Haaaaaa.Haya maaskari sijui yakoje sijui yanawaza nini. Leo mlinzi was getini nawapa Elimu nyie mabregedia masacp na macopolo .Kwanza kaa kimya soma kwa makini sana.Majeshi yote ni Idara ndani ya Wizara zake Hivyo msijione bora sana bosi was mkuu wa majeshi ni katibu mkuu wa Wizara na Bosi wa IGP ni katibu Mkuu tu baada ya hapo Waziri halafu Rais sasa msijone miungu watu hapa nyie sawa tu wafanyakzi wengine wa umma acheni mbwembwe. Sasa nawafafanulia kuhusu vyeo vyenu ni kwamba kazi za mwenye nyota moja Jeshi la Wananchi ni sawa tu na Jeshi la Polisi tofauti ni utendaji tu anzieni kwenye paredi ni nani anakagua wachafu na wasafi ni nani anawakagua malindoni ni nani anaongoza platoon ni nani anaongoza mkoa kanda mpaka nchi utagundua alama zao kwenye mabega zinafanana. Twendeni kwenye Ushaidi sasa. Nini maana ya Jeshi,Mwanajeshi,kazi za vyeo vyao
Ibara ya 151:ya katiba ya Tz
Jeshi" maana yake ni lolote kati ya majeshi ya ulinzi na ni
pamoja na jeshi lolote jingine lililoundwa na Katiba hii au
kwa mujibu wa sheria na linalotawaliwa kwa amri ya51.-(1) Katika Katiba hii, ila iwapo maelezo yahitaji
vinginevyo:
"amri ya Jeshi" maana yake ni sheria au amri
iliyotolewa kwa mujibu wa sheria, ya kusimamia nidhamu katika
jeshi;
"askari" likitumika kuhusiana na jeshi lolote, maana yake ni
pamoja na askari yeyote ambaye kwa mujibu wa amri ya
jeshi hilo ni mtu anayewajibika kinidhamu;
Ibara ya 147 maana ya Mwanajeshi.
147(3) Itakuwa ni marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na
chama chohote cha siasa, isipokuwa tu kama atakuwa na haki
ya kupiga kura iliyotajwa katika ibara ya 5 ya Katiba hii.
(4) Kwa madhumuni ya ibara hii, "mwanajeshi" maana yake
ni askari aliyeajiriwa kwa masharti ya muda au ya kudumu
katika Jeshi la Ulinzi, Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza au Jeshi
la Kujenga Taifa.
Twende kwenye majukumu
Sheria ya kanuni ya Adhabu
Kutoa tamko kwa
wafanya ghasia
kutawanyika
Sura ya 500 kif.
7; Sura 356 kif
11 (13) kifungu cha
77cha kanuni ya Adhabu kinasema Hakimu yeyote au, kama hayupo, afisa wa polisi wa au aliye juu ya
cheo cha mkaguzi(nyota moja na kuendele) au akida wa jeshi(Nyota moja na kuendelea/commissioned officer)la vita la Jamhuri ya Muungano,
atakayeona watu kumi na mbili au zaidi wamekusanyika kwa ajili ya
ghasia ana wasiwasi kuwa ghasia inataka kufanywa na watu kumi na mbili
au zaidi, au anaweza kutoa au kutolesha ilani kwa jina la Rais, kwa namna
atakayoona yafaa, kuwaamrisha wafanyaji ghasia hao au watu
waliokusanyika watawanyike kwa aman.
Mabano hayo nimeweka kwa ajili ya ufafanuzi tu kuonesha ulinganifu katika
Twendeni kwenye Uhalisia sasa
He unamkumbuka aliyekuwa kiongozi wa Operesheni tokomeza enzi za jk basi ni Simon Siro akiwa SACP wa Polisi aliongozi vikosi vya Jeshi la Polisi,Jeshi la Wananchi pamoja na Tanapa ndani ya vile vukokosi kulikuwa na majors wa kutosha na Makanali wote walpokea maelekezo kutoka kwake vipi apo mbona Hugo bado hakuwa kamishina kamili.Msichanganye mambo waungwana kamishina wa Polisi ni kamishina wa Polisi anaongoza commission Fulani kama vile fedha,utawala,mafunzo ,forensic na kadhalika sasa huku Jeshi la Wananchi commissioned Officer wanyota moja au mbili anaongoza commission gani? Mimi ninachojua anaongoza platoon tatu yaani company wakati kamishina msaidizi wa polisi anaongoza mkoa wenye watu askari pamoja na idara zote na ndiyo muongeaji hasa kwenye kamati ya Ulinzi na Usalama wa mkoa kama alivyolinda Heshima ya Jwtz pale Arusha kwa kuwajibu waandishi wa habari.Narudia tena kuwa kamishina ndani ya Polisi ni cheo cha mwisho kabisa maana kinachofuata ni hisani ya Rais sasa wewe na kanyota chako ukajifananishe na Mambosasa aliyepewa V8 na walinzi Nyumba Kali eneo sawa na Mawaziri na makatibu wakuu wakati wewe umeja wako unatembelea defender mbovu na unalala nyumba Dirisha kama LA choo tens chafu hasa. Acheni kulishwa ujinga askari na mnakaririshwa kasumba dharau mwishowe mnaanza kupigana. Ebu fikiri kwa kina unafikiri Mkuu wa wilaya ya Arumeru anaweza kumuamrisha Shana ? Maana Shana ni Dcp bado kuwa kamishina kamili .na mkuu wa wilaya ni kamishina? Fikiri kwa kina sana acha kudanganywa na macoplol sugu yanakuambia yalikwenda vitani Uganda wakati walioenda vitani wote wameshastafu maana aliyeingia na miaka 18 kastafu mwaka Jana.. Pia mkumbuke kila taaluma inaumuhimu katika jamii .
Nyongeza ya mawazo tu
Wote Nazi yetu kuu kutulinda sisi Wananchi na Mali zetu yanini mnaleta ligi na kufedheheshana kwa kujiona imara zaidi kiliko wengine.Nyie ni walinzi tu Nazi yenu kuu ni ulinzi .Amka kifikra askari acha ubabe wakishamba tafuta pesa uache kufungulia mageti wenzako.