Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #121
SEHEMU YA 94...
Siku hizo zikakatika, hakumuona Sarafina wala mtoto wake. Akarudi hospitalini, akalia sana, akakata tamaa na kadiri siku zilivyokuwa zikizidi kwenda mbele ndivyo alivyokuwa akizidi kuumia kitandani pale.
“Daktari!” alimuita daktari aliyekuwa akiingia na kutoka ndani ya chumba alichokuwemo.
“Unasemaje?”
“Naomba kalamu na karatasi!” alisema David kwa sauti ndogo, daktari akaondoka, ba baada ya dakika chache akarudi na kalamu, karatasi mikononi mwake, David akaichukua, akainuka kitandani pale, kwa tabu sana akakaa na kuegemea mtu kwa nyuma.
Alisikia mauamivu makali, alivumilia, alitaka kuandika vitu kwa ajili ya Sarafina, aliamini kwamba kamwe asingeweza kumuona ila aliamini kwamba maandishi yalikuwa yakiishi na ingetokea siku moja yangeweza kumfikia mwanamke huyo.
Kabla ya kuandika maneno yoyote yale katika karatasi ile, akatulia, akaangalia juu, mawazo yake yakaanza kurudi nyuma kabisa, tangu siku ya kwanza kuonana na msichana huyo, alikuwa mrembo, alimpenda, lakini kwa ujinga wake, kwa tamaa zake mwisho wa siku akampa mimba na kumshinikiza kuitoa kitu ambacho msichana huyo alikataa.
Kila kitu alichokuwa akikiwaza wakati huo, kiliuchoma moyo wake. Aliendelea kukumbuka mambo mengi, kumbukumbu zilizomuumiza ambazo zilimfanya kujuta zaidi na zaidi. Baada ya kukumbuka kwa dakika chache, akaanza kuandika maneno hayo.
Mpenzi Wangu Sarafina.
Nakumbuka siku ya kwanza nilipokuona, hakika ulikuwa msichana mrembo ambaye sikuamini kama ningeweza kuwa pamoja nawe. Nilikupenda kupita kawaida na nilipokwambia, ulijitambua, uliutambua uzuri wako, ukanikatalia lakini mwisho wa siku ukanikubalia.
Mpenzi Wangu Sarafina.
Nilikupata, nikakupenda, sikuwa na akili, nilikuwa kijana mwenye mambo mengi. Mbali na wewe nilikuwa na wanawake wengine, nilikuchukulia kama nilivyowachukulia wengine, sikukujali sana, nilikuchukulia kuwa mwanamke wa kupita, sikukuthamini inavyotakiwa. Nisamehe sana Sarafina.
Itaendelea.
Siku hizo zikakatika, hakumuona Sarafina wala mtoto wake. Akarudi hospitalini, akalia sana, akakata tamaa na kadiri siku zilivyokuwa zikizidi kwenda mbele ndivyo alivyokuwa akizidi kuumia kitandani pale.
“Daktari!” alimuita daktari aliyekuwa akiingia na kutoka ndani ya chumba alichokuwemo.
“Unasemaje?”
“Naomba kalamu na karatasi!” alisema David kwa sauti ndogo, daktari akaondoka, ba baada ya dakika chache akarudi na kalamu, karatasi mikononi mwake, David akaichukua, akainuka kitandani pale, kwa tabu sana akakaa na kuegemea mtu kwa nyuma.
Alisikia mauamivu makali, alivumilia, alitaka kuandika vitu kwa ajili ya Sarafina, aliamini kwamba kamwe asingeweza kumuona ila aliamini kwamba maandishi yalikuwa yakiishi na ingetokea siku moja yangeweza kumfikia mwanamke huyo.
Kabla ya kuandika maneno yoyote yale katika karatasi ile, akatulia, akaangalia juu, mawazo yake yakaanza kurudi nyuma kabisa, tangu siku ya kwanza kuonana na msichana huyo, alikuwa mrembo, alimpenda, lakini kwa ujinga wake, kwa tamaa zake mwisho wa siku akampa mimba na kumshinikiza kuitoa kitu ambacho msichana huyo alikataa.
Kila kitu alichokuwa akikiwaza wakati huo, kiliuchoma moyo wake. Aliendelea kukumbuka mambo mengi, kumbukumbu zilizomuumiza ambazo zilimfanya kujuta zaidi na zaidi. Baada ya kukumbuka kwa dakika chache, akaanza kuandika maneno hayo.
Mpenzi Wangu Sarafina.
Nakumbuka siku ya kwanza nilipokuona, hakika ulikuwa msichana mrembo ambaye sikuamini kama ningeweza kuwa pamoja nawe. Nilikupenda kupita kawaida na nilipokwambia, ulijitambua, uliutambua uzuri wako, ukanikatalia lakini mwisho wa siku ukanikubalia.
Mpenzi Wangu Sarafina.
Nilikupata, nikakupenda, sikuwa na akili, nilikuwa kijana mwenye mambo mengi. Mbali na wewe nilikuwa na wanawake wengine, nilikuchukulia kama nilivyowachukulia wengine, sikukujali sana, nilikuchukulia kuwa mwanamke wa kupita, sikukuthamini inavyotakiwa. Nisamehe sana Sarafina.
Itaendelea.