mtzmweusi
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 8,700
- 9,070
- Thread starter
- #41
- 11 -
Imetungwa na kuandikwa na Japhet Nyang’oro Sudi
Saa tatu na nusu juu ya alama watu watatu walikuwa ndani ya chumba. Watu hao ni Bi. Anita, Jacob Matata na Waziri mkuu, Silas Kiondo.
Pwaaa! Faili lilitupiwa mezani.
Faili hilo lilikuwa na jina Msako.
“Mwandishi wa faili hili ni Inspekta Msaidizi wa Polisi Lucas Mwenda ambaye ameuwa jana asubuhi kisha faili lake likaharibiwa kama utakavyoliona. Lucas Mwenda alikuwa akiongoza timu upande wa Jeshi la polisi, iliyokuwa ikisaka mtu anayehusika na mauaji ya Sabodo Msumari. Lakini kwa vile mambo yamepandana ilibidi timu yake iguse kwa kiasi kikubwa kutoweka kwa Judith Muga na pia kuanguka kwa ile ndege iliyokuwa na wale wataalam wa mambo ya gesi toka makampuni ya Magharibi. Faili hili kama unavyoliona, limefutwafutwa na karatasi nyingine zimeloana au zimelowekwa kwenye kitu ambacho inaaminika kuwa ni maji ili lisiweze kusomeka. Maiti ya Inspekta Lucas Mwenda ilikutwa daraja la Sarenda. Faili hili lilikuwa Kituo cha Polisi cha Msimbazi. Inaonyesha kuwa askari huyu alikuwa amefanikiwa kupata fununu fulani kuhusiana na mambo haya, ndiyo maana kumuua tu haikutosha ila wameharibu na faili alilokuwa akilitumia. Kwa sababu hii, Mkuu wa Kituo cha Polisi na watu wote waliokuwa zamu katika muda unaodhaniwa faili hili liliharibiwa wamewekwa chini ya ulinzi mkali sana, kupisha na kusaidia uchunguzi. Kama ukitaka kuwahoji tutaarifu tu” Ndiyo alivyoanza kuongea mhe. Silas Kiondo. Waziri mkuu.
Akamwangalia Jacob, kuona kama nafuatilia alichokuwa akisema.
Halafu ikawa zamu ya Bi. Anita kutoa maelekezo.
“Kama tulivyokuambia hapo awali, hiki ni chumba chenye mafaili yenye siri nzito za nchi. Ni watu wachache sana hapa nchini wanaojua kilipo na matumizi ya chumba hiki ambacho huitwa SAFE HOUSE. Watu wanaojua chumba hiki kina nini na umuhimu wake, hawafiki wane. Hata walinzi wanaokuja kulinda hapa hawajui umuhimu wa chumba hiki. Lakini kutokana na umuhimu wa suala lililoko mbele yetu tumefikiria namna ya wewe kuweza kujua historia hii kwa kina na tumeona hatuna njia nyuingine zaidi ya kukuleta kwenye hiki chumba. Tutakufungia humu”
“Awali tulitaka kulitoa hili faili na kukuletea. Lakini kwa hali ilivyo sasa hakuna namna tunaweza kutoa hili faili ndani ya chumba hiki. Tulitaka kutoa nakala ya ziada ya faili hili na kukuletea, lakini bado tukaona si salama sana kwako na nchi pia. Hivyo bwana Jacob Matata, ndani ya chumba hiki kuna mafaili zaidi ya elfu tatu lakini tunataka usome mafaili kumi na saba. Mafaili haya kumi na saba yako kwenye kabati lile pale. Kutokana na taarifa tulizonazo, kabati hilo lina mafaili ambayo tunahisi yatakuwa yanahusiana kwa namna moja ama nyingine na tukio hili. Lakini pia, tumekuwekea kitabu kimoja cha riwaya kiitwacho Patashika, ambacho kiliandikwa na mwandishi Japhet Nyang'oro Sudi. Utashangaa kitabu cha riwaya kinaingia namna gani kwenye mkasa huu. Ila kitabu hicho kina kisa ambacho upelelezi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha yatokeayo sasa yana muunganiko toka kwenye matukio ya kitabu hicho.” Alisema Bi. Anita mkuu wa Kitengo cha ujasusi - Ofisi Fukuzi. Kitengo hicho kilichosheheni vijana hatari wenye mafunzo ya juu katika ujasusi, upelelezi na kupigana.
“Kukuwezesha wewe kukaa humu wiki nzima huku ukifanya uchambuzi huo tumeona tukuwekee kila kitu. Kama nilivyosema hakuna mtu ajuaye juu ya nyumba hii zaidi ya watu wanne katika serikali. sasa wewe utakuwa mtu wa tano. Tutakuja hapa baada ya wiki na tutajua namna ya kuanza upelelezi mzito wa kumsaka huyo anayefanya matukio haya ya kutisha yanayohatarisha usalama wa taifa letu. Kama utagundua lolote wakati wowote ambalo unadhani haitakuwa na haja ya wewe kuendelea kukaa humu basi utanitaarifu kwa mawasiliano haya. Utachukua hiki kifaa kisha utaminya namba 00001111 utanipata. Hii ni secure line” Bi. Anita alisema. Halafu akamkabidhi Jacob kifaa Fulani kidogo kama kiberiti, kikiwa na batani zenye namba. Jacob Matata alikipokea na kukitupia juu ya meza. Kukawa kimya kwa muda.
“Jacob, najua wiki moja kwako inaweza kukufanya usome na kutafakari vitu ambavyo askari hata wapelelezi wengine wa kawaida wangetumia miezi sita kuvisoma, kuvielewa na kupembua ukweli uliko ndani ya kule kuelewa. Chukulia suala hili kwa uzito mkubwa. Kama ulivyosema, imetosha kwa washenzi wa magahribi kutaka kutuchezea. Imetosha, hebu tuwazime na kuwashikisha adabu. Kuna mengine siwezi kukuambia moja kwa moja, ila jua kuwa Taifa linatikisika hivi sasa. Rais, Mhe. Jovin Sekendu anaishi kwa wasiwasi mkubwa. Inabidi tumtafute yeyote aliyeko nyuma ya mpango huu” Bi. Anita alisema kwa uchungu. Maneno ambayo yaliuchoma moyo wa Jacob Matata na kumfanya awe tayari kwa kazi.
Baada ya hapo, waziri mkuu na Bi. Anita walimuaga mpelelezi Jacob Matata, ambaye angebaki ndani ya nyumba ile kama walivyosema.
“Nitajitahidi kufanya linalowezekana, japo naona jambo lenyewe limejifungafunga sana na muda wake ni mchache. Tuombe heri.” Jacob alisema huku macho yake yakiwasindikiza wakuu hawa waliokuwa wakitoka. Wote wawili walitembea kutoka mle chumbani huku Jacob Matata akiwa amesimama, mkono wake wa kushoto ukiwa umeshikilia lile faili. Walitoka mlangoni na wa mwisho kutoka alikuwa Mhe. Silas Kiondo, ambaye kabla hajafunga mlango nyuma yake aligeuka akamwangalia Jacob Matata, macho yao yakakutana.
"Jacob.."Mhe. Silas Kiondo aliita. Jacob akanyanyua kope kabla ya kusema, "Mkuu".
"Fanya kazi yako kwa makini, taifa hili linategemea sana matokeo ya kazi yako. Binafsi nimefurahi kuonana na wewe nimekuwa nakusikia tu." Waziri alisema, hakusubiri jibu la Jacob Matata.
Itaendelea
Leo ntatupia episode 2
Imetungwa na kuandikwa na Japhet Nyang’oro Sudi
Saa tatu na nusu juu ya alama watu watatu walikuwa ndani ya chumba. Watu hao ni Bi. Anita, Jacob Matata na Waziri mkuu, Silas Kiondo.
Pwaaa! Faili lilitupiwa mezani.
Faili hilo lilikuwa na jina Msako.
“Mwandishi wa faili hili ni Inspekta Msaidizi wa Polisi Lucas Mwenda ambaye ameuwa jana asubuhi kisha faili lake likaharibiwa kama utakavyoliona. Lucas Mwenda alikuwa akiongoza timu upande wa Jeshi la polisi, iliyokuwa ikisaka mtu anayehusika na mauaji ya Sabodo Msumari. Lakini kwa vile mambo yamepandana ilibidi timu yake iguse kwa kiasi kikubwa kutoweka kwa Judith Muga na pia kuanguka kwa ile ndege iliyokuwa na wale wataalam wa mambo ya gesi toka makampuni ya Magharibi. Faili hili kama unavyoliona, limefutwafutwa na karatasi nyingine zimeloana au zimelowekwa kwenye kitu ambacho inaaminika kuwa ni maji ili lisiweze kusomeka. Maiti ya Inspekta Lucas Mwenda ilikutwa daraja la Sarenda. Faili hili lilikuwa Kituo cha Polisi cha Msimbazi. Inaonyesha kuwa askari huyu alikuwa amefanikiwa kupata fununu fulani kuhusiana na mambo haya, ndiyo maana kumuua tu haikutosha ila wameharibu na faili alilokuwa akilitumia. Kwa sababu hii, Mkuu wa Kituo cha Polisi na watu wote waliokuwa zamu katika muda unaodhaniwa faili hili liliharibiwa wamewekwa chini ya ulinzi mkali sana, kupisha na kusaidia uchunguzi. Kama ukitaka kuwahoji tutaarifu tu” Ndiyo alivyoanza kuongea mhe. Silas Kiondo. Waziri mkuu.
Akamwangalia Jacob, kuona kama nafuatilia alichokuwa akisema.
Halafu ikawa zamu ya Bi. Anita kutoa maelekezo.
“Kama tulivyokuambia hapo awali, hiki ni chumba chenye mafaili yenye siri nzito za nchi. Ni watu wachache sana hapa nchini wanaojua kilipo na matumizi ya chumba hiki ambacho huitwa SAFE HOUSE. Watu wanaojua chumba hiki kina nini na umuhimu wake, hawafiki wane. Hata walinzi wanaokuja kulinda hapa hawajui umuhimu wa chumba hiki. Lakini kutokana na umuhimu wa suala lililoko mbele yetu tumefikiria namna ya wewe kuweza kujua historia hii kwa kina na tumeona hatuna njia nyuingine zaidi ya kukuleta kwenye hiki chumba. Tutakufungia humu”
“Awali tulitaka kulitoa hili faili na kukuletea. Lakini kwa hali ilivyo sasa hakuna namna tunaweza kutoa hili faili ndani ya chumba hiki. Tulitaka kutoa nakala ya ziada ya faili hili na kukuletea, lakini bado tukaona si salama sana kwako na nchi pia. Hivyo bwana Jacob Matata, ndani ya chumba hiki kuna mafaili zaidi ya elfu tatu lakini tunataka usome mafaili kumi na saba. Mafaili haya kumi na saba yako kwenye kabati lile pale. Kutokana na taarifa tulizonazo, kabati hilo lina mafaili ambayo tunahisi yatakuwa yanahusiana kwa namna moja ama nyingine na tukio hili. Lakini pia, tumekuwekea kitabu kimoja cha riwaya kiitwacho Patashika, ambacho kiliandikwa na mwandishi Japhet Nyang'oro Sudi. Utashangaa kitabu cha riwaya kinaingia namna gani kwenye mkasa huu. Ila kitabu hicho kina kisa ambacho upelelezi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha yatokeayo sasa yana muunganiko toka kwenye matukio ya kitabu hicho.” Alisema Bi. Anita mkuu wa Kitengo cha ujasusi - Ofisi Fukuzi. Kitengo hicho kilichosheheni vijana hatari wenye mafunzo ya juu katika ujasusi, upelelezi na kupigana.
“Kukuwezesha wewe kukaa humu wiki nzima huku ukifanya uchambuzi huo tumeona tukuwekee kila kitu. Kama nilivyosema hakuna mtu ajuaye juu ya nyumba hii zaidi ya watu wanne katika serikali. sasa wewe utakuwa mtu wa tano. Tutakuja hapa baada ya wiki na tutajua namna ya kuanza upelelezi mzito wa kumsaka huyo anayefanya matukio haya ya kutisha yanayohatarisha usalama wa taifa letu. Kama utagundua lolote wakati wowote ambalo unadhani haitakuwa na haja ya wewe kuendelea kukaa humu basi utanitaarifu kwa mawasiliano haya. Utachukua hiki kifaa kisha utaminya namba 00001111 utanipata. Hii ni secure line” Bi. Anita alisema. Halafu akamkabidhi Jacob kifaa Fulani kidogo kama kiberiti, kikiwa na batani zenye namba. Jacob Matata alikipokea na kukitupia juu ya meza. Kukawa kimya kwa muda.
“Jacob, najua wiki moja kwako inaweza kukufanya usome na kutafakari vitu ambavyo askari hata wapelelezi wengine wa kawaida wangetumia miezi sita kuvisoma, kuvielewa na kupembua ukweli uliko ndani ya kule kuelewa. Chukulia suala hili kwa uzito mkubwa. Kama ulivyosema, imetosha kwa washenzi wa magahribi kutaka kutuchezea. Imetosha, hebu tuwazime na kuwashikisha adabu. Kuna mengine siwezi kukuambia moja kwa moja, ila jua kuwa Taifa linatikisika hivi sasa. Rais, Mhe. Jovin Sekendu anaishi kwa wasiwasi mkubwa. Inabidi tumtafute yeyote aliyeko nyuma ya mpango huu” Bi. Anita alisema kwa uchungu. Maneno ambayo yaliuchoma moyo wa Jacob Matata na kumfanya awe tayari kwa kazi.
Baada ya hapo, waziri mkuu na Bi. Anita walimuaga mpelelezi Jacob Matata, ambaye angebaki ndani ya nyumba ile kama walivyosema.
“Nitajitahidi kufanya linalowezekana, japo naona jambo lenyewe limejifungafunga sana na muda wake ni mchache. Tuombe heri.” Jacob alisema huku macho yake yakiwasindikiza wakuu hawa waliokuwa wakitoka. Wote wawili walitembea kutoka mle chumbani huku Jacob Matata akiwa amesimama, mkono wake wa kushoto ukiwa umeshikilia lile faili. Walitoka mlangoni na wa mwisho kutoka alikuwa Mhe. Silas Kiondo, ambaye kabla hajafunga mlango nyuma yake aligeuka akamwangalia Jacob Matata, macho yao yakakutana.
"Jacob.."Mhe. Silas Kiondo aliita. Jacob akanyanyua kope kabla ya kusema, "Mkuu".
"Fanya kazi yako kwa makini, taifa hili linategemea sana matokeo ya kazi yako. Binafsi nimefurahi kuonana na wewe nimekuwa nakusikia tu." Waziri alisema, hakusubiri jibu la Jacob Matata.
Itaendelea
Leo ntatupia episode 2