Mara kadhaa nimekuwa nikiona askari wakigombana na kutunishiana misuri na mmoja kujiona bora zaidi kuliko mwenzake tena askari wa JWTZ wamekuwa Mara kwa Mara wakiwashambulia askari hasa wa Usala barabarani mbaya zaidi wao wapo Lori moja traffic mmoja haaaaaa.Kichekesho kwenye vyeo yule wa nyota moja Jwtz anajiona bora kuliko yule wa polisi nyota moja.Haaaaaa umbumbumbu in mzigo ssna.Sheria tu ndiyo inaweza kuwapima kulingana na vyeo vyenu si kingine .Je sheria inasema nini?
SURA YA TISA KATIBA YA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
MAJESHI YA ULINZI
Ibara ya
147.-(1) Ni marufuku kwa mtu yoyote au shirika lolote au
kikundi chochote cha watu, isipokuwa Serikali kuunda au
kuweka Tanzania jeshi la aina yoyote.
(2) Serikali ya Jamhuri ya Muungano yaweza, kwa mujibu
wa sheria, kuunda na kuweka Tanzania majeshi ya aina
mbalimbali kwa ajili ya ulinzi na usalama wa nchi na wananchi
wa Tanzania.
(3) Itakuwa ni marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na
chama chohote cha siasa, isipokuwa tu kama atakuwa na haki
ya kupiga kura iliyotajwa katika ibara ya 5 ya Katiba hii.
(4) Kwa madhumuni ya ibara hii, "mwanajeshi" maana yake
ni askari aliyeajiriwa kwa masharti ya muda au ya kudumu
katika Jeshi la Ulinzi, Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza au Jeshi
la Kujenga Taifa.
Madaraka ya
Amiri Jeshi Mkuu
Sheria ya 1984
Na.15 ib.49
148.-(1) Bila ya kuathiri masharti yatakayowekwa na sheria
yoyote iliyotungwa na Bunge, miongoni mwa madaraka ya Rais
akiwa kama Amiri Jeshi Mkuu ni kuyaamuru majeshi ya nchi
yatende mambo yanayohusika na vita vya ulinzi wa Jamhuri ya
Muungano, mambo ya kuokoa maisha na mali ya watu katika
hali ya hatari na mambo mengineyo ambayo Amiri Jeshi Mkuu
ataona yahitajika, na kwa ajili hiyo Amiri Jeshi Mkuu aweza
kuyaamuru hayo majeshi yatende mambo hayo ama ndani au
nje ya Tanzania.
(2) Bila ya kuathiri masharti yatakayowekwa na sheria
iliyotungwa na Bunge, madaraka juu ya mambo yafuatayo
yatakuwa mikononi mwa Amiri Jeshi Mkuu, yaani-
(a) madaraka ya kuwateua viongozi katika majeshi ya
ulinzi ya Jamhuri ya Muungano;
(b) madaraka ya kuwateua watu watakaojiunga na
majeshi ya ulinzi na madaraka ya kuwaondoa jeshini
wanajeshi;
(c) madaraka ya kuwateua wanajeshi watakaoongoza
Kuna mambo mengine ya kiutendaji yanawalinganisha katika sheria mfano kwenye kutuliza Fujo na kutawanya maandamano sheria inasema hivi
PENAL CODE (CAP. 16)
77. Any magistrate or, in his absence, any
police officer of or above the rank of
inspector» or any commissioned officer in
the military forces of the United Republic,
in whose view twelve ormore persons are
riotously assembled, or who apprehends
that a riot is about to be committed by
twelve or more persons assembled within his
view, may make or cause to be made a
proclamationin the president's name, in
such form as he thinks fit, commanding the
rioters or persons so assembled to disperse
peaceably.
Making
rioters todisperse
.pia askari safi kutoka jeshi LA wananchi kuwa mkuu wa wilaya no kamishina lakini hawezi kumuamrisha kamishina msaidizi wa polisi anayeongoza mkoa. Hivyo kulinganisha neno kamisha kwa maana ya nyota moja jw saw a na RPC no utoto uliopitiliza sana Saimon Siro aliongoza vikosi vya operesheni tokomeza akiwa kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi kukiwa na mameja wengi wa jwtz wakipokea maelekezo.waza kifaida nyie askari.