Sarafina - Mtunzi Nyemo Chilongani

Sarafina - Mtunzi Nyemo Chilongani

SEHEMU YA 148...

Kwa sababu walihitaji kitabu hicho kimfikie kila mtu, kikachapishwa kwa lugha nne, Kiingereza, Kifaransa, Kireno na Kiswahili na kiliandaliwa tayari kwa ajili ya kuuzwa duniani kote.

Kitabu kikachapishwa na Malaika kupelekwa nchini Marekani ambapo akavisaini vitabu vyote na kuanza kuuzwa. Yalikuwa ni mafanikio makubwa, kwa jinsi promosheni ya kitabu hicho ilivyofanyika, kila mtu akatamani kukisoma na hivyo kitabu hicho kuingiza dola milioni tano kwa wiki ya kwanza tu, pesa ambazo kwa thamani ya shilingi ya Kitanzania ilikuwa ni sawa na shilingi bilioni kumi.

Yalikuwa ni mafanikio makubwa, kilikuwa kitabu cha kwanza kuingiza kiasi kikubwa cha fedha kwa wiki ya kwanza tu. Watu walikinunua sana na kila aliyekuwa akikisoma, alilia kutokana na historia hiyo kumgusa kila mtu.

Yule Malaika mtoto wa mitaani, maisha yake yakabadilika, akaingiza mabilioni ya shilingi kwani ndani ya mwaka wa kwanza tu, kitabu hicho kiliingiza zaidi ya dola bilioni mbili, zaidi ya shilingi trilioni nne kwa pesa za Kitanzania.

Maisha yalibadilika, akafungua biashara zake huku zikisimamiwa na Richard aliyekuwa mzoefu katika biashara, hakutaka kuachana na Ibrahim, kwake, mwanaume huyo alikuwa kila kitu. Wakaamua kuishi pamoja katika jumba lao kubwa walilolinunua huko Mikocheni B, moja ya jumba kubwa lililokuwa na vyumba zaidi ya kumi na tano.

Malaika yule akawa bilionea na kilichokuwa kimempa pesa nyingi ni historia ya maisha yake ambaye baadaye aliiweka kwenye kitabu. Watu wengi walitaka kufahamu, msichana aliyekonda mno, aliyekaa kwenye kava la kitabu, aliyekuwa akiumwa kansa ya damu na sickle cell aliponyaje? Ili watu kujua hayo yote, ilikuwa ni lazima kununua kitabu na kusoma kitu kilichompa pesa nyingi msichana huyo ambaye aliamua kutoa asilimia kumi ya mauzo ya kitabu hicho kwa kuwasaidia watoto wa Kiafrika waliokuwa wakisumbuliwa na magonjwa mbalimbali duniani.
 
SEHEMU YA 149...

“Malaika! Mungu aliyaandaa maisha haya tangu ulipokuwa katika tumbo la mama yako. Alikuwekea kitu kimoja, ili uweze kuyafikia ilitakiwa kuamini. Namkumbuka mchungaji aliposema kwamba kama kweli unataka kufanikiwa ni lazima Mungu akupitishe katika tanuru la moto, kwenye hilo tanuru la moto kuna wengine watakata tamaa, wengine watapambana, na watu watakaovuka basi ndiyo watakutana na mafanikio ambayo Mungu aliwaahidi tangu wakiwa tumboni kwa mama zao,” alisema Richard huku akimwangalia Malaika.

“Nilizaliwa kuamini, nimekuwa nikiamini kwa kipindi chote cha maisha yangu. Nilijua kwamba kuna siku haya yaliyotokea yangetokea na hakika Mungu amefanya,” alisema Malaika na kumkumbatia Ibrahim ambapo ilipofika Jumamosi ya tarehe 03/07/2017 wawili hao wakafunga ndoa katika Kanisa la Living God lililokuwa jijini Dar es Salaam.

MWISHO
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom