Safi sana wabunge wa UKAWA

Safi sana wabunge wa UKAWA

Kama ni hivyo kwanini wasirudi majimboni basi wakawaambie wananchi sababu ya kutokaa bungeni?

Sasa kule kwenye mabaa wanamuwakilisha nani

Huko majimboni watatumia njia gani kuwaambia wananchi hizo sababu za wao kutoka ndani ya bunge kila wakati kiti kikikaliwa na NS?
 
Maumivu yenu tulikwisha yasikia kila kona ya nchi hii mkitaka muonewe huruma. Sauti hizo zimetolewa na Mbatia akitaka viongozi wa ccm waingilie kati kukutanisha pande husika. Sauti nyingine za maumivu ni kutoka kwa Kubenea akitangaza kususa kusalimiana na wabunge wa ccm. Lengo ni waungwana waingilie kati ili adhabu ipungue. Kilio cha tatu kimetolewa na bavicha kususa kushirikiana na vijana wa ccm pia lengo ni kuomba msaada kwa waungwana watoe msaada ili hawa wabunge waingie bungeni.
Kwa kuwa hilo ni janga la kujitakia huwa mtu apewi pole bali huonywa kuacha michezo ya hatari. Hakuna hata kiongozi wa dini aliyejitokeza kuongea nao angalau wapate kisingizio cha kusema tumerudi kwa sababu ya ushauri wa baba askofu.. au shekhe.... Mmeachwa mlinywe mliolikoroga.
Leo Mbowe alikuwapo. Kuacha kususa siku ambayo yeye kafika ingeleta picha mbaya hivyo tunachotegemea ni kuendelea kuona mbwembwe za namna ya kutoka.
Maumivu mnayo na huu ujinga umewaumiza sana wabunge wa chadema. Leo huenda ikawa siku ya 27 ya kususa. Majimbo hayana ahadi mahususi ya serikali kutoka kwa mbunge wao, mbunge hana posho kwa siku zote hizo. Saikolojia ya wabunge haina utulivi pindi wanapoona NS anaingia na kuwaanzishia safari ya kuzurura bila lengo. Pia akili haitulii pale mbunge anaposhindwa kiwasilisha kero za wananchi wake ili zipatiwe suluhu na serikali. Athari wanazokubwa sana
Maneno yako ni sawa na maneno ya wakoloni wakati tunadai uhuru hivyo sikushangai.
 
Mwenyenzi Mungu tunakuomba uendelee kuwajalia nguvu na hekima wabunge wetu wa UKAWA,wao ndio watetezi wetu waliofukua uozo na ufisadi uliokumbatiwa na chama tawala.Amin.
NA baadaye kumkumbatia Fisadi
 
hivi hao wabunge wa ccm wameshindwaje kujitetea viinua mgogo vyao kukatwa kodi au wamelegea baada ya kuambiwa Makufuli amekubali kukatwa kodi?na kama wanaona bajeti walioipitisha kwa kishindo ni nzuri kwa nini wanawalaumu UKAWA kutoka?na kama bajeti inamatatizo wanashindwaje kutoa hoja? ina maana wao kwenye matatizo wanawategemea tu,wabunge wa UKAWA ndio watoe hoja?kwa hio wanataka kutuambia kwamba wao ni watu wa ndio tu?
 
Siasa za Tanzania kwa wapinzani ni ngumu.....ninachojua haya yanamwisho wake. Huwezi kutumia ubabe na kiburi ktk uongozi mwisho wako ukawa wa neema. Haijatokea na haitatokea...

Tumenyanyaswa vya kutosha.....

Nawatia moyo wabunge wa UKAWA, ninawaelewa; watanzania wanaoipenda nchi yao wanawaelewa.....
 
Mungu ataamua kilio chetu maana ccm wana nguvu za polisi
Hii tangu 1995 haya maneno mnayataja tu. Na mbinu yenu ya mwisho ilikuwa kumchukia lowassa kuhubiri udini na ukanda. Na sasa utasikia tu na utaiona CCM inaongoza mpaka unazeeka.
 
Kuna taarifa kuwa wabunge wanawake wa UKAWA wameanza kuwatumia sms wabunge wanaume wa CCM ili wawasamehe kwa kauli alizotoa Kubenea
Huenda hata kile kibalaghashia ilikuwa ni kiashilio cha kumpuuza Kubenea.
 
Safi sana ukawa mnanikumbusha kipindi kile mwalimu kilaza akiingia darasani kufundisha somo asilolimudu tunapishana nae mlangoni Necta ikija wanaume tunapiga banda(A) waliokuwa wanabaki kumsikiliza wanapigwa miswaki tu(f)
 
Wabunge wa upinzani almaarufu UKAWA waendelea kususia vikao vya bunge wakiongozwa na kiongozi wao Mh. Mbowe.

Inasikitisha sana kwa wapiga kura wetu wito wangu wakae meza moja ya mazungumzo kumaliza mgogoro huu.
Juzi kuamkia jana ITV walisema ilikuwa ni siku ya 25. Angalia rekodi yako utusaidie na sisi wapenda kusema ukweli. Kama huna uhakika tumia maneno yatakayomaanisha hivyo.
 
Hahaha, ukawa nadhani watakua wanaugua ugonjwa wa akili, maana Mh. Dr. JPM siku anafungua bunge walitoka hivyo hivyo tena kwa mbwembwe kibao wakisema hawamtambui, ila baadaye wakaja mtambua. Na kila mwananchi anaona uwezo wa kufikiri wa wapinzani ni 0%.

Kuwa basi na akili yako hata kidogo kila kitu unataka kushikiwa. Ile wametoka wakati rais anazindua bunge walikua hawamtaki shein wewe unaongea utumbo wako wa bata hapa hata hujui dunia inavyokwenda. Pole sana Lumumba jinsi posho inavyo wasumbua ina hivi imeshuka toka buku saba mpaka buku mbili kweli hali ni mbaya
 
Hii hali sio ya kufurahia hata kidogo kwa pande zote mbili.Maadui wanatuona
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom