Rostam Aziz aachia ngazi CCM

Rostam Aziz aachia ngazi CCM

kashatangaza kujiivua madaraka yote aliyokua nayo...kasema uamuzi wake hauhusiani na kujivua gamba....kasema anaenda kufanya biashara zake
 
clouds wamemaliza kutangaza na rostam mwenyewe ndio ameongea wamesema taarifa zaidi kwenye jahazi jioni
 
CCM - c wako nyuma sana, hii new sisi wana JF tumeipata masaa matatu yameshapita duh.
 
Kuna wapuuzi wanashangilia huyu jamaa kujiuzulu..mmesoma na kuelewa? hajajiuzulu kwa sababu yeye ni gamba...amesema amejiuzulu ili kuachana na siasa uchwara,na si kweli kwamba yanayosemwa juu yake yana ukweli...na nilipost awali huyu anaweza kujiuzulu kwa agreement na JK lakini sio Chenge na Lowassa na nyie mnaoshangilia kujiuzulu kwake hamjui nini kinafuatia mbele poleni...
 
Tabora hakuna vijana mbona RA kila aya anataja wazee wake tu!
 
Kwa taarifa zilizo rasmi nilizozipata ivi punde ni kwamba mbunge wa igunga ROSTAM AZIZ amejivua nafasi zote za uwongozi alionao ndani ya chama ikiwamo ile ya au jumbe wa kamati kuu ya chama cha mapinduzi.....akisisitiza pia uwamuzi wa yeye kujitoa katika nafasi iyo hautokani na shinikizo toka kwa chama kwa sera ya kujivua gamba bali ni uwamuzi wake binafsi wakuachana na siasa uchwara na kutilia mkazo biashara zake....
 
There are currently 1091 users browsing this thread. (235 members and 856 guests)
 
Anawatupia lawama akina nape huku akijiosha kwa mkuu wa kaya....
kama kawaida mkuu wa kaya anaendelea kuwaharibia wenzake huku yeye akionekana malaika...
nadhani huu ndo unaitwa unafiki kama sikosei...

ni kama kipindi EL anajiuzulu,utadhani yeye mkuu hahusiki kabisa na kwamba labda kashinikizwa kumbe ukienda deep deep down utakuta yeye ndo source ya hayo yote...
duu,kama hizi ndo siasa basi noma..
ila katika yote bora ameondoka na upinzani changemkieni jimbo hilo fasta fasta....
 
Wasikilizaji wamesikika wakiimba "HATUTAKI", huku wakitaja majina Nape,Sita. ., hivyo kumfanya rostam kurudia rudia na kusisitiza kauli yake ya kuachia ngazi zote.
 
yaani natamani siku moja kikwete nae atangaze kwamba nchi imemshinda aachie ngazi kwa hiari tu nahisi nitatoa machozi
 
Zamu ya Lowasa na Chenge sasa....
Kwa Lowassa itachukua muda kwani taarifa za ndani zinasema alimgomea Msekwa na kueleza kuwa yeye hayuko tayari kujiuzulu kwa tuhuma hizo. na kikao baina yake na Msekwa kilimalizika bila adhimio. Kwa Rostam walikubaliana na alikubali kufanya hivyo na leo ametimiza. Chenge yeye sijajua itakuwaje, lakini nadhani anaangalia upepo na kushinikizwa na Lowassa kama Lowassa atagoma basi hata yeye atagoma. haya yetu macho ngoja tuone magamba yanavyotoka, na yakitoka yote tutaka na yale ya Kichwa kutoka (Kikwete).
 
Back
Top Bottom