Huna hoja!Nimewaambia wote wenye vichwa vigumu,Kuanzia nyota tatu ndio kamisheni inaanza kwa polisi.Na Nimewaambia wakuu wa polisi wa wilaya (OCD) wanaanza na nyota 3 (ASP),SP hadi SSP,inategemea na idadi ya maafisa na vyeo vyao waliopo mkoani.Na sio ACP.
Sasa kama OCD ana majukumu ya kusimamia usalama wa wilaya na ni mjumbe wa kamati ya ulinzi na usalama.
Ina maana hata Rais anapokuwepo kwenye wilaya yake ana wajibu wa kumlinda.Hata kwenye msafara wa Rais, gari ya OCD inatangulia mbele,ya Rais inafuata nyuma yake.
Sasa OCD mwenye nyota 3(ASP),au SP unasemaje hana kamisheni?Na kamisheni ni mamlaka ya Rais ofisa anakasimishwa na anakula kiapo cha utii mbele ya Rais.Kwamba atamtii Rais na atailinda na kuitetea Katiba ya taifa.
Hoja yangu ni uwelewe maana ya kamisheni na majukumu ya ofisa mwenye kamisheni.Kwa hiyo kama askari anasimamia usalama wa wilaya ujue ana kamisheni na anatekeleza jukumu lake la usalama Kwa niaba ya Rais.