Rostam Aziz aachia ngazi CCM

Rostam Aziz aachia ngazi CCM

Siamini kama kweli unajiudhulu kwa kuwa umechoswa na maneno au bughuza bali masilahi wamekuwa madogo. jk walambishe tam tam
 
Hii nchi ya ajabu sana.........kwamba rostam ni mchafu mbele ya ccm lkn ni msafi sana ndani ya bunge na machoni pa watz.........inatakiwa akijivua gamba akamatwe fasta afunguliwe mashtaka na kesi yake iendeshwe haraka sana na kisha afungwe alafu mali zake zote zitaifishwe...."najua ni ndoto za mchana kwani tangu lini kikwete akakubali mapendekezo km haya"

Nakuunga mkono Mkuu huyu anastahili kabisa kukamatwa na pia kujiuzulu Ubunge haraka sana. Wale akina Mkapa, Chenge, Yona nao wanatakiwa wafunguliwe mashtaka haraka sana kwa madudu waliyofanya katika mikataba mbali mbali na pia Mkulo, Ngeleja, na Waziri mdogo wa Nishati inabidi waachie ngazi haraka sana kwa utendaji wao mbovu hapo Watanzania ndio tutaanza kuamini kwamba kweli CCM wameamua kulivua gamba, vinginevyo ni kuendeleza usanii tu
 

Vichwa vya JF hivi, hawa wote wamechangia hii habari pasipo kuisoma vizuri ingawa habari inaelezea vyema juu ya yeye kuachia Ubunge hawa bado wanauliza juu ya swali hilo hilo?!

inawezekana wewe ndo hujaelewa hapa....hii hotuba imeletwa mchana na uvumi/tetesi zilikuwepo toka asbh....hata hii thread imeeditiwa tu kutoka tetesi nakuwa news alert...wote walokuwa wanauliza ilikuwa kabla ya hotuba kubandikwa hapa.
 
mkuu nadhani haujasoma vizuri hiyo habari,umeperuzi....
maana amesema na ubunge anaachia...
 
A dark day in the history of tanzania,a behind the scenes de facto president of the countryhas called it quits,the question is will he continue pulling strings from behind the curtain,and will these new CCM enforcers,the nape"s survive his claws-only time will tell

Defacto......quits strategically.it's just a retreat,long battle ahead.Kwanza CCM wanamgwaya,na yeye kwa jeuri amesubiria hadi siku 90 zimeisha na hawajathubutu kumfanya kitu mpaka ameamua mwenyewe katika mazingira yanayotia shaka.CCM hawana cha kujisifu wala kushangilia hapa ni bora wakae Kimya kabisa na hasa katibu mwenezi wao Nape Nnauye

Sasa kama amehusishwa na tuhuma za ufisadi,chama na serikali yake inazo nyaraka na ushahidi wa kutosha.Kitendo cha kuitikia wito wa chama chake uliosukumwa na ushahidi mzito wa kumtaka kujivua nyadhifa zake zote na yeye akachukua hatua hiyo basi CCM na serikali yake waende mbele zaidi kuonyesha dhamira yake ya dhati ya kupambana na ufisadi kwa kumfungulia mashtaka.Vinginevyo culture hii ya impunity iataendelea kuwapa hell.

Rostam ametekeleza wajibu wake,sasa CCM na serikali yake itekeleze wajibu wake kuhakikisha haki inatendeka kwa watanzania na hela za walipa kodi zinarudishwa.

Pia,nimtahadharishe Bashe,asije akawa na wazo la kugombea Igunga akitazamia kupata sapoti kutoka kwa Rostam Aziz,atakuwa amejizika kisiasa.Ana haki ya kugombea kikatiba though lakini angalie dhamira yake.

Na sisi CHADEMA kama habari hii ni yakweli,basi ni muda wetu sasa tujipange kikamilifu tuwapatie wanaigunga Mwakilishi maanake naamini jimbo hilo limekuwa wazi vipindi vinne mfululizo ambavyo RA amekuwa Mbunge!
 

Vichwa vya JF hivi, hawa wote wamechangia hii habari pasipo kuisoma vizuri ingawa habari inaelezea vyema juu ya yeye kuachia Ubunge hawa bado wanauliza juu ya swali hilo hilo?!

Pole sana, Hujuhi kawaida ya JF,
Breaking News ilkitangulia kabla ya hiyo Barua kamili.
Hope utakuwa umeelewa sasa!
 
Sad enough..., habari hii haitamsaidia Mtanzania, CCM inajisafisha, Mali alizopora anabaki nazo, na ufisadi unaendelea kama kawaida.., Bila mtu kuwajibishwa wengine wataendelea na Business as Usual
 
Wakati mwafaka kwa CDM kujipanga na kuhakikisha wanalichukua jimbo hilo lililokosa mwenyewe. Hii ni aibu kwa mkuu wa nchi aliyekwenda pale na kumpigia campain akidai jamaa hana mfano kwa uchapakazi wake na hategemei serikali kutimiza wajibu wake kama mbunge hvyo anafaa kuendelea nalo jimbo tena na tena. Leo msela ameonesha sera ya uwajibikaji kwa vitendo anapoachia ngazi na hivyo kutoa mwanya wa uchunguzi huru na tuhuma zake tunaomba uchunguzi usiingiliwe na taasisi yoyote isiyohusika akiwemo rais wa nchi. Na kama anakutwa na hatia kwa makosa yake basi kinachofuata ni kufilisiwa mali zote alizonazo.
 
Hili nipigo kwa CCM, haya sasa NAPE mchochezi wa siasa za maji taka!! Umeona ulivyoshutumiwa??Sie yetu macho, ngoja tumpige kitanzi kabla hajakimbia!!
 
Nakuunga mkono Mkuu huyu anastahili kabisa kukamatwa na pia kujiuzulu Ubunge haraka sana. Wale akina Mkapa, Chenge, Yona nao wanatakiwa wafunguliwe mashtaka haraka sana kwa madudu waliyofanya katika mikataba mbali mbali na pia Mkulo, Ngeleja, na Waziri mdogo wa Nishati inabidi waachie ngazi haraka sana kwa utendaji wao mbovu hapo Watanzania ndio tutaanza kuamini kwamba kweli CCM wameamua kulivua gamba, vinginevyo ni kuendeleza usanii tu

hivi jamani mmesoma habari yenyewe???
mbona kasema amejiuzulu hata ubunge???
kumbe ndo maana watu wanasaini mikataba bila hata kuisoma.
 
bora nludi sasa nkagombee ubunge jimbo langu la igunga
 
22222222222222222222222222222222
Keep us updated, all eyes naelekeza TBR. Je anafanyia wapi hiyo press conference (namaanisha ukumbi gani hapo TBR? )

Hizo nyadhifa ni za ccm pekee au na Ubunge anautema?

Toa chanzo cha habari na mkutano utafanyikia wapi ili tuwe na uhakika isije ikawa ni kutaka kutupotezea muda. Na ikiwa kweli basi nategemea aachie pia ubunge

Hiyo bado haitamtakasa. Haachie na ubunge.

Hii nchi ya ajabu sana.........kwamba rostam ni mchafu mbele ya ccm lkn ni msafi sana ndani ya bunge na machoni pa watz.........inatakiwa akijivua gamba akamatwe fasta afunguliwe mashtaka na kesi yake iendeshwe haraka sana na kisha afungwe alafu mali zake zote zitaifishwe...."najua ni ndoto za mchana kwani tangu lini kikwete akakubali mapendekezo km haya"

Ubunge hawezi achia kwani kanuni za bunge na katiba bado vinaruhusu mafisadi kuwa waheshimiwa. Tena, hawana aibu kabisa hata mtu akipatwa na kashfa ya aibu lakini ubunge haachii.

Hivi ubunge sio wadhifa?
Damn!

Aahh kumbe tetesi! Ntarudi

matetesi matetesi:A S 103:

=Bigirita;2222229]Huna uhakika sasa unaleta ya nini?

Ingekuwa tetesi hisingekuwa na taarifa yake ya habari kwa wazee wa TBR! labda mseme uongo siyo tetesi
 
Nimeisoma hii hotuba yake, kimsingi kama wanaigunga wameilewa kama Rostam anavyotaka waielewe ntawashangaa sana wana Igunga
 
MWANZO WA KUNUKUU; "Kutokana na ukweli huo na sababu zote hizo basi, kwa moyo wa dhati na kwa nia thabiti, hatua ya kwanza niliyoiona kuwa ninapaswa kuichukua ilikuwa ni hii ya kuitikia wito unaotokana na msukumo wa ndani ya nafsi yangu wa kuamua kukomesha kabisa malumbano na mivutano isiyo na manufaa kwangu binafsi, kwa viongozi wa chama changu na chama chenyewe.

Msukumo huo si mwingine bali ni ule wa kuamua kuachia nafasi zangu zote za uongozi ndani ya chama, nikianzia na ile ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa nikiuwakilisha Mkoa wa Tabora na hii ya ubunge wa Igunga ambazo kama si kwa baraka za chama changu nisingelikuwa nazo" .
MWISHO WA KUNUKUU.
From RA
 
Back
Top Bottom