Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Kaanza "vibaya". Hawatamruhusu kuchukua nafasi hiyo kwa sababu hawaelewi ataishia wapi. Angesubiri aingie kwanza au labda alitaka kuufikisha tu huo ujumbe.
 
Payback time......mambo ya mchakato kuelekea CHIMWAGA (2005)....

Amakweli harakati za MTANDAO zimeleta na kufungua wengi katika Tanzania yetu

Tanzanianjema
 
Nimeamsikia Nchimbi akisema kijana huyo hatapita,labda yeye siyo Nchimbi
 
Amesema kuwa mwekezaji aliyepewea kuendeleza jengo hilo amepewa umiliki wa asilimia 75 ya hisa wakati umoja huo ukibakiwa na hisa 25 tu wakati mwekezaji huyo hakutoa hata senti moja katika mradi huo.

Alisema alichofanya mwekezaji huyo (ambaye hakumtaja) ni kutumia hati za umiliki wa jengo na kiwanja hicho kuombea mkopo benki ambao anautumia kuendeleza jengo hilo.

Amesema kinachosikitisha zaidi ni sehemu ya mkataba huo kinachoeleza kuwa makubaliano hayo ni ya masiaha, ikimaanisha kuwa familia ya mwekezaji huyo itaendelea kula fedha kupitia mgongo wa Umoja wa Vijana wa CCM.


Amesema kama vile ambavyo viongozi wa UWT na WAZAZI walivyowajibishwa kwa kushindwa kusimamia mali za jumuiya hizo, lowassa na nchimbi nao wanapaswa kuwajibishwa au kuwajibika kwa kushindwa kusimamia maliz a UVCCM.

Nape amesema kwua ameamua kuwania nafasi hiyo ili kukisafisha chama kutokana na kuchafuliwa na mafisadi.

Kuna mambo mengine yanatisha katika nchi hii. Yaani wanasiasa wanasaini mkataba wa maisha!- forever mpaka siku ya kiyama! Hata viwanja vya nyumba vina mikataba ya miaka 99 itakuwaje huu uwe wa maisha? Ina maana kuwa hajaui kuwa mktaba wa kiwanja kile utaisha, na kulingana na maendeleo miji wakati huo inawezekana jangeo hilo likabomolewa?

Halafu wanampa mwendelezaji ambaye haweki downpayment!!

Hiyo ni hapa Tanzania tu; hata Kenya wangekatana masikio.
 
Mwenyewe anaahidi kwua safari hii yuko determined kuhakikisha kuwa anasafisha uchafu ndani ya chama. Sijui kama ni dhamira ya dhati au maneno ya kuombea kura tu. Tusubiri tuone

Mkuu yawe ya dhati au siyo kwanza hatapita hilo la kwanza tulitambue kabisa kwa sababu amegusa mabapo hapagusiki na tena haparuhusiwi kuguswa.wewe unamchokonoa Lowassa unategemea nini?Vile vile hayo siyo maneno ya kuombea kura.CCM waahidi fedha then watakupa kura.
 
Nimeamsikia Nchimbi akisema kijana huyo hatapita,labda yeye siyo Nchimbi
.................Si uchaguzi wao ni wa kidemokrasi jamani, iweje Nchimbi ndiye aamue yupi wa kupita na yupi asipite.


.................Kijana huyu kaanza siasa vizuri hata kama hatapata uongozi huko UWVCCM, lakini sijui mwisho wake utakuwaje kwani siasa za Tanzania ni za miujiza miujiza vile.
 
Huyu Nape anajiamini nini? mbona naona kama anagusa pabaya? hafahamu kama "Dk." Nchimbi anajifanya mungu mtu hapo UVCCM? anatafuta balaa gani kumnyooshea kidole mtu huyo na EL? Yetu macho na masikio tuone yatakayojiri!
 
Nimeamsikia Nchimbi akisema kijana huyo hatapita,labda yeye siyo Nchimbi

Ahaaa haaa, ilikuwa zamani siku hizi huo ubavu hana kwa sababu akina JK walishamtumia na hawana shida naye tena! Huyu Nape ana nafasi kubwa sana, and, to be honest, he could the best among those who have declared their intentions so far!.
 
Yetu macho kijana Nape, ila ingekuwa busara kimya kimya ukapiga kampeni, ukaukwaa then ukasafisha. Ungependwa na wazalendo.

WanaJF hivi Nchimbi bado ni kijana au ndo mmiliki wa UVCCM?
 
Ahaaa haaa, ilikuwa zamani siku hizi huo ubavu hana kwa sababu akina JK walishamtumia na hawana shida naye tena! Huyu Nape ana nafasi kubwa sana, and, to be honest, he could the best among those who have declared their intentions so far!.
Kitila,
Kila mtu anataka Nape Apite,ila kuna kitu nyuma..hawampendi nape..so fara waliochukua Fomu ni kama ifuatavyo

1.Jerry silaa
2.Musa Mnyeti
3.Beno Malisa


wengnie sifahamu...
 
Yetu macho kijana Nape, ila ingekuwa busara kimya kimya ukapiga kampeni, ukaukwaa then ukasafisha. Ungependwa na wazalendo. WanaJF hivi Nchimbi bado ni kijana au ndo mmiliki wa UVCCM?

Hili ni moja ya tatizo la watanzania, kama akiingia kimya kimya hatakuwa na deni la utekelezaji, ni lazima atuambie sasa anasimamia wapi ili nasi tujue na wapiga kura wake wajue.
 
Nami nina wasi na zengwe atakalopigwa na wazoefu wa fitna za siasa maana kwa sasa Dr na EL wameiva kwa fitna walizocheza 2005...sasa Nape namuonea huruma sana sana maana najuaa itakuwa ndio mwisho wake......sidhani labda kama waamue kudharau au labda kama ana back up kubwa ya wajumbe la sivyo.....ataangukia pua...watu wa fitna haoo ooh wanageuza "figures"kwenye deal kubwa na makashfa mazito sembuse hiyo?????jamaa wamekuwa wabaya sana jamani...duu CCM mmeliwa....mmewapandikiza wenyewe mnashindwa kuwang'oa.....
 
Mwana Mnauye

Hata kama watakunyima, lakini si umeshawaambia kuwa wanafanya ufisadi wa hatari. Asikubabaishe mtu bwana We endelea mbele!!!!!!! Wabane na zaidi. Kila kukija sababu ya kugombea beba hoja moja ya ufisadi uwaumbue nayo! Ebo!! Eti watu wengine wanakuhakikishia kuwa hutapata kura kwa kuwa tu umesema ukweli. Nakuhakikishia endelea kuwabana sana utapata kura nyingi tu!

Why????
Kwa nini????????
 
tena hata kama akikosa hiyo nafasi, akusanye ushahidi wa ufisadi anaouchukia halafu awaburuze mahakamani
 
Huyu Nape anajiamini nini? mbona naona kama anagusa pabaya? hafahamu kama "Dk." Nchimbi anajifanya mungu mtu hapo UVCCM? anatafuta balaa gani kumnyooshea kidole mtu huyo na EL? Yetu macho na masikio tuone yatakayojiri!
Mkuu,
Kwenye siasa hizi za maji taka,kauli kama aliyotoa NAPE ina maana kubwa sana,sidhani kama kakurupuka kuwavaa EL na EN, kuna secure base nyuma yake inayompa kusema aliyosema.
Kumbuka sisiem haiwezi kamilika bila kuwa UVCCM ktk kueneza propaganda zao.
Hata hao anaowatuhumu kuwa mafisadi hawawezi kumvamia tu bila kujua hii nguvu inayompa kutamka hivo inatoka wapi.
 
Nimemsikia Nchimbi akisema kijana huyo hatapita, labda yeye siyo Nchimbi

Mkuu Gembe,

mbona kauri hizi zinafanana na za kule kwa Jongwe (Robert Mugabe)! Hivi yale makeke ya Tanzania na Demokrasia yako wapi?
 
nape Nnauye Umethubutu, Sasa Kwa Msimamo Huu Ninapenda Niendelee Kukuheshimu Kijana Mwenzangu. Ni Vema Umethubutu Kuyazungumza Ya Uvccm Wewe Mwenyewe Kama Kada, Kimsingi Mzee Nchimbi Hapaswi Kumpiga Vita Nnauye Bali Kumuunga Mkono Na Pia Mtumishi Lowasa Hapo Atumie Hekima Tu Ingawaje Sidhani Kama Anahusika Na Hiyo Game Ya Jengo La Vijana. Mwisho Mkuu Nape Nikuhakikishie Tu Kuwa Mimi Ni Shabiki Wako Na Mwanamapinduzi Mwenzio Toka Mkoa Hapo.
 
Jamani mbona kina Lowassa na Nchimbi wanaonewa hivyo? CCM ni chama safi kabisa na haya yote ni maneno ya wapinzani. Nape angekuja na hoja yake hili la ufisadi is non starter.
 
Nimeamsikia Nchimbi akisema kijana huyo hatapita,labda yeye siyo Nchimbi

Hivi bado yuko India huyo kijana?

Maana ni heri abaki huko huko kwani kila aliyetangaza kugombea Uenyekiti wa UVccm...Basi Nchimbi aliwashughulikia.

Sasa wamesahau ya Chifupa.

Hata hivyo ni hatua nzuri..Ila utekelezaji wake utaiyumbisha ccm establish kwani huwezi kohoa kwa wanamtandao ndani ya ccm la sivyo wata kukolimba!

Wamesahau hata wabunge wenyewe wanasuwasuwa?

Ndio iwe mtu anayepiga kelele kwasababu tu anataka uongozi?

Hawa watu hawajuwi ccm imekufa?

Wasifikiri eti Nape Nnauye ndiye atakayekikomboa chama...Anahitaji ushirikiano.

Yeye anampigia kelele mtu ambaye hata mwenyekiti wa chama kamshindwa na hata NEC yenyewe ni mafisadi.

Mi naona ni kelele za kampeni tu!

Unless aungwe mkono na viongozi wakuu wenye ushawishi na ama wale wasiokuwa mafisadi!

Kwani tumeona kuwa mafisadi wana influence kubwa na ndio maana mara baada ya kashfa zote waliwatumia hao hao kina Nape na wengineo walioko UK kufuguwa matawi ya kuendeleza libeneke la UFISADI KWA STYLE YA KIMATAIFA!

Kama wana nia nzuri wafanye mapinduzi na sisi tutajiunga!

Lakini hizo kelele eti kwasababu tu ni mtoto wa Nnauye kasema...Ama mtoto wa Kawawa nk...Hilo halina mantiki!

Kama ni ufisadi ushapigiwa kelele sana tu na hadi CHINGA NA WALALAHOI NA HATA WANAFUNZI WANAUJUWA NA WALISHA MZOMEA HATA MKAPA NA MAKAMBA...

Bado zamu ya JK.

Na hao kina Nape pia wawe makini wasilete POLITICS KWANI WATAUMBUKA!
 
Back
Top Bottom