Msukuma…” alisema jamaa huyo.
“Msukuma gani?” aliuliza jamaa mmoja huku akimwangalia mwenzake huyo aliyeamua kutangaza.
“Sarafina Butati! Yaani hakunaga!”
“Hahaha!” watu wote wakajikuta wakicheka.
“Jamani yule mtoto mkali! Jamani yule mtoto anaita! Jamani yule mtoto ana figa! Jamani! Jamani! Jamani! Nasema hivi! Kwa hapa chuo hakuna demu mkali kama Sarafina,” alisema jamaa huyo.
“Anamshinda Manka wa Kichaga?” aliuliza jamaa mwingine.
“Manka! Hivi yule demu anaingia kwa Sarafina? Hivi ushawahi kuvuta picha kichwani mwako ukamuona Sarafina akiwa mtupu? Yule mtoto jamani ni mkali sana, kuna kila haki ya sisi marijali kumpigia misele,” alisema jamaa huyo na wote kuanza kucheka.
Huyo ndiye msichana aliyekuwa gumzo katika Chuo cha Amazon kilichokuwa Temeke jijini Dar es Salaam. Kila mwanaume aliyekuwa katika chuo hicho cha ufundi alivutiwa na msichana huyo, uzuri wake uliwapagawisha wanaume wengi kiasi kwamba kila mmoja alimtolea macho.
Sarafina alikuwa msichana mrefu, mwenye mwendo wa maringo, alikuwa na hipsi pana ambazo kwa watoto wa mjini walipenda kuziita pisto, alikuwa na miguu iliyojazia kidogo huku akiwa na mapaja manene kiasi kwamba kila alipoyaruhusu yaonekane, kila mwanaume aliyamezea mate.
Usoni hakuwa wa kawaida, alikuwa na sura nyembamba, mdomo wake ulikuwa na lipsi pana, hata kama macho yake alikuwa akiyakaza, bado yalionekana kusinzia kwa mbali mithili ya mwanamke aliyekula kungu.
Mashavuni mwake alikuwa na vishimo viwili ambavyo viliufanya uzuri wake kuonekana kila alipokuwa akicheka hata kutabasamu. Hakuwa msichana wa kusuka, muda mwingi nywele zake alikuwa akizikata huku sura yake hiyo akiipendezesha na miwani meusi.
Sarafina hakujua kutembea kwa kasi, kila alipokuwa akitembea, alitembea kwa mwendo wa maringo kana kwamba hakuwa akikanyaga ardhi hiihii.
Aliwadatisha wanaume wote waliokuwa chuoni hapo, kila mmoja alimpenda, kila mmoja alitamani hata siku moja msichana huyo mrembo awe mpenzi wake.
Itaendelea
“Jamani leo natangaza rasmi….” alisikika jamaa mmoja akiwaambia wenzake.
“Tangaza…” wenzake walisema huku wakicheka.
“Kuanzia leo kwa hapa chuo, hakuna demu mkali kama yule Msukuma…” alisema jamaa huyo.
“Msukuma gani?” aliuliza jamaa mmoja huku akimwangalia mwenzake huyo aliyeamua kutangaza.
“Sarafina Butati! Yaani hakunaga!”
“Hahaha!” watu wote wakajikuta wakicheka.
“Jamani yule mtoto mkali! Jamani yule mtoto anaita! Jamani yule mtoto ana figa! Jamani! Jamani! Jamani! Nasema hivi! Kwa hapa chuo hakuna demu mkali kama Sarafina,” alisema jamaa huyo.
“Anamshinda Manka wa Kichaga?” aliuliza jamaa mwingine.
“Manka! Hivi yule demu anaingia kwa Sarafina? Hivi ushawahi kuvuta picha kichwani mwako ukamuona Sarafina akiwa mtupu? Yule mtoto jamani ni mkali sana, kuna kila haki ya sisi marijali kumpigia misele,” alisema jamaa huyo na wote kuanza kucheka.
Huyo ndiye msichana aliyekuwa gumzo katika Chuo cha Amazon kilichokuwa Temeke jijini Dar es Salaam. Kila mwanaume aliyekuwa katika chuo hicho cha ufundi alivutiwa na msichana huyo, uzuri wake uliwapagawisha wanaume wengi kiasi kwamba kila mmoja alimtolea macho.
Sarafina alikuwa msichana mrefu, mwenye mwendo wa maringo, alikuwa na hipsi pana ambazo kwa watoto wa mjini walipenda kuziita pisto, alikuwa na miguu iliyojazia kidogo huku akiwa na mapaja manene kiasi kwamba kila alipoyaruhusu yaonekane, kila mwanaume aliyamezea mate.
Usoni hakuwa wa kawaida, alikuwa na sura nyembamba, mdomo wake ulikuwa na lipsi pana, hata kama macho yake alikuwa akiyakaza, bado yalionekana kusinzia kwa mbali mithili ya mwanamke aliyekula kungu.
Mashavuni mwake alikuwa na vishimo viwili ambavyo viliufanya uzuri wake kuonekana kila alipokuwa akicheka hata kutabasamu. Hakuwa msichana wa kusuka, muda mwingi nywele zake alikuwa akizikata huku sura yake hiyo akiipendezesha na miwani meusi.
Sarafina hakujua kutembea kwa kasi, kila alipokuwa akitembea, alitembea kwa mwendo wa maringo kana kwamba hakuwa akikanyaga ardhi hiihii.
Aliwadatisha wanaume wote waliokuwa chuoni hapo, kila mmoja alimpenda, kila mmoja alitamani hata siku moja msichana huyo mrembo awe mpenzi wake.
Itaendelea