Rostam Aziz aachia ngazi CCM

Rostam Aziz aachia ngazi CCM

amejiuzulu ubunge na ujumbe wa NEC mkoa wa Tabora...imesharushwa live ITV SASA HIVI..! ni hatua nzuri..ninampa hongera kwa uamuzi mgumu..
 
Hivi Ben, umeandika nini hapa, ni wazi ulikuwa na mgongano wa mawazo kwenye kichwa chako. Ulianza kwa akili yako na umakini ambao unao siku zote. Haahaahaa baadaye ukakumbuka kuwa unatakiwa uendeleze kile alichotuonya RA kwenye hotuba yake, "yaani siasa za kuchafuana" maana huo ndiyo mtaji wa chama chako. Hii ni mbaya sana ni afadhali ungenyamaza tu kuliko kujiweka katika kundi la wafuata upepo. Nimekerwa sana na hii post nadhani hii ni miongoni mwa comment mbovu kuwahi kutokea kwa mtu kama wewe "Mwanasiasa kijana".

Eeeeeh...wala hii haistahili kukufurahisha hata kidogo.Kwanza nimemchafua nani,unaweza kuchafua watu ambao ni wachafu zaidi? Naendelea kusizitiza bado hizi ni sarakasi tu,duara la Ufisadi na impunity linaanza tena na linaendelea/CCM na serikali yake wamfikishe mahakamani na kutaifisha mali zake .Na wala hata mkifanya hivyo hatutawapongeza kwa sababu mlipaswa kutekeleza wajibu.So mpaka sasa hivi Rosatam,CCM na serikali ya CCM haijafanya kitu.Yaani mtu aibe halafu atanue na hela mtaani kwa sabubu ya kujivua nyadhifa tu?haya ndiyo mapambano dhidi ya ufisadi? Tanzanians deserve better than this.otherwise,thanks for your comment Sir/Madame
 
Kama ni kweli itabidi sasa apelekwe mahakamani au wataendelea kumkumbatia
kafulila jana kasema na mimi sitaki kurudia rudia, ila hii ndiyo tafasiri yake. hakuna wa kumfungulia mtu mashitaka ili haki itendeke.

Serikali regerege huwapigia magoti mafisadi -- by J.K. Nyerere.
 
Duh! Hii ni mbaya kwa siasa za nchi yetu...japo 2nashabkia tu watanzania...
Hv nan acyejua siasa mchezö mchafuu..?
 
Kwa taarifa zilizo rasmi nilizozipata ivi punde ni kwamba mbunge wa igunga ROSTAM AZIZ amejivua nafasi zote za uwongozi alionao ndani ya chama ikiwamo ile ya au jumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi.....akisisitiza pia uwamuzi wa yeye kujitoa katika nafasi iyo hautokani na shinikizo toka kwa chama kwa sera ya kujivua gamba bali ni uwamuzi wake binafsi wakuachana na siasa uchwara na kutilia mkazo biashara zake....

Angejiuzulu na ubunge ingependeza sana lakini mi naona bado ni kiini macho tu
 
JK alimfananisha RA na mchezaji muhimu kwenye timu kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu huko Igunga.Hii ni Embarrasement(fedheha) miezi 9 baada ya kampeni za uchaguzi

Kuna jamaa yangu nimeongea nae kafurahi kweli,akidai
chama "kitaonekana kisafi sasa"!

Watu hawa hawakujua kwamba huo ndo mwiba mkubwa sana kwao,..
1.najua hawawezi kumshitaki na afungwe,....(wapinzani watatumia hilo kuwashitaki ccm kwa wananchi)
2.siku zote wapinzani waliambiwa ni wapiga domo tu ,....(hapa wapinzani ndio walio fanya ccm wajivue gamba) so imani
wa wapinzani itaongezeka zaidi ya itakavo ongezeka kwa ccm.
 
amejiuzulu ubunge na ujumbe wa NEC mkoa wa Tabora...imesharushwa live ITV SASA HIVI..! ni hatua nzuri..ninampa hongera kwa uamuzi mgumu..

Hastahili hongera yoyote huyu fisadi ambaye ameliingizia Taifa letu hasara kubwa sana kwa kuhusika na EPA, Meremeta, Kagoda na Richmond/Dowans anastahili kupandishwa kizimbani na kufilisiwa utajiri wake alioupata kiharamu kwa kuwafisadi Watanzania.

 
Hata hivyo symbion itamlipa vizuri tu kesha sema yeye ni bizinesman
 
habari nilizo zipata ni kwamba rostam azizi ajivua gamba rasmi kajivua ubunge na kajitoa nec, source, radio one breaking news


Mimi nadhani ajivue pia na uraia wa nchi hii. Ahame tanzania atuachie nchi yetu. Ametuibia vya kutosha na kujifnya mfanyabiashara kumbe mwizi. Ahame nchi hii
 
hivi hawa jamaa kweli kama waliiba pesa kwanini hawakufunguliwa mashtaka kufungwa na hadi kufilisiwa kujiuzulu ili ale chenji ilobakia sio....this is what i call 100% BULLSHIT...
zaidi naweza sema gud move for Rostam serikali haikuwezi....SIMPLE
 
hivi jamani mmesoma habari yenyewe???
mbona kasema amejiuzulu hata ubunge???
kumbe ndo maana watu wanasaini mikataba bila hata kuisoma.

Hahaha inachekesha, kwa nini hawajasoma habari yote?

Tatizo wengine husoma title bila kupitia body text yote, matokea wanauliza hapa maswali ambayo yamejibiwa kwenye ujumbe. Someni habari yote unapochangia unakuwa na dondoo za uhakika si kutuuliza wengine mambo ambayo yana majibu kwenye ujumbe wa habari
 
It's about f#@*%ng time! Sasa Rais Jakaya Kikwete afanye "maamuzi magumu" na kumpeleka fisadi huyu namba 1 Tanzania mahakamani! Mpaka akimbie nchi kama Shailesh Vithlani wa rada
 
Nilisema,kama MP akidanchi au anyhow chance ikitokea natangaza nia,...

Nitagombea Igunga kupitia chadema,
 
Mimi nataka akamatwe na arudishe hela ya uma na afilisiwe. Na JK naye ajivue gamba
 
Back
Top Bottom