Defacto......quits strategically.it's just a retreat,long battle ahead.Kwanza CCM wanamgwaya,na yeye kwa jeuri amesubiria hadi siku 90 zimeisha na hawajathubutu kumfanya kitu mpaka ameamua mwenyewe katika mazingira yanayotia shaka.CCM hawana cha kujisifu wala kushangilia hapa ni bora wakae Kimya kabisa na hasa katibu mwenezi wao Nape Nnauye
Sasa kama amehusishwa na tuhuma za ufisadi,chama na serikali yake inazo nyaraka na ushahidi wa kutosha.Kitendo cha kuitikia wito wa chama chake uliosukumwa na ushahidi mzito wa kumtaka kujivua nyadhifa zake zote na yeye akachukua hatua hiyo basi CCM na serikali yake waende mbele zaidi kuonyesha dhamira yake ya dhati ya kupambana na ufisadi kwa kumfungulia mashtaka.Vinginevyo culture hii ya impunity iataendelea kuwapa hell.
Rostam ametekeleza wajibu wake,sasa CCM na serikali yake itekeleze wajibu wake kuhakikisha haki inatendeka kwa watanzania na hela za walipa kodi zinarudishwa.
Pia,nimtahadharishe Bashe,asije akawa na wazo la kugombea Igunga akitazamia kupata sapoti kutoka kwa Rostam Aziz,atakuwa amejizika kisiasa.Ana haki ya kugombea kikatiba though lakini angalie dhamira yake.
Na sisi CHADEMA kama habari hii ni yakweli,basi ni muda wetu sasa tujipange kikamilifu tuwapatie wanaigunga Mwakilishi maanake naamini jimbo hilo limekuwa wazi vipindi vinne mfululizo ambavyo RA amekuwa Mbunge!