Mkandara, samahani sikupata muda wa kujibu kwenye hili.
Mwafrika,
Mkuu wangu ktk hili umekosea sana kwa sababu mimi simjui huyo Halima Mdee ndiye nani! wala sina mazoea wala ukaribu naye iweje nianze kufikiria kwamba wewe Mwafrika ndiye Mndee.
Mkandara, rudia tena kusoma nilichoandika na utaona point yangu
Mkuu utanisamehe lakini nakuomba sana unisikie hapa.. Tatizo la hoja zako nyingi zinahusu WATU yaani unatumia muda mwingi kuchambua na kufikiria watu wakati sisi tunazungumzia issues.
Mkandara,
Ukiongea habari za siasa, muda mwingi utakuwa unaongelea wanasiasa (watu kama unavyowaita wewe). Nimekusoma sana hapa ukiongelea kuhusu Mkapa, Nyerere, au yule guy aliyeteka ndege wakati wa Nyerere.
Katika yote hayo, sikuona ukiweka disclaimer kwamba unaongelea watu hao (kina nyerere na wenzake) kwa muda tu na kisha utarudi kwenye issues.
Issues unazozitaja hapa ziko kwa watu ninaowaongelea mimi.
Sijali wewe ni nani uwe Mbowe, Dr.Slaa au Mndee mimi sina mshirika katika habari yoyote zaidi ya kusoma hoja na kuzichanganua ktk mtazamo wangu. Mara kibao nimemkorofisha Zitto humu, nimezungumza mambo mengine kinyume cha ustaarabu pasipo kufikiria huyu ni nani isipokuwa maadishi ya mhusika.. That's me kwa hiyo unapohisi ama kudhani kwamba hata mimi nimenunua hiyo propaganda mkuu wangu inaonyesha wazi jinsi unavyojikisia mwenyewe.
Naona unataka kusahau kuwa kwa miaka yote hii (mitatu), nimekuwa (kwa nguvu zote) nakuwa upande wa zitto katika karibu kila kitu. Usidhani tu kuwa hili la kupingana naye limetokea tu angani. Mtizamo wangu kuhusu Zitto umebadilika sana kutokana na aliyofanya (au kutofanya) kwa siku za karibuni.
Mimi nipo kwa jina langu, Zitto yupo kwa jina la ke huyo Omar nasikia pia yupo kwa jina lake isipokuwa wewe tu.
Ukishajua jina langu then what?
Na kama sikosei ni wewe uliyetufahamisha kuhusu huyo Omar ni nani na wana uhusiano gani na Zitto, kulikuwa na haja au sababu ya kufanya hivyo!..Pengine hufahamu kwamba sisi wengine tunapenda sana kuyaona hayo majina bandia kwani unaweza kurusha madongo pasipo kuonea aibu mtu, Nitakushauri tu mkuu wangu hizi habari za kutoa ID ya mtu achana nazo kwani wewe mwenyewe unaelewa vizuri hasara zake..
Halafu huu ubishi wenu mkuu wangu wala hauna maana hata kidogo, yaani tunakusomeni kama vile tunatazama horror movie - Inatisha.
Mkandara,
Naona hapa umeamua kupingana na ukweli. Mimi sijawaambia Omar ni nani hapa. Omar anatumia jina lake na haikuhitaji mimi kumtambulisha. By the way, kabla sijasema chochote kuhusu Omar, Zitto alimtambulisha hapa JF kwa kuwaambia wana JF mambo yote makubwa aliyofanya Omar - likiwemo la kufanya kazi na SAS.
Hayo mengine inaonekana unafanya selection tu ya nini cha kuamini na kipi cha kutoamini.