Riwaya ya Kijasusi: "Msako wa Mwehu"

Riwaya ya Kijasusi: "Msako wa Mwehu"

Itamaliza humu humu au ndiyo kutuonjesha kisha unapotea?
 
- 16 -

Riwaya: Msako
Mtunzi: Japhet Nyang’oro

Bi. Anita alitembea taratibu kuelekea ulipo mlango wa ofisi yake. Mawazo yake na akili ilikuwa ikitafakri maongezi yake na Rais. Ilikuwa wazi kuwa taaluma yake ilikuwa imeingia kwenye mtihani mkubwa sana ambao hajawahi kuupata tangu ameanza kazi hii. Mama huyu ambaye wengi walipenda kujua jina lake la pili lakini hakuna hata mmoja aliyefanikiwa. Vilevile hakukuwa na mtu aliyekuwa na uwezo wala kupata ujasiri wa kumwuliza mama huyu kuhusu jina lake la pili. Bi. Anita ni mtaalam wa juu katika masuala ya upelelezi na ujasusi. Sifa hizi ndizo zilizofanya mkuu wa nchi kutosita kumpa kazi ya kusuka na kusimamia kikosi cha siri kinachojihusisha na masuala ya ndani sana ya upelelezi na ujasusi. Kikosi hicho kinajulikana kwa jina la “Ofisi Fukuzi” Inasemekana kuwa mama huyu ni mwanamke pekee ambaye nchi ilimteua kuungana na kundi la wanaume kadhaa kwenda kuchukua mafunzo ya juu ya mambo hayo ya upelelezi na ujasusi enzi hizo, mara tu baada ya kupata uhuru miaka ile ya sitini. Ambapo nchi ilikuwa katika uhitaji mkubwa wa watu wa usalama ambao ni wazalendo na ambao hawakuwa wameathirika na fikra za kikoloni.

Safari yake kuchuma ujuzi huu ilimchukua miaka kadhaa. Katika miaka hiyo yote ilimlazimu kupita katika nchi nyingi zilizoendelea sana katika fani aliyokuwa akiihitaji. Ni katika miaka hiyo pia, ambapo ilimbidi kupitia katika mitihani mingi ya kazi za hatari na mateso makubwa. Mpaka aliporudi nchini, Bi. Anita alikuwa na sifa zote za kuitwa Komandoo.

Kwa miaka kadhaa tangu arejee nchini amekuwa akifanya kazi mbalimbali za kipelelezi na kijasusi, mpaka pale Serikali kwa sababu ambazo hazijulikani kwa hakika ilipoamua kuanzisha kitengo hiki cha Ofisi Fukuzi. Kitengo hiki ni maalum kwa masuala ya kijasusi ambayo si rahisi kutatuliwa na vyombo vingine vya usalama. Haikuwa kazi kumpata mtu wa kuweza kusimamia kazi hiyo ya siri sana. Jina la Bi. Anita lilijitokeza mara moja katika kumbukumbu za kichwa cha mkuu wa nchi wa wakati huo.

Kitengo hiki anachokiongoza kimesheheni vijana waliopikwa na kupikika katika masuala ya upelelezi. Nchi imekuwa ikitenga fungu maalum kama matumizi ya ofisi hii. Hali hii imesababisha, “Ofisi Fukuzi” kuwa na vifaa vya kisasa na vijana ambao wana mafunzo ya juu kabisa na kisasa toka nchi zilioendelea katika masuala ya ukachero.

Japo wataalam wa bajeti wamekuwa wakitaka kujua undani wa fungu linalotengwa kwa ajili ya Ofisi Fukuzi lakini walichoweza kujua na kuambulia ni, ‘ni kwa usalama wa nchi’. Wakanyamaza. Mawaziri wa Ulinzi walishajaribu mara kadhaa kujua undani wake lakini waliishia hewani. Ilikuwa ofisi ya siri yenye kufanya kazi moja kwa moja na Rais na kwa kiasi fulani Waziri Mkuu ambaye hata hivyo hakuwa na mamlaka ya moja kwa moja na ofisi hii. Ilikuwa ni nje ya mfumo wa kawaida wa madaraka na utawala.

Bi. Anita aliingia ofisini kwake kisha akaitisha kuonana na Jacob Matata. Jibu alilopewa ni kuwa Jacob Matata alikuwa hapo nusu saa iliyopita, amekwisha ondoka.
"Umeongea na Jacob alipokuja?" Bi. Anita alimuuliza Mkuu wa Ofisi, aitwaye mama Mbembela.
"Ndiyo, alivyofika tu aliuliza kama ulikuwepo ofisini nikamwambia hukuwepo. Basi akaenda ofisini kwake akajaza fomu ya dharula ya kuchukua silaha. Lakini pia, alikuja ofisini kwako, unajua kwa ngazi aliyopo anaweza kuingia ofisini kwako kwa dharula. Hakumaliza hata dakika tatu akawa ametoka. Akaondoka eneo hili, alionekana kuwa na haraka. Hilo halikuwa la ajabu kwangu, unajua Jacob Matata ni mtu mwenye majukumu mengi makubwa. Kwani kuna shida yoyote? Meneja wa Ofisi, Mama Mbembela alihoji baada ya kuona sura ya Bi. Anita iko katika hamaniko.
"Hakuna shida yoyote!’’ Bi. Anita alijibu huku akionyesha kuwa hakuwa na hamu kuendelea na maongezi, Mama Mbembela aliliona hilo, akasimama na kutoka mle chumbani, chumba cha ofisi ya Bi. Anita. Mama Mbembela alipoondoka, Bi. Anita aliingiza mkono kwenye uvungu wa meza moja kubwa iliyokuwa mbele yake.
"Shiiit!, Jacob anakusudia kufanya nini? What is going on?’’ Alisema baada ya kuwa amesoma kijikaratasi alichokikuta uvunguni mwa meza. Bi. Anita akiwa bosi wa Jacob Matata alikuwa anamjua vema Matata. Walikuwa wameshafanya kazi pamoja kwa muda mrefu na katika mazingira mbalimbali. Walikuwa na namna yao ya kufanya kazi, kuwasiliana, kuadhibiana na kutaniana ambayo hakuna mtu mwingine kwenye Ofisi Fukuzi alikuwa akijua japo wengi walijua fika kuwa Bi. Anita alikuwa akimpenda sana Jacob Matata. Hivyo baada ya kuwa ameambiwa mazingira ambayo Jacob Matata alikuwa ameondoka mara moja akahisi lazima Jacob atakuwa amemwachia ujumbe. Kweli alichokuwa akiangalia chini ya uvungu wa meza ilikuwa ni uwezekano wa kupata ujumbe wa Jacob Matata, hiyo ni moja ya sehemu ambazo hutumiwa na Jacob kumwachia ujumbe kukiwa na dharula. Ujumbe alioupata ulisomeka.
“Ruhusu mwindaji awe mwindwaji. I trust no one....” Ujumbe huu haukumshangaza Bi. Anita, kilichomshangaza na kujua kuwa wakati huu ofisi yake iko kwenye mtihani mzito ni zile nukta zilizofuata baada ya neno ‘one’. Jacob alikuwa ameweka nukta nne, yaani,(….) . Haikuwa bahati mbaya kwa Jacob Matata kuweka zile nukta nne , kwa mtu mwingine yeyote huo ungekuwa ujumbe wa kawaida ambao ulimaanisha kuwa Jacob Matata hamwamini mtu yeyote mpaka wakati huo. Katika utendaji wa Ofisi Fukuzi, mpelelezi wakati wote alikuwa na sehemu kuu nne muhimu, nazo ni Ofisi Fukuzi, Rais, Waziri Mkuu na Mpelelezi mwenyewe. Huo ndiyo uliitwa ‘mfungamano yakinifu’. Sasa Jacob Matata kuandika kuwa hamwamini mtu yeyote kisha akaweka nukta nne ilimaanisha kuwa hamwamini Rais, Waziri Mkuu, Ofisi Fukuzi na hata yeye mwenyewe! Hilo ndilo lililomshangaza Bi. Anita. Alielewa ilimaanisha nini mpelelezi anapokuambia kuwa, hajiamini hata yeye mwenyewe. Hi inamaanisha kuwa hana hakika kama anatumiwa au hatumiwi na adui. Ujumbe ulikuwa ni mmoja, mpelelezi alihitaji muda wa kuchanganua mambo. Tayari ilikuwa saa tano na dakika arobaini asubuhi.

* * *

Karatasi yenye ujumbe, “Ruhusu mwindaji awe mwindwaji. I trust no one....’’ iliweza kuoneka vema kwenye darubini ya Nyoso, aliyekuwa kwenye ghorofa iliyokuwa ikitazamana na majengo ya Ofisi Fukuzi. Alikuwa katika kutekeleza amri aliyopewa na Waziri Mkuu ambaye aliambiwa na Rais, "afuatilie, mienendo yote na mawasiliano ya Bi. Anita tangu sasa". Nyoso hakujua alikuwa akimfuatilia nani, wala maadili ya kazi yake hayakumtaka kujua ila alijua fika kuwa alitakiwa kumfuatilia mlengwa kwa ukaribu sana. Hivyo alipoona gari la Bi. Anita inaingia kwenye majengo hayo, yeye kwa haraka sana alitafuta namna ya kuingia kwenye jengo la ghorofa lililokuwa likipakana na jengo alilokuwa ameingia Bi. Anita. Kwa hila na mbinu za hapa na pale alifanikiwa kufika juu ghorofani na sasa alikuwa akichunguza kila kilichokuwa kikiendelea kwenye lile jengo. Darubini aliyokuwa nayo ilimwezesha kufanya hivyo. Mara moja alipiga picha ile karatasi, toka umbali ule na kwa kutumia ileile darubini. Kisha kwa kubonyeza vitufe vichache kwenye ile darubini, ile picha yenye ujumbe aliituma. Kisha akaisindikiza kwa ujumbe toka kwenye simu yake.

* * *

Haikuchukua Muda mrefu, dakika tano badaye yaani saa tano na dakika hamsini ujumbe uliingia kwenye simu ya Waziri Mkuu, Mhe. Silas Kiondo. Aliusoma, hakuelewa hadi pale ujumbe mfupi toka simu ya kiganjani ya Nyoso ulipoingia na kusomeka; “Mtu wako uliyesema nimfuatilie amekuta huo ujumbe kwenye meza yake.” Ndipo akaelewa haraka kuwa ujumbe huo ungekuwa umeandikwa na Jacob Matata kwenda kwa Bi. Anita. Mara moja akaufikisha ule ujumbe kwa Mhe. Jovin Sekendu, aliusoma kisha akaomba kuwa na nafasi ya peke yake. Kuna kitu alihisi kuwa alihitaji kuelewa. Katika mafunzo aliyopewa wakati ameingia madarakani, kulikuwa na kipengele cha usalama. Katika kipengele hicho alipata nafasi ya kufunzwa machache na Bi. Anita. Katika mada iitwayo ‘Kwa Wateule Wanne’, Bi Anita aliwahi kumweleza kwa kifupi juu ya zile nukta. Hivyo Mhe. Jovin Sekendu alipoziona kwenye ule ujumbe alitaka kujua zaidi.
"Naomba unikumbushe kidogo kuhusu nukta." Mhe. Jovin Sekendu, alisema mara baada ya kuwa kwenye simu na Bi. Anita.
"For your eyes only." Bi. Anita alisema.
"Okay, ila amri yangu inasimama palepale kama tulivyoongea asubuhi hii." Mhe. Jovin Sekendu alisema kwa mkazo.
"Nashauri Jacob Matata atafutwe kwa ajili ya nukta ya mwisho kama ulivyoona ujumbe!’’ Bi. Anita alisema.
"Sawa!’’ Mhe. Jovin Sekendu alisema kisha akakata simu. Mhe. Jovin Sekendu, alielewa lakini hakuelewa. Anakumbuka nukta zinasimama badala ya watu muhimu, lakini hakuelewa kama ujumbe umeandikwa na mtu kama Jacob Matata watu hao angekuwa nani na nani. Alichoelewa ni ‘for your eyes only.’ Hii ilimaanisha kuwa kuna kitu ambacho Bi. Anita hawezi kukisema toka kwenye ule ujumbe wa Jacob Matata, ila pia, inamaana na yeye Mhe. Jovin Sekendu, kama kuna kitu amekigundua asikiseme. Hivyo ‘for your eyes only’ ilikuwa ni lugha yao wawili ambayo Mhe. Jovin Sekendu aliielewa.
"Natoa agizo, Jacob Matata atafutwe kwa usalama wa nchi. Isitangazwe ila iwe kimyakimya. Namtaka akiwa hai." Mhe. Jovin Sekendu alimwambia Waziri Mkuu baada ya wawili hawa kuungana tena kwenye chumba kile cha awali.

* * *

Ngongoseke alitabasamu, kazi ilionekana kuwa nyepesi kuliko alivyokuwa ametazamia. Mamilioni ya dola yalikuwa yanaingia kwenye akaunti yake muda wowote, pale ambapo angeweza kutuma vithibitisho kuwa hakuna masalia ya ripoti ya gesi ya Mtwara na kuwa kile kisanduku cheusi cha ndege iliyoangushwa kuwa kimeshaharibiwa. Alikuwa karibu sana kuyatimiza hayo yote, lakini pia, alitaka kuhakikisha kuwa anakuwa karibu sana na Serikali kiasi kuwa kusiwe na hisia zozote kuwa ana mkono kwenye haya mambo. Kama kawaida sasa alikuwa kwenye jumba lake la kifahari, Bagamoyo.
Waliompa tenda hii ya kuvuruga mchakato wa gesi ya Mtwara, waliona ana kila sifa, hasa zile kuu mbili; ana sifa njema Serikalini na yuko jirani na viongozi halafu ya pili, anajua kuishi gizani bila taabu kana kwamba ndiko alikozaliwa, kukulia na ndiko atafia.

Hakuna anayekataa pesa, unaweza kunywa maji ukasema inatosha. Unaweza fanya chochote ukasema kinatosha, lakini kamwe huwezi sema pesa zinatosha. Hili linathibitika kwa Ngongoseke Amos Nkwija. Sasa alikuwa kwenye mipango yake tena. Na wakati huu alikuwa kwenye zile simu zake ambazo kila amalizapo kuongea huharibu kadi ya simu na hivyo kutumia mpya kila mara. Aliongea na Poka Kingu akaona mambo yako sehemu yake, alipoongea na Nyoso akahakikishiwa kuwa asiwe na wasiwasi. Frank Misanya yeye akasema ahesabu kila kitu kimeshakamilika. Akapiga simu nyingine mbili kwa vigogo. Halafu akapiga masafa marefu huko ughaibuni. Alipomaliza, alijuhusudu yeye mwenyewe; hakuna ambaye angeweza msifia kwa vile wachache waliokuwa wanajua alichokuwa anafanya. Na mbinu yake ni moja, kila aliyempa kazi alimpa kipande cha kazi, kazi kamili alikuwa akiijua yeye mwenyewe. Huyo ndiyo Ngongoseke Amos Nkwija.

Ungekuwa Jacob Matata au Bi. Anita ungefanya nini kwenye mazingira kama haya?
 
RIWAYA: MSAKO WA MWEHU
MTUNZI: Badi .M. Bao
MAWASILIANO. 0625920847, ( whatsap )
E- mail: badi.bao11@gmail.com
Dar es Salaam

SEHEMU YA TANO


️[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji737]
Jumamosi nyeusi iliyotanda huzuni
Kulipokucha kila kona ya nchi katika siku hiyo ya Jumamosi gumzo lilikuwa ni tukio la mlipuko wa jana yake kwenye jengo la Wizara ya Mambo ya Ndani. Magazeti yote yalitoa taarifa ya tukio hilo kwa ufasaha kabisa. Televisheni zote za ndani ya nchi zilisitisha vipindi vya burudani na michezo wakawa wanaripoti juu ya tukio hilo la kishenzi na kinyama mfululizo.
Mpaka kufikia saa sita mchana wa siku hiyo ya Jumamosi ilithibitika watu 50 walifariki dunia huku zaidi ya 100 wakilazwa hospitalini Muhimbili kama wahanga wa kisanga hiko cha kigaidi. Miongoni mwa waliofariki dunia walikuwa ni Mabalozi wote wawili wa Marekani na Canada, pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani. Pia Wabunge 10 nao walipoteza maisha yao, hivyo ilikuwa ni misiba iliyogusa Tanzania nzima. Kama hukufiwa na Mbunge wako, basi utakuwa umepoteza Mjomba, Shangazi, Rafiki, Baba, au Mama ili mradi kila mtu aliguswa kwa namna moja au ingine.
Amiri Jeshi Mkuu, Rais wa Nchi alizungumza mubashara na wananchi kupitia vyombo vya habari vya redio, televisheni na mitandao ya kijamii. Alitangaza maombolezo ya kitaifa ya wiki moja na bendera ya taifa itapepea nusu mlingoti. Pia aliwataka wananchi kuwa watulivu wakati vyombo vya usalama vinawasaka wahusika ili wafikishwe mahakama. Akawahakikishia kuwa serikali yao ipo makini kuhakikisha inavitumia vyombo vyake vya ulinzi na usalama na wananchi kukabiliana na tishio la makundi ya kigaidi dhidi ya Tanzania.
Ikapangwa Ijumaa ijayo kuwa ni ya mazishi ya kitaifa. Ambapo Wabunge waliofariki watapelekwa Dodoma Bungeni kuagwa kwa heshima zote kisha maiti zao zitapelekwa Majimboni kwao kwenda kuzikwa. Miili ya Mabalozi wa Marekani Na Canada ilisafirishwa kwenda nchini kwao kuzikwa. Pia serikali ya Marekani ikawataka raia wake wote waliopo Tanzania warejee nyumbani mara moja mpaka tishio la kigaidi dhidi yao litakapokoma. Wingu jeusi lilitanda katika nchi ya Tanzania kwa upande wa kidiplomasia. Ilishachafuka kimataifa sifa yake ya kuwa kisiwa cha amani na usalama, ikapotea na kuanza kuonekana kuwa sio sehemu salama tena bali ni kisiwa cha mauti na machafuko.
Vyombo vya usalama vilikuwa sasa vinaanza mkesha wa usiku na mchana kwa ajili ya kuwasaka wahusika wa tukio hilo la kigaidi.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji737]
SURA YA NNE
"Magaidi wajianika dhahiri shahiri"
Vyombo vya Dola vilichanganyikiwa havikufahamu lengo la magaidi kufanya shambulio hilo kwa nchi ya Tanzania. Mashushushu wakatawanywa kila mtaa wanahaha na kunusanusa kutafuta penyenye za watu waliokula njama za kulipua mabomu kwenye Jengo la Wizara ya Mambo ya Ndani, Ijumaa iliyopita.
Ilipofika siku ya Jumapili asubuhi fumbo la makusudio ya shambulio hilo likateguka, likawa hadharani kweupe. Vipeperushi viliokotwa vimesambazwa mitaani maeneo yote ya Jijini kuanzia Posta Mpya mpaka Kariakoo. Mbagala kuu mpaka Bunju, hakuna kichochoro, wala kinjia ambacho vipeperushi hivyo havikufika. Kipeperushi hicho kilisomeka kama ifuatavyo :
"TUNATAKA NCHI YA TANZANIA IKATE MAHUSIANO YA KIDIPLOMASIA NA MAADUI ZETU NCHI YA KENYA MARA MOJA. TUNATOA MUDA WA SIKU TATU TU BALOZI WA TANZANIA AWE AMERUDISHWA TANZANIA, MWISHO JUMATANO IJAYO, VINGINEVYO KISHINDO KINGINE KIKUBWA KINAKUJA MJIANDAE KUCHIMBA MAKABURI MENGI ZAIDI"
احب الحور العين
Ujumbe huo ulioishia na chata ya maandishi ya lugha ya kiarabu ulizusha kizaa upya na kupandikiza hofu mpya miongoni mwa wananchi. Hapo kila mtu akawa anajiuliza "hao walioandaa kipeperushi ni watu gani, mbona hawajajitaja!". Wale watu waoga wenzangu na mimi wakaanza wakakacha kwenda Mjini tena, na wengine wakarudi Mikoani kwao kabisa kupisha upepo mbaya upite.
Magaidi walishafanikisha walichokikusudia, nacho ni kupandikiza hofu na taharuki miongoni mwa wananchi na kudhoofisha uchumi wa nchi. Pia watalii wakaanza kuogopa kuitembelea Tanzania. Kwa watu wa usalama kwao haikuwa shida kutambua kuwa hivyo ni vitisho toka kundi la kigaidi la "Al-shabaab", walihitaji muda tu kuthibitisha dhana yao hiyo. Adui aliyetangaza vita ya hadharani na nchi ya Kenya ni kundi la kigaidi la "Al-shabaab". Kundi hilo lilikuwa linaendesha mapambano ya ulipizaji kisasi dhidi ya Jeshi la Kenya ambalo katika miaka michache iliyopita lilijiunga na "Vikosi vya Umoja wa Afrika" (AMISON) kwa lengo la kuwaondoa wapiganaji wa kundi hilo katika Miji mikubwa na midogo nchini Somalia. Hivyo vipeperushi hivyo sasa vilionyesha "Al-shabaab" wanakusudia kuifanya Kenya ni kisiwa, iwe nchi iliyotengwa na majirani zake wa Afrika Mashariki. Mipango ambayo walijua fika kama itafanikiwa itadhoofisha Umoja wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Hivyo kuzima ndoto za viongozi waasisi wa Afrika akina Kwame Nkurumah wa Ghana na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wa Tanzania. Ndoto yao ya kutamani uwepo wa Umoja wa Afrika wenye nguvu ya kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni na kila nyanja ya kimaendeleo. Magaidi tayari walileta kishindo cha mtego kilichowanasa wakazi wa Tanzania.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]

[emoji3586]Vibaraka wa Al-shabaab wakabidhiwa mikononi mwa Kachero Manu[emoji3586]

Ofisi za Usalama wa Taifa kitengo maalumu cha Ujasusi, zilikuwa zipo katika jengo la "Benjamin William Mkapa Pension Tower" roshani ya tano katika mtaa wa Azikwe. Zamani jengo hili lilikuwa linaitwa "Mafuta House". Zilikuwa ni ofisi za siri ambazo mtu wa kawaida huwezi kujua kazi wanazofanya watu hao. Ilikuwa ni Ofisi yenye Makachero bobezi wasiozidi watano, pamoja na Mkuu wao wa kazi mpya Bwana Omega Mtanika na Katibu Muhtasi wao dada Kokunawa.

Siku hiyo ya Jumatatu asubuhi Makachero wawili 'Manuel Yosepu maarufu kama "Kachero Manu" na Kachero wa kike Yasmine Abeid walikuwa wameitwa ofisini kwa Mudiru wao wa kazi Bwana Omega Mtanika ili wapewe jukumu jipya la kikazi.
Kachero Manu alikuwa ndio kwanza bado mpya mpya hajamaliza hata fungate lake la ndoa aliyoifunga hivi karibuni na mpenzi wake wa siku nyingi, tokea akiwa Chuo Kikuu, Bi Faith Magayane. Alipigiwa simu jana yake Jumapili saa sita mchana, akiwa yupo "Hotel Verde", Zanzibari na Katibu Muhtasi wa Mudiru wake kuwa anatakiwa arudi ofisini mara moja.

Mara baada ya vipeperushi vya magaidi wa "Al-shabaab" kusambazwa kwenye kila kona ya Jiji. Idara ya Usalama wa Taifa ikaona kuna haja ya Jeshi la Polisi kupigwa jeki na Kachero Manu, ambaye ametabahari katika fani ya Ukachero. Maji yalishazidi unga kwa Jeshi la Polisi, mapambano dhidi ya magaidi walio na uthubutu wa kufanya shambulio katika Makao Makuu ya Wizara ya Mambo ya Ndani yalikuwa ni mapambano kabambe. Ilikuwa ni patashika ya nguo kuchanika, mtoto hatumwi dukani, ngoma inogile mpaka kieleweke.

Kachero Manu kumuelewesha mkewe kuwa anavunja fungate kwa sababu ameitwa ghafla kazini, ilikuwa ni kazi nzito kueleweka. "Kama kazi yenyewe hiyo ambayo inakukosesha hata muda wa kutulia na mke wako katika kipindi muhimu kama hiki cha fungate bora uache kazi tu. Huu ndio muda adhimu tuliotakiwa kama wanandoa wapya kujenga mustakabali wetu mpya wa namna ya kuendesha maisha yetu" yalikuwa ni maneno makali yaliyoropokwa na mke wa Kachero Manu akiwa amefungwa na joto la hasira kooni mwake.

"Sasa mke wangu nikiacha kazi hii nitafanya kazi gani? " aliuliza Kachero Manu swali la mtego kwa sauti ya kubembeleza huku amemkazia macho mkewe. "Utajiajiri tu, utafute shamba Bagamoyo unalima mbogamboga na matunda na huku unafuga ng'ombe na kuku maisha yatajipa tu" aliweka msisitizo kwa sauti ambayo inaonyesha anamaanisha kile anachokizungumza hatanii japo chembe.

"Mke wangu, uhondo wa ngoma ingia uicheze, usizuzuke na ile michanganuo ya kilimo sijui cha matikiti au ufugaji wa kuku inayokufikia mezani kwako pale benki kwenye idara yako ya mikopo ukajua basi kilimo na ufugaji kinalipa sana.

Michanganuo mingi inakolezwa matokeo kuliko uhalisia ulivyo, mie imani yangu naamini kila Mtanzania mkubwa kwa mtoto ana Diploma ya Usanii hata kama hajasomea sanaa kule chuo cha TASUBA, Bagamoyo. Utaletewa mchanganuo wa kilimo cha matikiti uelezwe ekari moja itakuzalishia milioni sita, lakini ukienda kukifanya hicho kilimo au kuangalia hali halisi ya uchumi wa wakulima hao wa matikiti hauendani na michanganuo yao uliyoisoma. Kilimo na ufugaji Tanzania bado kuna changamoto kubwa ya masoko, bei duni, pembejeo feki, na zinginezo kibao. Labda serikali yetu siku za mbele ije na sera ya kulinda bei ya wakulima wa mbogamboga na matunda na bidhaa za mifugo kama mayai, maziwa na nyama. Vinginevyo bado haujanishawishi mke wangu kucheza pata potea na ya kuacha kibarua changu kinachonipa jeuri Jijini" alimalizia maelezo yake Kachero Manu bila kupindisha maneno kwa mkewe ili kumuweka sawa.

"Mhhh....haya bana ngoja tukomae na ajira za mkoloni za maofisini, ambazo zinatubana mpaka tunashindwa kufurahia maisha ya kifamilia, muda wote tunatenganishwa na majukumu ya kikazi tu" alijisemesha kwa manung'uniko mke wake huku akionekana ameshakubaliana na maelezo ya mumewe kwa shingo upande.

"Magaidi wamelipua Wizara ya Mambo ya Ndani na kusababisha vifo vya viongozi kadhaa, hivyo hamna mtu anaweza kuwafunza adabu magaidi kama mimi serikali ndio imeona hivyo, ngoja nikatoe jasho na damu yangu kwa ajili ya nchi yangu. Nchi ikichezewa na magaidi wakafanya wanavyotaka wao watakuja kutupangia mpaka muda wa kulala na kuamka" aliendelea kukizalendo kwa mkewe ili kumjenga kuwa ameolewa na mpambanaji katika medani za kivita, ambaye anaweza hata kuiacha familia yake miaka miwili mtawalia anaipigania nchi. Alitaka atambue kabisa kuwa hajaolewa na mwanamuziki ambaye anabembeleza mpenziwe kwa nyimbo, vilio na chakula cha nyuki, zawadi ya mauaridi.

Kachero Yasmine Abeid nae alijumuishwa kwenye jukumu hili kutokana na sababu mbili kubwa. Kwanza yeye ndio aliyefanikiwa kuzima mashambulio ya mabomu yenye viashiria vya ugaidi yaliyokuwa yanarindima Zanzibar kila kukicha katika miaka ile ya 2012-2013. Pia alikuwa ni fasaha sana katika bahari ya lugha za Kiarabu na Kisomali, hivyo huenda kuna nyaraka zinaweza kupatikana za siri yeye ndio atakuwa mtarujumani wa lugha kwa Kachero Manu. Alihamishiwa kikazi kuja bara kutokea Zanzibar yapata mwaka na nusu sasa.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji737]
 
Traitor wapo Ofisi pekuzi,ofisi ya rais na Jeshini
 
Ahsante sana lakini kama vile leo umetuma fupi sana kaka
 
- 17 -

Riwaya: MSAKO

Mtunzi: Japhet Nyang’oro

Frank Misanya yeye akasema ahesabu kila kitu kimeshakamilika. Akapiga simu nyingine mbili kwa vigogo. Halafu akapiga masafa marefu huko ughaibuni. Alipomaliza, alijuhusudu yeye mwenyewe; hakuna ambaye angeweza msifia kwa vile wachache waliokuwa wanajua alichokuwa anafanya. Na mbinu yake ni moja, kila aliyempa kazi alimpa kipande cha kazi, kazi kamili alikuwa akiijua yeye mwenyewe. Huyo ndiyo Ngongoseke Amos Nkwija.

*****Kitabu cha riwaya hii sasa kinachapwa kwa idadi ya wale walioweka ODA tu, kinatoka tarehe 15/6/2020. Weka ODA yako sasa 0762204166********

BAADA ya kutoka yalipo majengo ya Ofisi Fukuzi, mpelelezi Jacob Matata aliazimia kuanzia nyumbani kwa Afande Lucas. Kufutwafutwa kwa faili alilokuwa ameandaa kisha kuuawa ilikuwa dalili tosha kuwa kuna hatua alikuwa amepiga katika uchunguzi wake. Hivyo kwenda msibani na kuonana na mjane aliona kuwa lingekuwa wazo zuri. Afande Lucas alikuwa akiishi uraiani, Mwananyamala Komakoma jirani na Mwinjuma road.

Hakupata shida kuiona nyumba yenyewe, wamama wenye khanga tatu-tatu walionekana kufanya hili na lile. Upande wa kulia wa nyumba hiyo kulikuwa na turubai lililowekwa ili kuwapa watu kivuli. Aliangalia saa yake ya mkononi ilikuwa saa tano na dakika arobaini asubuhi. Kama utakumbuka wakati huu ndiyo Bi. Anita na yeye alikuwa ofisini kwake. Jacob Matata aliendesha taratibu kuliendea eneo lile. Hakukuwa na sehemu ya kuegesha gari hivyo alipitiliza kwa mwendo mdogo huku akijitahidi kutafuta sehemu ya kuegesha. Mbanano wa nyumba na ujenzi usio na mpangilio katika eneo hili ulifanya uzuri wa nyumba ambayo watu walikuwa wamejaa usionekane.

Aliiangalia ile nyumba ambayo aliamini kuwa ndiyo yalipo makazi ya marehemu Inspekta Lucas. Ilikuwa nyumba nzuri ya kisasa na thamani kubwa. Alishangaa kuona nyumba kama ile kujengwa eneo kama lile, maana nyumba kama hizo huonekana yale maeneo ya watu wazito. Kingine alichoshangaa ni kwa namna gani Askari Polisi alifanikiwa kujenga nyumba ya kifahari kama ile, ila alipokumbuka kuwa kwenye nchi yake mtu anaweza pata pesa kwa njia nyingi, alinyamaza. Kutafuta sehemu ya kuegesha kulimpeleka hadi mtaa wa nyuma ambapo kulikuwana kiwanja ambacho hakijajengwa. Hapo alikuta magari kadhaa yakiwa yameegeshwa. Kwa bahati nzuri aliona sehemu ambayo alipachika gari alilokuwa anatumia ambalo alikuwa amelikodisha. Hakuona busara kwenda nyumbani kwake baada ya yale yaliyokuwa yametokea usiku. Pia, isingekuwa akili nzuri kutumia gari lake analotumia siku zote. Hadhari lilikuwa jambo la msingi sana kwake wakati huu. Baada ya kuteremka na kufunga gari aliangaza kama anaweza pata kichochoro cha kumpeleka nyumbani kwa Afande Lucas, badala ya kuzunguka na barabara. Mara hii tena bahati ilikuwa upande wake, aliona kichochoro ambacho pia kilikuwa kikipitisha maji machafu. Haikuchukua muda alihisi yuko nyuma ya nyumba aliyokuwa akiiendea maana aliweza kusikia sauti za watu wakiongea katika hali ya kushirikiana kazi za upishi. Aliendelea mbele kidogo hadi alipokuwa usawa wa dirisha moja. Alipofika hapo alisita kidogo baada ya kusikia sauti ambayo haikustahili kusikika msibani. Alisimama kisha akajivuta ukutani jirani na lile dirishi ilikotokea ile sauti nzito ya amri.

“Kama akija mtu atakayejitambulisha kwa jina hilo tupe taarifa, maana mtu huyo ni hatari kwako na familia yako. Chukua simu hii, ukiminya tu hiki kidude utaongea na mimi moja kwa moja nami nitatuma askari wakusaidie. Pia, ukihitaji hela ziko kwenye akaunti yako ya benki.” Ilikuwa ni sehemu ya sauti hiyo nzito iliyoongea kwa amri. Jacob alitaka kuchungulia ili amwone aliyekuwa akiongea lakini kulikuwa na pazia zito hivyo hakufanikiwa. Aliharakisha kutembea ili awahi kuwaona watu hao kabla hawajatokomea. Akiwa na matumaini ya kufanikisha hilo mara uchochoro ule ukampeleka mbele ya dimbwi kubwa la maji machafu. Kwa mbele yake kulikuwa na choo ambacho kuta zake zilikuwa ni mabati na pembeni yake ambapo ndio kichochoro hiki kilipita lilichimbwa hilo shimo kubwa lililokuwa na maji machafu. Ilivyokuwa hakuwa na namna ya kuenedela na kichochoro hicho la sivyo ajitolee kutumbukia kwenye maji yale. Aliangalia kwa namna ya kukata tamaa, hii ilimaanisha asingeweza kuonana na yeyote aliyeongea kwa ile sauti. Alikata shauri kurudi na kuzunguka na barabara.

* * *

Wakati Jacob Matata akikwama kwenye kile kichochoro, Luteni Frank Misanya yeye alikuwa ndani ya gari lake akiendesha wakati simu ya Ngongoseke ilipoingia. Alipunguza mwendo wakati anakunja kushoto mbele ya Chuo cha Diplomasia akiiacha barabara ya Kilwa na kuingia Kurasini, mkono wa kushoto ulichukua simu hiyo iliyokuwa ikilia kwa fujo.
“Sema!’’ Alisema baada ya kuona namba asiyoifahamu “Ngongoseke hapa.” Alijitambulisha.
“Sema Mzee!’’ Luteni Misanya alisema.
“Nilikwambia wale vijana wamejua mengi kuhusu kazi zetu....” Ngongoseke alisema kabla hajakatizwa na Frank,
“Yaani umejuaje hapa ndio nakaribia nyumba wanayoishi, nataka nikawam...” Frank alisema lakini naye alikatishwa,“ Nilikwambia usiwaue wewe. Sasa sikiliza, sasa hivi wapeleke pale anapokaa Nanalungu, Jacob Matata, yuko hapo.” Ngongoseke alisema
“Aaaaah, aisee wewe Mzee ni kiboko!” Luteni Frank alisema, maana alishaelewa akili ya Ngongoseke.
“Ulikuwa hujui au unathibitisha tu?’’ Ngongoseke alisema kwa majivuni.
“Akili yako inafanya kazi kwa kiwango cha ajabu sana.” Frank alisema.
“Waende sasa hivi maana nimeambiwa Jacob yuko hapo muda huu. Yeye atatusaidia kuwaua.” Ngongoseke alisema.


* * *

Robo saa baada ya Ngongoseke kutoa maelekezo hayo kwa Luteni Frank Misanya, Jacob Matata yeye sasa alikuwa mbele ya mlango wa chumba alichoelekezwa kuwa mjane wa Afande Lucas alikuwemo. Kama alivyoiona kwa mbali, ilikuwa nyumba kubwa ambayo hukuhitaji elimu kubwa kuitaja kuwa ya kifahari japo ilikuwa maeneo yasiyoistahiki kuwepo. Alibisha na kukaribishwa. Aliangaza macho huku na huko. Kilikuwa chumba kilichojaa wanawake tu, ambao wengi wao macho yao yalikuwa mekundu na wengine yakiwa yamevimba. Mara alimwona msichana mmoja mrembo wa haja ambaye pembeni yake kulikuwa na kitu kama simu. Macho yake yakavutika na muundo wa ile simu, aliiangalia tena kwa makini na mara Jacob Matata akabaini kwa kilikuwa kinasa sauti. Akili ya Jacob Matata ilifanya kazi haraka, alijua yule mtu mwenye sauti ya amri ndiye aliyempatia huyo mwanamke kile kifaa akimdanganya kuwa ni simu ili aweze kurekodi mazungumzo yote ya yule Mjane wa Afande Lucas.

“Pole sana dadangu!” Jacob alisema baada ya kuwa ameinama alipokuwa ameketi yule dada. Alikuwa mwanamke, mzuri, mrembo wa umri wa kati, si mtoto si mtu mzima. Maana Jacob yeye anajua kuwa urembo na uzuri kwa manamke ni vitu viwili tofauti, lakini huyu alikuwa navyo vyote.

“Asante sana!” Alisema yule msichana kwa sauti kavu, huku akijitahidi kumwangalia Jacob Matata.

“Sijui unawe......” Kabla Jacob Matata hajamaliza alichotaka kusema, yule mwanamke haraka akaweka kidole katikati ya midomo yake kama ishara ya kumtaka Jacob Matata anyamaze. Kisha akasimama na kumwonyesha Jacob ishara kuwa amfuate.

“Bila shaka unaitwa Jacob Matata?’’ Msichana alihoji. “Kama ndiye?’’ Jacob alisema kwa mshangao.

“Ndiye wewe, maana hata jibu lako limekuwa sawa na nilivyoelekezwa na mume wangu. Naitwa Nana Lucas, marehemu mume wangu katika siku zake za mwisho alikuwa anakutafuta sana. Alijua maisha yake yako hatarini ila hakuona kama angeweza pata msaada toka kwa mtu yeyote yule mwingine zaidi yako. Juhudi zake za kukutafuta hazikuzaa matunda hadi alipouawa. Ila akawa amenielezea sifa zako akiwa na hakika kuwa kwa namna moja ama nyingine ungeingia kupeleleza kitu alichokuwa ameanza kupeleleza. Hivyo alikuwa na hakika kuwa ipo siku ungekuja kwangu. Hivyo nilivyokuona tu mara moja nikajua ndiye.” Alisema yule mwanamke huku sasa machozi yakiwa yanamtiririka. Jacob alimvuta na kuanza kumbembeleza.

“Je, unaweza kuniambia kama kuna lolote alitaka unifikishie?’’ Jacob alisema kwa sauti ya kubembeleza pia, huku akili yake ikiwa makini kabisa.

“Jumatatu wiki iliyopita ndiyo alikuja akiwa amebadilika sana. Nikamuuliza vipi, akaniambia kuna kazi amekuwa akifanya, anasema uchunguzi wake umemfikisha sehemu ambayo amegundua kuna watu wa usalama na viongozi wanahusika. Hilo halikumtisha sana, ila anasema alimtembelea Luten Frank Misanya, baada ya kuongea naye amemtishia maisha kama hatoachana na kazi hiyo. Hivyo akaniambia nikikuona nikuombe uanzie kwa Luten Frank Misanya.” Alisema yule msichana huku akilia kwa kwikwi.

“Je, kuna jingine Nana?’’ Jacob alihoji.

“Hapana Jacob, ila kuna watu walikuja wakijifanya wao ni Jacob Matata na kuniuliza kama kuna ujumbe wowote marehemu aliuacha kwa ajili yao. Lakini katika wote sikuona kama kuna mtu ana viashiria vya sifa ambazo mume wangu aliniambia. Hivyo sikusema lolote.’’

“Okay, bila shaka ndiyo waliyokupa hiyo simu ambayo pia ni kinasa sauti?’’ Jacob alihakiki.

“Ndiyo, nilipoiona niligundua. Wengi hudhani miye ni mwanamke wa kawaida tu, lakini si kweli. Ni mtu niliyepitia mafunzo mengi ya namna hiyo wafanyayo na mapenzi yangu kwa Lucas yaliyonifanya nijitulize kwake. Lakini hivi nilishapanga kama nisipokuona kesho nianze mikakati ya kisasi. Mazishi tumefanya jana, nilipanga kupumzika leo halafu kesho nianze mishe-mishe.” Nana alisema.

“Ulipanga ungeanzaje kulipa kisasi?’’ Jacob alihoji.

“Sina mpango kamili kwa sasa, ila kwa harakaharaka bila shaka ningeanza na waliokuja kunipa hii simu.” Nana alisema.

“Nadhani inaweza kuwa hatari kuliko unavyodhani.’’ Jacobo alisema kisha akamkumbatia yule Msichana ambaye sasa alianza kububujikwa na machozi.

“Nini kimekufanya uamini kuwa mimi ndiye Jacob Matata?’’ Swali hilo la Jacob lilimfanya yule msichana amsukume Jacob na kujitoa mikononi mwake. Akamwangalia kwa muda kana kwamba ndiyo kwanza anamwona. Kisha kwa sauti ya kutafakari akasema, “Wewe siyo kama askari wengine, askari ni wababe na wala siyo kama jambazi, una mvuto kwa mwanamke na ndiyo mume wangu alivyoniambia. Kitendo cha kupiga magoti pale wakati unanisalimia, muonekano wako na ulivyoitoa ile pole ilikuwa alama tosha kuwa wewe ndiye!’’ Alisema alafu akamkumbatia tena Jacob Matata huku, akilia kwa sauti na uchungu.
“Jacob, nisaidie kulipa kisasi kwa Mwenda wangu. Niko tayari kukusaidia kama ukitaka!’’ Alisema kwa uchungu, sauti yake kama iliingia kwenye masikio ya Jacob, haikuishia hapo tu bali iliingia kwenye nafsi na moyo wake. Matokeo yake akajikuta akisema,
“Tuombe uzima, Mungu atusaidie.”

"Kwa nini nisiwapigie halafu uje uwakamate Jacob?’’ Nana alihoji.

"Wazo zuri lakini sishauri ufanye hivyo. Watu hawa si wa kuwafanyia mzaha hata kidogo. Endelea kuwepo, ukiwa mtulivu na kufanikiwa kuwafanya wasijue kuwa umeonana na mimi hilo litatusaidia sana mbele ya safari tukiendelea kuwa hai. Lengo si kupata tawi bali mzizi wa mambo haya.’’ Jacob alisema huku macho yake yakiwa yametulia kifuani kwa Nanalungu. Alihusudu jinsi Afande Lucas alivyokuwa amefanikiwa kuchagua mwanamke mrembo.

Kama umesoma weka like na comment yako nijue tuko wote[emoji1488]
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom