Ubungoubungo
JF-Expert Member
- Jul 28, 2008
- 2,502
- 743
Tanzania imekuwa kimbilio la amani kwa mataifa mengi kama Rwanda, Burundi na Congo kwa miaka mingi. ukienda mkoa wa kagera hata kigoma, wakimbizi hadi wamekuwa raia, tumewalisha na kuwapa maeneo hadi ya kulima...lakini utashangaa mtu kama PAUL KAGAME, asiye na shukran, amesahau yote hayo. labda kwasababu tuliwapokea wakimbizi walio wengi wahutu?...mbona wakimbizi wa kitusi wengi tu tumekuwa tukiwapokea tangu miaka ya 1950? tumewapokea, nimezaliwa mimi nikiona wakimbizi wapo hapa tz na kuambiwa wametoka Rwanda na Burundi. tumepokea watusi na wahutu kwa miaka mingi, lakini angalia kagame anavyokuja kututukana sisi watz na rais wetu kana kwamba hatujawahi kuwapatia makazi kipindi wanakimbia kifo.....SHUKRAN YA PUNDA SIKU ZOTE NI MATEKE.