Rostam Aziz aachia ngazi CCM

Rostam Aziz aachia ngazi CCM

At what Price myfriend..., at what Price???!!!!!!!

Huku ndio kununua Baiskeli kwa bei ya Ferrari

Ameamua kuondoka baada ya kukamilisha ufisadi kubwa alioufanya na si ajabu ile pesa ya mitambo ya Richmond/Dowans ya $94million aliyodai anastahili kulipwa na TANESCO kishalipwa ndio maana kaamua kubwanga manyanga. Hebu tufuatilie hili tujue kama ile pesa ya ufisadi ambayo RA hakustahili kulipwa, imelipwa au la.
 
bado chenge naye aachie gamba.

hongera ccm lini mbowe atavua magwanda kwa kukataa kulipa pesa za maskini alizokopa.
Hivi una weza ukakopa na ukakataa kulipa.... je nchi hii haina sheria...Ngoja tuivue magamba Tanzania maana inamadeni mengi sana na yanazidi kuongezeka mwaka hadi mwaka hasa kipindi hiki cha fisadi Ki kwete...
 
Kama ni kweli itabidi sasa apelekwe mahakamani au wataendelea kumkumbatia
 
Kwa taarifa ambazo zipo ni kuwa RA ameamua kujiuzulu

Lakini hii haitoshi ni lazima tuhuma zake zote zishughulikiwe ikiwa ni pamoja na kupelekwa mahakamani na pia kuhakikisha fedha za kagoda zinarudishwa na kuwanufaisha watz.

Sio yeye tu wapo wengi ikiwemo viongozi waliopo serikalini waliokuwa wanashirikiana nae katika kufanikisha hili akiwemo Samuel Sitta ambaye wakati akiwa TIC alimpa deal nyingi sana huyu.

Nawasilisha.
 
Kauri ya utusiutusi iliyotolewa na Mh.6 ingetolewa na mbunge wa kawaida nisingeshangaa lakini huyu aliyeitoa ndiye aliyenisukuma kuuliza swali hili TUNAWEZA KUMPEKA KWENYE KAMATI YA MAADILI?
Kiongozi wa shughuli za serikali bungeni anaejibu bila kufikiri kama Sita anaweza kupelekwa kwenye kamati ya maadili? Sio kwamba jana amedhalilisha Bunge na chama chake tu bali pia Serikali nzima imeonekana hovyo na legelege. Na hapo ndipo ulegelege unapozidi. Najua ndani ya JF kuna waheshimiwa huingia na kusoma humu naombeni mwongozo wenu tunaweza kumpeleka huko?
 
Kama ni kweli itabidi sasa apelekwe mahakamani au wataendelea kumkumbatia
Kama CHENGE anakingiwa kifua na serikali kuwa hakuiba itakuwa huyu alie kwapua pesa zikamsaidia Ki kwete kuingia madarakani hapa tuna pumbazwa tuone wanatekeleza hasa baada ya kuona mambo magumu kila kona...
 
quote_icon.png
By Edson
vyanzo vyangu vyote vinasema hakuna kitu kama hicho.......

ila nianchojua ni kwamba jk anakutana na Rostam leo jion huko serengeti Bilila lodge kempinski ambako jk ameenda kwa ajili ya mapumziko.....

jk na lowasa walishamaliza kuongea mda mrefu + chenge

hakuna atakaye fukuzwa toka ccm

jana haikuwezekana maana mzee ndo alikuwa anafika.....wataonana leo bilila lodge kempinsk


006980-15-Exterior_View-twilight.jpg
Umejitahidi sana leo kutetea uongo,
ulikuwa huna haja ya kutuletea picha ya hotel kama ulikuwa huna uhakika.
 
CCM INAVYOKUFA-ASANTE MUNGU, UNASIKIA KILIO CHANGU amen
 
Naomba kujua amejiuzuru vitu gani? ni kwamba amejitoa uanachama na ubunge? au ndo tunadanganywa kua amejiuzulu vyeo ambavyo ni kama Mlezi wa Vijana tarafa ya Nkinga?
 
Yaani waTZ bwana! Nilikuwa nasikiliza Clouds; Breaking News ya kujivua gamba kwa Rost Tam Aziz, wakati akitangaza kuna watu wamesikika wakipiga kelele; hatukubali, hatukubali, hatukubali! Sasa sijui ni mtindio wa ubongo au wamepumbazwa na huyu Fisi Adi!
 
Yani miaka 16 kashikilia jimbo yeye tu?!Inabidi kuwe na sheria ya kuwalimit watu na madaraka.Maana kwa style hii hamna kitu kitakaa kibadilike...gamba linakua mpaka linakomaa ndo wanajifanya kulivua.

Ndesamburo ni mwaka wake wa ngapi huu kuwa mbunge??
 
Mbunge wa Igunga Rostam Azizi ametangaza kujivua gamba kwa kujiuzulu nafasi zake kwenye cham na Ubunge!

Source ITV
 
Back
Top Bottom