Rufaa ya Babu Seya, tumuombee atoke?

Rufaa ya Babu Seya, tumuombee atoke?

tumuombe mungu mpe malipo ya aliyoyafanya,mungu mjuzi wa yote anajua yenyekuonekana kwa macho na yaliyojificha ndani ya nafsi
 
bado nashangaa waliwezaje kutembea pamoja nakukandamizwa mbele na nyuma. ?

Naelewa sana concern yako. Lakini inaniwia vigumu sana kuamini kwamba ushahidi uliotolewa na watoto ulikuwa ni wa kutunga!
She said one day as she was going to school, Babu Sea who was latter identified to be the 1st appellant called her, asked her where she lived and with whom. He then asked her if she was being given school money, to which she replied that it was not daily. The 1st appellant is alleged to have given her chewing gum and promise that he would be giving her money. Then one day as she was going home from school, the 1st appellant called her, gave her a soda, took her into his room, told her to close her eyes, tied her with a black peace of cloth over her eyes, undressed her, applied an ointment in her private parts and raped her. During the process the 1st appellant also told her to suck his penis, which she did.

She was not alone. She told PW 2 that she had gone to the 1st appellant’s house with her friends whom she mentioned. After she had been told this sad story, PW 1 did a visual examination of PW 2’s private parts and found fresh blood and pus oozing there from. Her immediate reaction was to take PW 2 to hospital where she was turned down and told that this was a police case. At around 8.00 p.m. of the same date 9/10/03 she reported to Urafiki Police Station, was given a PF 3 with which she took PW 2 to Mwananyamala Hospital after being referred there from Magomeni Hospital. Examinations revealed that PW 2 was infected with gonorrhea. She was treated.
 
lakini kwa nini tunaomba atoke?kwamba hajafanya kosa au? kwamba ametumikia vya kutosha au? kwa sababu anaonewa au?
siamini kama sheria ipo.......kama ipo tuiache itende kazi yake kama haipo basi tuwaache wakubwa wafanye wajuavyo.................
 
Ujue hii habari ya babu Seya wala haileweki, wengine wanasema kweli alifanya hayo makosa na watoto wake.
Ila kuna vitetesi huku mitaani kwamba hakufanya, ila kuna mtu mmoja ni mkubwa hapa nchini ndio kaamua kumuweka ndani yeye na watoto kwa sababu babu Seya alikuwa anamnyemelea mke wa huyo mkubwa flani. Hivyo eti hata wale mashahidi ni wakupikwa.

kwa mujibu wa magazeti ya jana 3/12/2009 eti babu yesa anasema kunamwanamke alimtema akamwambambi lazima atamkomesha, hata hivyo mitaani kuna habari nyingi sana mojawapo ikiwa ni hiyo ya kigogo kuamua kumkomesha

mimi binafsi haikuingia akili kwamba hilo swala linaweza kufanywa na wana familia wote , haki inawza kuwa ilipindishwa katika kesi ya awali na inaweza pia kupindishwa kunye rufaa wengi wakaamini kwamba alitenda kosa hilo na ndipo utakapoona watu watakavyomponda vibaya

ila nasikia wakili Marando watu walimshangilia sana jana wakamwita eti simba wa yuda. binafsi naomba haki itendeke maana kama watahukumu kwa haki basi ikiwa alitenda atahukumiwa kwa matendo yake na ikiwa hakutenda basi vile vile
ila nimejiuliza ikiwa atashinda hii rufaa na kuja uraina atakuwa ni mtu wa namna gani maana ameteka hisia za watu wengi sana kwenye hii kesi yake na inavyooneka watu wengi wanamwonea huruma wanafikiri kuwa pengine hakutenda kosa hili tusubiri ila nina hamu na mwishao wa kesi hii kwani kuna mambo ya kujifunza hapa katika maisha
 
tanzania yetu.............nchi ya furaha
 
lakini kwa nini tunaomba atoke?kwamba hajafanya kosa au? kwamba ametumikia vya kutosha au? kwa sababu anaonewa au?
siamini kama sheria ipo.......kama ipo tuiache itende kazi yake kama haipo basi tuwaache wakubwa wafanye wajuavyo.................
Hapa tunaangalia sheria za kibongo zinavyoendeshwa kibongo bongo, ukifuatilia Marando alivyoongea jana, utaona kuwa wanaonewa tu, na wanastahili kutoka hata leo.

Pia na sisi ni watuhumiwa wa kusingiziwa watarajiwa, lazima tuangalie vizuri haya mambo.

Kumbuka Bw, Mahumba, alisingiziwa hivi na alipokata rufaa ikaonekana alisingiziwa, akaachiwa, hapa tunaangalia je wanaotafsiri sheria zetu wanatenda sawa?
 
Dunia hii imejaa mambo ya ajabu sana. Great people do great mistakes!. Nilipata kusoma ile hukumu ya mwanzo ya Babu Seya na wanawe. Kwa ushahidi ulivyokuwa ni vigumu sana kuamini kama haya mambo waliyotuhumiwa nayo yote ni ya kupika/kupangwa tu. Na hata ukisoma utetezi wao (kupitia wakili wao) hakuna mahala wanalalamika au wamemtaja mtu kwamba amewa'frame'.

Binafsi siamini kama wanaweza kushinda hiyo rufaa na wakaachiwa huru. Labda adhabu inaweza kupungua tu.


bora unyamaze wewe..inaonekana hata hujafuatilia kesi...ametajwa mwanamke aliekuwa inasemekana amem-frame..
 
bora unyamaze wewe..inaonekana hata hujafuatilia kesi...ametajwa mwanamke aliekuwa inasemekana amem-frame..

Inawezekana upo sahihi kwamba sijaifuatilia hii kesi! Katika utetezi wao wa awali huyo mwanamke hakutajwa. In fact Babu Seya alikuwa anajitetea kwamba 'hasimamishi' na hivyo asingeweza kuwabaka/lawiti hao watoto!. Kwenye rufaa ya mwanzo ya Nyage sikuona kama aliiraise hilo jina la huyo mwanamke anaedaiwa kwamba alimframe. Ninavyojua Marando baada ya kuchukua hiyo kesi kutoka kwa Nyange alifanya marekebisho kwenye rufaa ambayo awali ilipelekwa na Nyange, pengine hilo la huyo mwanamke ni mojawapo.
 
Kwa mujibu wa jinsi kesi ilivyokwenda jana na maelezo ya Wakili Mabere Marando mimi ninasema Babu Seya na wanae wataachiwa kwani kulikuwa na ukiukaji mkubwa wa kanuni za uendeshaji mashtaka. Na kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa Upande wa Mashtaka haukuthibitisha hatia ya washtakiwa bila ya kuwepo mashaka yoyote yale ya msingi. Lakini ajuaye ukweli wote ni Mungu ila sisi wanadamu mizani yetu ni hiyo inayodai uthibitisho bila mashaka yoyote yale ya msingi kitu ambacho hakikuwepo.

kesi ya babu seya ilivyonguruma mahakama ya rufani leo

Nguza Viking a.k.a Babu Seya (kulia) na
wanawe watatu wakiwa kizimbani


Mwanamuziki Nguza Vikingi, ambaye anatumikia kifungo cha maisha baada ya kukutwa na hatia ya kulawiti na kubaka watoto 10, amedai kuwa hukumu kesi hiyo dhidi yake ilikuwa ni kisasi cha mpenzi wake aliyemuapia kulipiza kisasi, baada ya kuachana naye.

Hayo yalijulikana leo katika Mahakama ya Rufaa Tanzania, wakati mahakama hiyo ilipokuwa ikisikiliza rufani ya mwanamuziki huyo na watoto wake, waliopinga kuwa wakipinga hukumu hiyo ya kifungo cha maisha, iliyotolewa na Mahakama ya HAKIMU Mkazi Kisutu.

Mbali na hilo imedaiwa kuwa Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Addy Lyamuya alitoa hukumu kwa mwanamziki huyo pamoja na watoto wake kwa kutumia mawazo yake binafsi.

Katika rufani hiyo, Nguza (babu Seya) pamoja na watoto wake - Papi Ngunza, Nguza Mbangu na Francis Nguza - wameiomba mahakama hiyo, kupitia mwenendo mzima wa ushahidi uliopelekea wao kutiwa hatiani na kusababisha kuhukumiwa kifungo hicho.

Wakili Mabere Marando ambaye anawatetea washitakiwa hao, aliwasilisha hoja hizo mbele ya Jopo la Majaji watatu lililokuwa likiongozwa na Nathalia Kimaro pamoja na wenzake ambao ni Jaji Mbarouk Salim Mbarouk na Jaji Salum Massati.

Marando alidai kuwa Babu Seya alikuwa na mpenzi wake aliyemtaja kwa jina la Farida ambaye mara baada ya kuachana alimuambia kuwa atamkomesha ambapo alidai kuwa kunauwezekano kesi hiyo ikawa ni kisasi cha mwanamke huyo ambaye alitoa vitisho hivyo.

Aliendelea kudai kuwa kunauwezekano wa Farida kuwafundisha watoto hao wanaodaiwa kubakwa, kusema uongo Mahakamani ili kuweza kumfunga Babu Sey na wanawe kama kisasi alichodai kumlipia.

Awali Marando alidai Mahakamani hapo kuwa upande wa utetezi unaondoa sababu za kutaka rufani hizo ambazo ni sababu ya 1,2,3,5,6,7,8,11,14 na 15 ambapo alidai kuwa katika rufani hiyo wataanza na sababu namba tisa kutokana na misingi ya kisheria.

Alidai kuwa sababu hiyo inaeleza maelezo ya anayeitwa Mahakamani kwa ajili ya kutoa ushahidi ambapo alidai kuwa mujibu wa sheria za motto kutoa ushahidi Hakimu ananatakiwa kumuhoji kabla ya kutoa ushahidi wake ili aweze kuona kama motto anauelewa gani juu ya kiapo cha ushahidi.

Marando alidai kuwa katika rufani ya awali katika Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam, nchini ya Jaji Thomas Mihayo alisema kuwa utaratibu uliokuwa umetumiwa na hakimu aliyekuwa ametoa hukumu hiyo ilikuwa na makosa kutokana na watoto ambao walitoa ushahidi kutohojiwa kabla ya kutoa ushahidi wao.

Alidai kuwa mahojiano ya awali na mtoto anayetoa ushahidi ni ili kupata maamuzi na kujua kama mtoto anajua maana ya kiapo ambapo mahojiano hayo baina ya hakimu na mtoto yanatakiwa kuhojiwa.

"Kwa kutozingatia mambo hayo ushahidi ambao utakuwa umetolewa na mtoto huyo utakuwa batili na hauna maana yoyote," alidai Marando.

Aliongeza kuwa muelekeo wa Jaji Mihayo aliyesikiliza rufani hiyo kwa mara ya kwanza haukuwa mzuri kutokana na sheria mbalimbali alizozitumia kugongana ambapo alidai kuwa kutokana na hali hiyo Jaji huyo alifanya kosa kisheria.

Wakili huyo alidai kuwa mashahidi 10 kati ya tisa wa upande wa Jamuhuri ambao walitoa ushahidi wao hawakuapishwa wala kuangalia uwezo wao kama wanaelewa maana ya kiapo.

Pia alidai kuwa katika rufani iliyosikilizwa na Jaji Mihayo alisema kuwa hakimu aliyetoa hukumu hiyo kwakuangalia ushahidi wa pande mbili ambapo alidai kuwa Jaji huyo alikosea kwakua ushahidi wa utetezi haukuangaliwa vyema.

" Katika nyaraka rejea zilizotumiwa na hakimu aliongeza mawazo yake binafsi kutokana na kupingana na maelezo ya mashahidi, katika ukurasa wa 532 mstari wa saba katika hukumu hii, hakimu anapingana na shahidi aliyejitambulisha kwa jina la Lubaba ambaye mama yake ni Mzaramo na baba yake Mkongo.

"Lakini katika maelezo ya hakimu anaonyesha kijana huyo ni Mzaramo wakati si kweli, hiyo yote inaonyesha jinsi gani hakimu alivyokuwa akiweka mawazo yake binafsi," alidai Marando.

Marando alidai kuwa kwa muda wa miaka 30 ambayo amefanya kazi ya uwakili hajawahi kuona hukumu ya namna hiyo ambayo hukumu inatolewa kwa kufuata mawazo ya hakimu badala ya ushahidi wa pande mbili.

Aliendelea kudai kuwa hakuna ushahidi ambao ulionesha mshitakiwa wa pili alibaka au kulawiti kabla au baada ya kufanya safari zake za kimuziki katika mikoa ya Mwanza na Arusha ambapo alisema kuwa hakimu aliweza kuweka mawazo yake binafsi ili kuwezesha mshitakiwa huyo kuwa na hatia ya kumfunga gerezani.

"Mbali na hayo mshitakiw ahuyo wa pili alidai kuwa kati ya Agosti na Septemba alikuwa akirekodi albamu yake na mwanamuziki Lady Jee dee , lakini badala ya hakimu kuandika maelezo hayo na matokeo yake aliandika ‘So what?'," alidai wakili huyo.


Alidai kuwa hakimu huyo hakuandika maelezo ya mashahidi wa upande wa utetezi na badala yake aliandika idadi ya mashahidi ambao walifika kutoa ushahidi wa upande wa utetezi ambapo wakili huyo alihoji hali hiyo iliyofanywa na hakimu huyo.


Wakili huyo alidai kuwa kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa na watoto ambao wanadaiwakufanywa vitendo vya ubakaji na kulawitia walitaja baadhi ya watu ambao hawakuweza kuitwa na upande wa mashitaka kufika Mahakamani kwa ajili ya kutoa ushahidi wao.

Alidai kuwa watoto hao walimtaja Mangi ambaye anauza duka ambalo lipo karibu na nyumbani kwa Babu Seya ambaye anadaiwa kuona watoto hao wakati wakiingia na kuchukuliwa na mshitakiwa huyo wa kwanza na pia anadaiwa kusikia wakati watoto hao wakilia wakati wakifanyiwa vitendo hivyo.

Pia mbali na Mangi pia ilidai kuwa watoto hao walimtaja dada na bibi ambao walikuwa wakikutwa katika nyumba hiyo ambapo Marando alihoji kutokuitwa kwa watu hao kufika kutoa ushahidi ili kuweza kuthibitisha madai hayo.

"Kitu cha kushangaza zaidi ni madai ambayo yalitolewa kuwa watoto hao walifanyiwa vitendo hivyo tarehe 11 Oktoba wakati siku hiyo ilikuwa ni Jumamosi na pia mshitakiwa wa kwanza alikuwa amekamatwa na katika maelezo ya watoto hao inadaiwa kuwa walikuwa wakifanyiwa vitendo hivyo wakati wakitoka shule.

"Je siku hiyo ya jumamosi mbona haikutajwa wakati maelezi yanadai kuwa walifanyiwa siku za katikati ya wiki, Jamuhuri ingeweza kufanya uchunguzi ili kuweza kubaini mtu ambaye aliweza kuwabaka watoto hao na si kama jinsi inavyodaiwa," alidai.

Alidai kuwa baadhi ya shahidi mtoto alishindwa kumtambua Babu Seya na mwingine alikanusha kubakwa na mshitakiwa wa 3 na 4 ambapo alidai kuwa hakimu aliandika kuwa kutokana na watoto hao kujuana alihisi kuwa ni lazima watoto hao walibakwa licha ya watoto hao kutothibitisha.

Aliongeza kuwa katika kielelezo kilichotolewa na Hospitali ya Mwananyamala kilidai kuwa mtoto mmoja aliambukiza Kisonono ambapo washitakiwa hao kupitia mawakili wao waliomba kwenda kuwapima washitakiwa hao ili kuweza kuona ni mshitakiwa yupi aliyekuwa amemuambukiza ugonjwa huo wa zinaa.

Alidai kuwa licha ya ombi hilo upande wa Jamuhuri ulikataa kuwapeleka washitakiwa hospitali kwa ajili ya kuweza kuwapima ugonjwa huo ambapo alidai kuwa mtoto mwingine katika maelezo yake alidai kuwa alilazimishwa na Babu Seya kumkamua vipele vilivyokuwa katika sehemu zake za siri vilivyokuwa vikitoa usaha na maji.

Hata hivyo wakili huyo alidai kuwa upande wa Jamuhuri haukuwa tayari kuwafikisha watuhumiwa hao katika kituo cha afya ili kuweza kuthibitisha madai hayo yaliyokuwa yamedaiwa.

"Mshitakiwa wa nne ambaye alikuwa ni mwanafunzi naye pia anadaiw akushiriki katika vitendo hivyo lakini upande wa Jamuhuri haukuwahi kumuita Mkuu wa shule ya sekondari ya Mbezi ambayo alikuwa anasoma ili kuweza kuthibitisha kama mwanafunzi wake alikuwa hafiki shule.

"Lakini mambo yote hayo hayakuweza kufanywa wakati kila mmoja anaelewa kuwa muda ambao anatoka mwanafunzi huyo watoto hao wanakuwa tayari hawapo lakini hazikuweza kufanyika jitihada mbalimbali," alidai.

Alidai kuwa katika jarada la kesi hiyo, mashitaka mawili yalikuwa yakiingiliana ambapo shitaka moja lilidai kuwa watoto hao walifanyiwa vitendo hivyo Oktoba ambapo shitaka jingine lilidai kuwa watoto hao walifanyiwa vitendo vinvyo kwanzia April hadi Oktoba.

Alidai kuwa katika maelezo ya mashahidi hakuna shahidi aliyedai kuwa alifanyiwa vitendo hivyo kati ya Aprili hadi Julai na kwamba kwa kipindi hicho ambacho kimetajwa mshitakiwa wa 2 na 3 walikuwa wakishinda katika kambi yao ya mazoezi ya FM Academy.

Naye wakili wa upande wa Jamuhuri uliokuwa ukiongozwa na Justuce Mlokozi alikili watoto hao kutorekodiwa na pia kutofanyiwa kiapo ambapo alidai kuwa Mahakama iliegemea ushahidi wa Jamuhuri na kwamba hata kama kulikuwa na makosa madogomadogo yanaweza kutibika chini ya sheria namba 388 ya mwenendo wa mashahidi.

Mlokozi alidai kuwa waliamua kuwaleta watoto katika ushahidi huo kutokana na wao ndio walikuwa walengwa zaidi na wakati wakifanyiwa kitendo hicho hakuna watu wengine waliokuwa wakiona.

Aliendelea kudai kuwa kuhusu kutofautiana kwa miezi katika jarada la kesi hiyo alidai kuwa hakukuw ana tarehe maalum ambayo watoto hao wlaifanyiwa vitendo hivyo na kwamba walikuwa wakifanyiwa kwa nyakati tofauti.

Aliongeza kuwa kuhusu kusafiri kwa mshitakiwa wa 2 alidai kuwa hiyo si hoja kuwa hajatenda kosa ambapo alidai kuwa anaweza kuwafanyia kipindi ambacho anakuwa hapa jijini Dar es Salaam na kudai kuwa kuhusu Farida haiwezekani kuwafundisha watoto wote kusema uongo kama inavyodaiwa na utetezi.

Akihairisha kesi hiyo Jaji Kimaro, alisema kuwa Mahakama itatoa tarehe ya hukumu ya rufani hiyo baada ya kusoma maelezo yote yaliyotolewa na pande hizo mbili ikiwa ni pamoja na nyaraka rejea zilizotolewa.

Wakati kesi hiyo ikisikilizwa umati mkubwa watu ulimiminika Mahakamani hapo kwa ajili ya kusikiliza rufani hiyo ambapo watu walijaa katika chumba cha Mahakama na katika naeneo ya Mahakama hiyo.

Mara baada ya kuhairishwa kwa kesi hiyo Marando alionekana kuwa mfalme na mkombozi kutokana na maelezo ambayo aliweza kuyatoa jambo ambalo liliwafanya mashabiki wa wanamziki hao kumita Simba wa Yuda Simba wa Yuda huku wakimpigia makofi.

Licha ya hayo wakati rufani hiyo ikiendelea hali isiyo ya kawaida watu walijikuta wakipiga makofi wakati ndani ya chumba hicho kilichokuwa kikitumiwa wakati wa kusikiliza rufani hiyo.

Babu seya na watoto wake watatu walihukumiwa kifungo cha maisha mwaka 2004, baada ya Mahakama kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na mashahidi wa upande wa Jamuhuri dhidi ya kesi ya kudhalilisha kijinsia watoto wa kike.

Kesi hiyo iliyovuma kwa wakati huo ambayo ilikuwa ikisikilizwa na kutolewa hukumu na Hakimu Mkazi Addy Lyamuya ambaye amestaafu hivi karibuni.

 
Kuleni recorded hiyo movie hiyo Babu Seya akitoka mahakamani.

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=CUfLZv77YC8&feature=player_embedded[/ame]
 
[B said:
MARANDO[/B];686690]aidha, alidai mmoja wa watoto hao alidai kubakwa hadi kutoka damu, lakini taarifa ya daktari iyowasilishwa mahakamani hapo ilionyesha kuwa mtoto huyo ni bikira na wala haonyeshi aliwahi kubikiriwa wala kuingiliwa kinyume na maumbile, hivi tujiulize, kibaiolojia kweli inawezekana mtoto wa miaka sita abakwe na wanaume hawa (warufani) nyuma na mbele halafu mtoto huyo aweze kutembea? Haiingii akilini hata kidogo, nasema kesi hii ni ya kutunga, kwani hata mwanamke mwenye umri wa utu uzima akifanyiwa unyama huo hawezi kutembea," alidai marando.
.
ni kweli mtoto wa miaka sita - nane abakwe mbele na nyuma atembee, mmh amakweli dunia inashangaza.
 
ni kweli mtoto wa miaka sita - nane abakwe mbele na nyuma atembee, mmh amakweli dunia inashangaza.
Wale wote waliotunga/kutengeneza kesi hii, na walio hukumu isivyo sahihi walaaniwe, hata hivyo Mungu yupo, Babu seya na wanawe atawajalia watatoka na kuungana na familia zao.
 
hapahitaji maombi, tunataka sheria ifuatwe ili haki itendeke
 
ni kweli mtoto wa miaka sita - nane abakwe mbele na nyuma atembee, mmh amakweli dunia inashangaza.


...Pamoja na yote haya,mimi bado naona hii KESI ni nzito sana,na hata kuipangua kwake ni ngumu sana,watu tusifikirie hii kitu ni rahisi hivi,tatizo linakuja ilikuaje huyo wakili wa kwanza wa babu SEYA hakuchalenji kiukwelii hii kesi baada ya kukata RUFAA????,manake alipolainika pale mwanzo na ushahidi ukawa CEMENTED kwa kiasi hiki,mzee kuchomoka hapa ni ngumu sana,,,Unajua kwa level iliofikia kesi hii,ni majaji kuchukua ushahidi uleule wa hukumu na rufaa yao halafu wautolee maamuzi mapya,sijui hii kama inaweza ikawapa fikra mpya kama wengi tunavyopenda iwe.
...Mi kwa ushahidi huu,sikuelewa ni kwa nini huyo Mheshimiwa Hakimu aliamua kuwafunga hawa jamaa kama hivi bila kuangalia au kujiuliza aliwezaje KUVIKAMUA vitoto hivyo,tena wakati mwingine vinasema vilikua VIKISULUBIWA tena vikiwa vimepangwa foleni ati mpaka kwenye godoro la chini,sijui ilikuaje hapo,ni kesi ngumu wadau,acha tuone.
 
In real sense ni nguma kuamini kuwa familia nzima inaweza kuwa na tabia aina 1. Yani baba na watoto wake wote kweli wawe na tabia 1 hata 1 wao asiwe ni tofauti...!! Kesi yenyewe ilivyopelekwa pelekwa!! ingekuwa kesi za mauaji ya albino zote zingeshikiliwa bango kama ilivyoshikiliwaga hii...! Maalbino wangekuwa na amani kweli!! TUOMBE SHERIA ISHIKE MKONDO WAKE.
 
"Peace is not the absence of war but the presence of justice"-Harrison ford

If there was no justice, no one is safe in Tanzania!
 
Back
Top Bottom