Gagurito
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 5,600
- 811
CDM ndio mwiba wao mkuu! Sita mbayuwayu!Mi nashangaa ameishambulia CHADEMA wakati hoja ilitolewa na Kafulila wa NCCR Mageuzi.
CDM ndio mwiba wao mkuu! Sita mbayuwayu!Mi nashangaa ameishambulia CHADEMA wakati hoja ilitolewa na Kafulila wa NCCR Mageuzi.
Mimi nataka akamatwe na arudishe hela ya uma na afilisiwe. Na JK naye ajivue gamba
Ubunge sio nyadhifa, ubunge ni uwakilishi na wanaomchagua ni wananchi. Tazama Shibuda alipotemwa CCM akaukwaa Ubunge kupitia cdm. Au umesahau, nikukumbushe na Slaa? Alipopigwa chini akaukwaa ubunge kupitia wapi? Kuweni makini kidooogo. Kwa kiwango alichofika Rostam anaweza kuwatumikia wananchi bila ya kuwa Mbunge. Hilo likumbuke.
Itashangaza sana Kama katibu Mwenezi wa CCM atajitapa kwamba hayo ni mafanikio.........Sidhani kama atakuwa desparate kiasi hicho katika kurejesha imani ya wananchi kwa chama chake,Naamini hatafanya hivyo
Kashfa ingine kwa CCM ya akina Nape. Kumbe walichakachua maamuzi ya kikao chao, na kumbe ni vita ya makundi ya kuchaguana na kuchafuliana kisiasa. Hii ni tuhuma nzito na ni ufisadi mwingine hatari zaidi. Itabidi waweke minutes za kikao wazi. Viinginevyo, watatumia the next three years kukanusha kashfa mpya ambayo ni nzito zaidi kuliko hiyo iliyomfanya ajiuzulu.
https://www.jamiiforums.com/
Florian Kezilahabi So u guys r on ur knees pleading with the rest to follow suit. LOL! 6 minutes ago · LikeUnlike
Fatma Aman BADO KIKWETE 2 minutes ago · LikeUnlikengoja tumsubiri yule kikwete kama atatia neno kuhusiana na kujiuzulu kwa ra, mtu ambaye alimuweka kikwete na serikali yake yote mifukoni mwake.
Mara tu baada ya kumalizika kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ambacho kilichagua wajumbe wapya wa Kamati Kuu na kuidhinisha uundwaji wa Sekretarieti mpya, dhana ya kujivua gamba ambayo naamini Mwenyekiti wetu aliianzisha kwa nia njema ilianza kuenezwa ikichukua tafsiri na mwelekeo tofauti na ule wa awali.
Wajumbe wawili wa Sekretarieti, Naibu Katibu Mkuu (Tanzania Bara), Mhe. John Chiligati, na Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi, Mhe. Nape Nnauye, walisikika wakitangaza kwamba Halmashauri Kuu ya Taifa ilikuwa imefikia uamuzi wa kuwapa siku tisini wale walioitwa watuhumiwa wanaokabiliwa na tuhuma za ufisadi ndani ya chama kujitoa katika nafasi zao za uongozi vinginevyo watafukuzwa na chama.
Wazee wangu, baada ya kushinikizwa sana na vyombo vya habari wawataje kwa majina wanasiasa waliokuwa wakituhumiwa kwa ufisadi ambao ni wajumbe wa NEC na ambao wanapaswa kujiuzulu nyadhifa zao, wajumbe hao wa Sekretarieti walikwenda mbele zaidi.
Baada ya awali kuwaeleza waandishi wa habari kwamba majina ya watuhumiwa hao yalikuwa yakifahamika kutokana na kuhusishwa katika kashfa tofauti kama zile za Richmond, EPA na ununuzi wa rada, mwishoni viongozi hao walikaririwa wakiyataja majina ya wanasiasa watatu kuwa ndiyo ambao walikuwa wakilengwa na maamuzi hayo.
Wazee wangu, nilishangazwa na kushitushwa na namna porojo na fitina za kisiasa zilivyofinyangwa kwa mara nyingine tena baada ya kusikia jina la mbunge wenu ambaye ni mimi, likitajwa kuwa miongoni mwa yale matatu ya viongozi waliokuwa wakitakiwa eti kupima wenyewe na kisha kuchukua uamuzi wa kujiuzulu nafasi zao za uongozi ndani ya NEC katika kipindi cha siku tisini.
[QUOTE]Napenda kuliweka hili sawa sawa. Uamuzi wangu wa kuachia nafasi zangu zote za uongozi nilizopata kwa tiketi ya CCM haukutokana na wala haumaanishi kukubaliana na shinikizo lililopotoshwa kuhusu azma ya utekelezaji wa dhana ya kujivua gamba, la hasha, bali dhamira ya dhati ya kuachana na siasa hizi uchwara (gutter politics) na kutumia muda wangu kushughulika na biashara zangu.Katika ulimwengu wa kibiashara wa leo, vita hivi ambavyo vinaweza kuonekana kuwa ni vidogo tu vyenye malengo ya kuchafuana kisiasa, vinakuwa na athari kubwa katika uhusiano wa kibiashara kuliko hata wale wasioelewa wanavyoweza kukadiria. Ndiyo maana nimeona ni afadhali sasa niwape nafasi wale wanaoendesha siasa hizi uchwara na zisizo na tija waendelee na siasa zao hizo ambazo kwa bahati mbaya kwao, mimi sina muda nazo na siwezi kuwa sehemu yake. Na mimi kwa upande wangu niendelee na maisha yangu.
Msukumo huo si mwingine bali ni ule wa kuamua kuachia nafasi zangu zote za uongozi ndani ya chama, nikianzia na ile ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa nikiuwakilisha Mkoa wa Tabora na hii ya ubunge wa Igunga ambazo kama si kwa baraka za chama changu nisingelikuwa nazo.
Duuh jamaa biashara zilianza muendea mrama.. nilisafiri nae wiki chache zilizopita na aliyekua akizungumza nae kikubwa alichokua akilalamikia ni hili la biashara kutokwenda vyema maana kila mmoja anaogopa kushirikiana nae kwa hizi kashfa zilizomuandama. It is a strategic kuhakikisha anaendesha maisha yake binafsi bila bughudha za magazeti.
Sir Leem,
Natanguliza pole maana utalazimika kuja ku-EDIT.