Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #141
SEHEMU YA 108...
Akampigia simu, kitu cha kwanza kabisa alichokutana nacho ni malalamiko kutoka kwa mzee huyo kwamba hakumpata mtoto, pale walipokubaliana kwamba mtoto angekuwepo, hakumkuta.
“Unasemaje?” aliuliza nesi huku akishtuka.
“Hakuna mtoto! Yupo wapi?”
“Si nilikwambia kwenye lile pipa nililokuonyeshea jana!” “Sikumkuta!”
“YoU must be kidding me,” (unanitakia) alisema nesi huku akionekana kuchanganyikiwa.
Hakutaka kubaki ndani ya hospitali, akatoka huku akiwa na presha kubwa, hakutegemea kusikia kile alichokisikia kwamba mtoto hakuwepo katika pipa lile na wakati alimuweka na kurudi ndani.
Alipotoka nje, akaelekea katika pipa lile, hakumkuta mtoto kitu kilichomchanganya. Hakuridhika kuangalia juu ya pipa tu bali akaanza kuangalia kila kona, hakikubadilika kitu, kila kona hakuona mtoto kitu kilichomfanya kuwa na hofu kubwa.
“Ila alikuwa hapa,” alisema nesi.
“Yupo wapi sasa?”
“Nilimuweka hapa,” alisema nesi na kuondoka mahali hapo, akaenda kwa walinzi getini, alijua fika kwamba kama mtoto alichukuliwa mahali pale ilikuwa ni lazima mtu huyo apite pale getini, akaenda mpaka kule, alipouliza akaambiwa kwamba kulikuwa na mwanaume aliyepita dakika chache zilizopita akiwa na mtoto.
“Mbona hamkumzuia?” aliuliza nesi huku akichanganyikiwa.
“Sisi tulijua ndiyo mtu wa mipango ndiyo maana tukaachana naye!” alijibu mlinzi mmoja.
“Mungu wangu! Tumekwisha!”
Nesi akarudi ndani huku akikimbia, kijasho chembamba kilikuwa kikimtoka, hakumjua mtu aliyemuiba mtoto huyo, alitetemeka kwa hofu kubwa, akawafuata wenzake, akawaambia kila kitu kilichotokea kwamba mtoto hakuwepo.
Kila mmoja alichanganyikiwa, wengine wakahisi kwamba kama wanataniwa kwani kila wapokuwa wakifanya dili la kuiba watoto walikuwa wakipelekwa huko na hakukuwa na mtu aliyekuwa akiwachukua, sasa ilikuwaje huyo achukuliwe?
Hospitalini kulikuwa ni kizaazaa, kitendo cha kutumia bastola humo kiliwafanya polisi kumkamata na kumpeleka kituoni ambapo huko akaelezea kila kitu kilichokuwa kimetokea.
Itaendelea
Akampigia simu, kitu cha kwanza kabisa alichokutana nacho ni malalamiko kutoka kwa mzee huyo kwamba hakumpata mtoto, pale walipokubaliana kwamba mtoto angekuwepo, hakumkuta.
“Unasemaje?” aliuliza nesi huku akishtuka.
“Hakuna mtoto! Yupo wapi?”
“Si nilikwambia kwenye lile pipa nililokuonyeshea jana!” “Sikumkuta!”
“YoU must be kidding me,” (unanitakia) alisema nesi huku akionekana kuchanganyikiwa.
Hakutaka kubaki ndani ya hospitali, akatoka huku akiwa na presha kubwa, hakutegemea kusikia kile alichokisikia kwamba mtoto hakuwepo katika pipa lile na wakati alimuweka na kurudi ndani.
Alipotoka nje, akaelekea katika pipa lile, hakumkuta mtoto kitu kilichomchanganya. Hakuridhika kuangalia juu ya pipa tu bali akaanza kuangalia kila kona, hakikubadilika kitu, kila kona hakuona mtoto kitu kilichomfanya kuwa na hofu kubwa.
“Ila alikuwa hapa,” alisema nesi.
“Yupo wapi sasa?”
“Nilimuweka hapa,” alisema nesi na kuondoka mahali hapo, akaenda kwa walinzi getini, alijua fika kwamba kama mtoto alichukuliwa mahali pale ilikuwa ni lazima mtu huyo apite pale getini, akaenda mpaka kule, alipouliza akaambiwa kwamba kulikuwa na mwanaume aliyepita dakika chache zilizopita akiwa na mtoto.
“Mbona hamkumzuia?” aliuliza nesi huku akichanganyikiwa.
“Sisi tulijua ndiyo mtu wa mipango ndiyo maana tukaachana naye!” alijibu mlinzi mmoja.
“Mungu wangu! Tumekwisha!”
Nesi akarudi ndani huku akikimbia, kijasho chembamba kilikuwa kikimtoka, hakumjua mtu aliyemuiba mtoto huyo, alitetemeka kwa hofu kubwa, akawafuata wenzake, akawaambia kila kitu kilichotokea kwamba mtoto hakuwepo.
Kila mmoja alichanganyikiwa, wengine wakahisi kwamba kama wanataniwa kwani kila wapokuwa wakifanya dili la kuiba watoto walikuwa wakipelekwa huko na hakukuwa na mtu aliyekuwa akiwachukua, sasa ilikuwaje huyo achukuliwe?
Hospitalini kulikuwa ni kizaazaa, kitendo cha kutumia bastola humo kiliwafanya polisi kumkamata na kumpeleka kituoni ambapo huko akaelezea kila kitu kilichokuwa kimetokea.
Itaendelea