mtzmweusi
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 8,593
- 8,876
-1-
“KWA NINI UMEMCHAGUA POKA KINGU, wakati siku za karibuni kumejitokeza mafundi wengi wa kufanya mauaji, kwa ustadi wa hali ya juu?’’
“Huyu anafaa! Aliongea Ngongoseke
“Ndiyo niambie sasa, kwa nini anafaa?
“Poka Kingu ni mvivu.” Akajibu Ngongoseke kwa utulivu huku akifikiri.
“Uvivu ni sifa nzuri ya kumchagua mtu?” Mzungumzaji wa upande wa pili wa simu, ambaye ni mzungu. Akauliza kwa mshangao.
“Hasa!” Ngongoseke akasisitiza.
“Yaani unataka mtu mvivu, kwenye kazi ngumu na hatari kama hii?” Mzungu huyo akauliza, kutoka upande wa pili wa simu. Katika mshangao usiyoelezeka.
“Ndiyo! Nimepitia mafaili takribani saba, niliyoletewa mezani, yenye sifa za watu ninaowahitaji, kwa ajili ya kazi hii. Nimejiridhisha kuwa, Poka Kingu ana vigezo vya kuwazidi wengine. Kutokana na kazi ninayotaka ifanyike.” Akaongea Ngongoseke kwa hakika. Mkono wake mmoja ameshika kiwambo cha simu sikioni, mkono wake mwingine, ukipapasa waya wa simu hiyo ya mezani.
“Sifa yenyewe ndiyo iwe uvivu?”
“A killer on the payroll isn't good for business. Sitaki mazoea, nataka msisimko wa kazi.” Ngongoseke akasisitiza.
“Unadhani mtu aliyeko kwenye orodha ya malipo, hafai kwa kazi hiyo?” Mzungumzaji wa upande wa pili, akauliza kwa udadisi. Akionekana kutoridhishwa na uamuzi wa Ngongoseke.
“Vidole vyao ni vizito kwa shabaha, mishipa yao imejaa mafuta kwa sababu wanalipwa mishahara minono na kula ovyo. Hawana njaa wala mdadi wa kazi.” Akafafanua Ngongoseke.
“Hii kali! Yaani uvivu umekuwa sifa kwa muuaji tishio!” Akashangaa Mzungu simuni.
“Sitaki mtu anayeua kwenye muda wa nyongeza, yaani, extra time killer. Mtu ambaye ananiweka kwenye wasiwasi kwa muda mwingi. Nataka muuaji anayekamilisha kazi yake bila kutoa jasho, ndani ya sekunde za awali za tukio.” Ngongoseke akafafanua.
“Okay! Sifa nyingine ni ipi?”
“Poka Kingu anaweza kuishi kama mzimu. Kwa vile ana hulka ya uvivu, hapendi kupambana na mtu kwa muda mrefu. Hivyo hujua namna ya kujificha na kuua haraka, pale anapopata nafasi finyu ya kufanya hivyo. Kwenye kazi hii, sitaki mtu wa kuremba. Kumbuka watu tunaokwenda kupambana nao, hawastahili kupata nafasi ya kuishi mara mbili. Lazima wafe hata kwenye mpenyo mdogo wa kupitisha wembe.
“Uvivu wake umemfanya awe mtu anayeshika rekodi ya juu barani Afrika. Rekodi ya kuua watu wengi ndani ya muda mfupi zaidi kwa mapambano ya ana kwa ana. Uvivu umemfanya awe stadi wa mapigo ya kifo, kwa vile asivyopenda kupoteza muda. Hapendi kushughulika na mtu au jambo fulani kwa muda mrefu, kwa vile anavyopenda kupumzika na kustarehe. Hivyo amejifunza kupiga mapigo machache ya kifo. Hataki kumpiga mtu muda mrefu. Namfananisha na wembe upitavyo kwa wepesi kwenye mnofu wa nyama. Huyu atatufaa sana. Inadhaniwa kuwa ndiye mtu makini anayeweza kuua haraka bila silaha.” Ngongoseke akaweka kituo huku akitazama picha ya Poka Kingu kwenye jalada juu ya meza iliyokuwa mbele yake.
“Okay! sikuwahi kuwaza kuwa uvivu unaweza kuwa sifa ya muuaji hatari wa kukabidhiwa kazi hatari kama hii.” Mzungu akaongea kwa shauku huku wasifu wa Poka Kingu ukionekana kumuelea vyema.
“Wauaji wasio makini hawaoni shida kukwambia, watu uliowatuma kuwaua wamewaponyoka kwa bahati mbaya. Japo watakuambia kuwa wamefanikiwa kuwajeruhiwa vibaya. Mbaya zaidi, watakueleza kuwa hawafahamu aliyenusurika kuuawa amekimbilia wapi. Poka Kingu hafanyi makosa ya namna hiyo. To me, when a serial killer have to kill the same target twice in one week, then there's either something wrong with his skills or something wrong with instructions. Nataka akipiga amepiga, tumesahau na tunaongelea habari nyingine.” Alisema Ngongoseke huku akiweka msisitizo kwa lugha ya Kiingereza.
“Okay! Sasa naanza kuafikiana na wewe. Hata hivyo bado nina shaka.”
“Shaka gani?” Ngongoseke akauliza kwa udadisi.
“Poka Kingu yuko kifungoni, tena kwenye gereza la wafungwa hatari, linalolindwa kwa ulinzi mkali, masaa ishirini na nne, siku saba kwa wiki. Bila shaka kumbukumbu zangu ziko sahihi, sivyo?” alihoji Mzungu huyo
“Upo sahihi kabisa. Usijali suala hilo niachie mimi. Unajua huwezi kujua kila kitu kabla ya kuanza kutekeleza jambo lenyewe. Ujuvi wa jambo huja wakati jambo hilo likiwa linaendelea kutendeka. Kukaa na kusubiri ujue kila kitu kabla ya kuanza kutekeleza jambo, ni sawa na kupoteza muda. Tunachotakiwa ni kuwa tayari kwa mambo yasiyojulikana.” Ngongoseke akajitapa na kuongeza.
“Tunachopaswa kufanya sasa ni kutafuta watu wa kufanya nao kazi. Wiki chache zijazo, nitakuwa nimetengeneza timu ya kazi na kuanza fujo ndani ya jiji hili la Dar es Salaam.”
“Hebu niambie juu ya hiyo timu unayotarajia kuitumia.” Mzungumzaji wa upande wa pili, akazidi kuhoji.
“Poka, Naomi, Misanya, Nyoso na Mheshimiwa, wataongoza timu hiyo katika mazingira na nyakati tofauti.” Ngongoseke akabainisha mpango wake.
“Mh! Mbona sioni mchanganyiko mzuri kati ya Poka Kingu na yule mrembo Naomi?” Mzungu akatia shaka kwa mara nyingine.
“Hawa viumbe wawili, ni kama pande mbili za sarafu. Hazifanani lakini zinafanya thamani ya pesa. Ni kama jua linavyotawala mchana, na mbalamwezi unavyoangaza usiku, vyote huangaza dunia. Naomi na Poka wanaunganishwa na hewa iliyopo pande zote, yaani, mchana na usiku. Uwanja wa Poka Kingu ni sehemu ya jua kali na misukosuko. Sehemu yenye upole na mwanga hafifu wa mbalamwezi, yenye hamasa za mahaba, ni ya Naomi Nanalungu. Wote wapo kwenye sayari moja ya matukio ya kutisha, wakiishi kwa kuvuta hewa moja, mchana na usiku.” Ngongoseke akafafanua nadharia yake kwa ujivuni.
“Kwa hivyo Poka unamfananisha na Jua, anafanya kazi mchana kwenye mazingira magumu. Naomi kama mwezi, anafanya kazi usiku kwenye mazingira laini yenye mahaba. Umesema wanaunganishwa na hewa ambayo iko mchana na usiku. Sasa hewa ndiyo nani kwenye nadharia yako?” Mzungu akahoji.
“Hiyo sehemu ya hewa ndiyo mimi. Sionekani lakini nitawaunganisha vyema.” Ngongoseke akaongea kwa utulivu na kuweka kituo. Baada ya ukimya mfupi wa tafakuri, mtu wa upande wa pili akasema.
“Lo! Nimevutiwa sana na mkakati wako. Nadhani mpango wetu utafanikiwa bila shaka.” Kauli hiyo ikafuatiwa na kimya kifupi.
“Nataka Tanzania ichafuliwe, nataka kusiwe na ripoti yoyote kuhusiana na gesi ya Mtwara. Sijui nikueleze vipi ili uelewe namna wakubwa watakavyofurahi, baada ya kufanikiwa kwa tukio hili. Makampuni takribani kumi na tano ya nchi za ulaya na Marekani, yatasaini mkataba wa kuendelea kununua gesi kutoka PAW & Company. Mpango huu ukishindwa, makampuni yote yatakimbilia kwenye gesi ya Mtwara. Ambayo itakuwa rahisi kwao kununua, na upatikanaji wake ni endelevu wa muda mrefu, kutokana na siasa tulivu za Tanzania”
“Hivi sasa kampuni zote zimeshaweka angalizo kuwa hazina hakika kama zitaongeza mkataba wa kununua gesi kwetu. Baada ya kutathimini angalizo lao hilo, tumejiridhisha kuwa zinasubiri hiyo ripoti ambayo inaandaliwa sasa kuhusu gesi ya Mtwara. Ni wazi kuwa tukiharibu utaratibu mzima wa ripoti hiyo katika kiwango ambacho kitaifanya Tanzania itake siyo chini ya mwaka mmoja kuandaa ripoti nyingine. Tutakuwa tumefanikiwa kuyalazimisha makampuni hayo kuendeleza mkataba wa kibiashara baina yetu. Nasi tutawabana walau mkataba mpya uwe wa miaka kumi, ili hata kama Tanzania ikijipanga upya, ikute tumeshatawala soko. Hivyo kazi hii ni muhimu sana kwako na kwetu, bwana Ngongoseke.”
“Ondoa shaka! Japokuwa inaonekana ni kazi ngumu, lakini itafanyika tu. Nikimaliza hii kazi, nitakuja Washington kununua zile nyumba, ulizoniambia habari yake. Nifanyie mpango.” Ngongoseke akaongea kwa hakika, huku akisimama.
“Bila shaka. Kesho nitakutumia picha za nyumba unazoweza kununua, zilizopo maeneo mazuri.” Mzungu akaongea kwa matumaini, upande wa pili wa simu.
“Nitashukuru sana. Basi tutawasiliana wiki ijayo baada ya mambo kuanza.” Ngongoseke akasisitiza.
“Sawa! Natarajia kusikia kasheshe huko. Nimetuma malipo ya awali, malipo ya pili yatafanyika nitakapopata kiboksi cheusi cha kurekodi safari ya ndege. Malipo ya mwisho yatafanyika pale itakapothibitika, kuwa timu yako imefanikiwa kuondoa na kuharibu nakala zote za ripoti ya gesi ya Mtwara.” Mzungu akafafanua.
“Mtathibitishaje kuwa nakala zote zimefutwa?” Ngongoseke akahoji.
“Ni rahisi sana.”
“Kwa vipi?”
“Tanzania itakapoanza upya mchakato wa kupima na kuandika ripoti mpya kuhusu; mchanganuo, aina, ubora na thamani halisi ya gesi ya Mtwara. Jambo ambalo litawachukua takribani mwaka mzima kulifanya. Hapo tutajua kuwa mpango wetu ulifanikiwa na kampuni yetu itakuwa imefanikisha azma yake. . Na ndiyo hapo tutajua kuwa ulifanya vema kazi yako.”
“Nashangaa unatia hofu wakati unajua rekodi yangu ya kazi.”
Njoo tena saa 12:00 jioni.
Like au Comment ili nijue kuna watu wanafuatilia.
Sent using Jamii Forums mobile app
“KWA NINI UMEMCHAGUA POKA KINGU, wakati siku za karibuni kumejitokeza mafundi wengi wa kufanya mauaji, kwa ustadi wa hali ya juu?’’
“Huyu anafaa! Aliongea Ngongoseke
“Ndiyo niambie sasa, kwa nini anafaa?
“Poka Kingu ni mvivu.” Akajibu Ngongoseke kwa utulivu huku akifikiri.
“Uvivu ni sifa nzuri ya kumchagua mtu?” Mzungumzaji wa upande wa pili wa simu, ambaye ni mzungu. Akauliza kwa mshangao.
“Hasa!” Ngongoseke akasisitiza.
“Yaani unataka mtu mvivu, kwenye kazi ngumu na hatari kama hii?” Mzungu huyo akauliza, kutoka upande wa pili wa simu. Katika mshangao usiyoelezeka.
“Ndiyo! Nimepitia mafaili takribani saba, niliyoletewa mezani, yenye sifa za watu ninaowahitaji, kwa ajili ya kazi hii. Nimejiridhisha kuwa, Poka Kingu ana vigezo vya kuwazidi wengine. Kutokana na kazi ninayotaka ifanyike.” Akaongea Ngongoseke kwa hakika. Mkono wake mmoja ameshika kiwambo cha simu sikioni, mkono wake mwingine, ukipapasa waya wa simu hiyo ya mezani.
“Sifa yenyewe ndiyo iwe uvivu?”
“A killer on the payroll isn't good for business. Sitaki mazoea, nataka msisimko wa kazi.” Ngongoseke akasisitiza.
“Unadhani mtu aliyeko kwenye orodha ya malipo, hafai kwa kazi hiyo?” Mzungumzaji wa upande wa pili, akauliza kwa udadisi. Akionekana kutoridhishwa na uamuzi wa Ngongoseke.
“Vidole vyao ni vizito kwa shabaha, mishipa yao imejaa mafuta kwa sababu wanalipwa mishahara minono na kula ovyo. Hawana njaa wala mdadi wa kazi.” Akafafanua Ngongoseke.
“Hii kali! Yaani uvivu umekuwa sifa kwa muuaji tishio!” Akashangaa Mzungu simuni.
“Sitaki mtu anayeua kwenye muda wa nyongeza, yaani, extra time killer. Mtu ambaye ananiweka kwenye wasiwasi kwa muda mwingi. Nataka muuaji anayekamilisha kazi yake bila kutoa jasho, ndani ya sekunde za awali za tukio.” Ngongoseke akafafanua.
“Okay! Sifa nyingine ni ipi?”
“Poka Kingu anaweza kuishi kama mzimu. Kwa vile ana hulka ya uvivu, hapendi kupambana na mtu kwa muda mrefu. Hivyo hujua namna ya kujificha na kuua haraka, pale anapopata nafasi finyu ya kufanya hivyo. Kwenye kazi hii, sitaki mtu wa kuremba. Kumbuka watu tunaokwenda kupambana nao, hawastahili kupata nafasi ya kuishi mara mbili. Lazima wafe hata kwenye mpenyo mdogo wa kupitisha wembe.
“Uvivu wake umemfanya awe mtu anayeshika rekodi ya juu barani Afrika. Rekodi ya kuua watu wengi ndani ya muda mfupi zaidi kwa mapambano ya ana kwa ana. Uvivu umemfanya awe stadi wa mapigo ya kifo, kwa vile asivyopenda kupoteza muda. Hapendi kushughulika na mtu au jambo fulani kwa muda mrefu, kwa vile anavyopenda kupumzika na kustarehe. Hivyo amejifunza kupiga mapigo machache ya kifo. Hataki kumpiga mtu muda mrefu. Namfananisha na wembe upitavyo kwa wepesi kwenye mnofu wa nyama. Huyu atatufaa sana. Inadhaniwa kuwa ndiye mtu makini anayeweza kuua haraka bila silaha.” Ngongoseke akaweka kituo huku akitazama picha ya Poka Kingu kwenye jalada juu ya meza iliyokuwa mbele yake.
“Okay! sikuwahi kuwaza kuwa uvivu unaweza kuwa sifa ya muuaji hatari wa kukabidhiwa kazi hatari kama hii.” Mzungu akaongea kwa shauku huku wasifu wa Poka Kingu ukionekana kumuelea vyema.
“Wauaji wasio makini hawaoni shida kukwambia, watu uliowatuma kuwaua wamewaponyoka kwa bahati mbaya. Japo watakuambia kuwa wamefanikiwa kuwajeruhiwa vibaya. Mbaya zaidi, watakueleza kuwa hawafahamu aliyenusurika kuuawa amekimbilia wapi. Poka Kingu hafanyi makosa ya namna hiyo. To me, when a serial killer have to kill the same target twice in one week, then there's either something wrong with his skills or something wrong with instructions. Nataka akipiga amepiga, tumesahau na tunaongelea habari nyingine.” Alisema Ngongoseke huku akiweka msisitizo kwa lugha ya Kiingereza.
“Okay! Sasa naanza kuafikiana na wewe. Hata hivyo bado nina shaka.”
“Shaka gani?” Ngongoseke akauliza kwa udadisi.
“Poka Kingu yuko kifungoni, tena kwenye gereza la wafungwa hatari, linalolindwa kwa ulinzi mkali, masaa ishirini na nne, siku saba kwa wiki. Bila shaka kumbukumbu zangu ziko sahihi, sivyo?” alihoji Mzungu huyo
“Upo sahihi kabisa. Usijali suala hilo niachie mimi. Unajua huwezi kujua kila kitu kabla ya kuanza kutekeleza jambo lenyewe. Ujuvi wa jambo huja wakati jambo hilo likiwa linaendelea kutendeka. Kukaa na kusubiri ujue kila kitu kabla ya kuanza kutekeleza jambo, ni sawa na kupoteza muda. Tunachotakiwa ni kuwa tayari kwa mambo yasiyojulikana.” Ngongoseke akajitapa na kuongeza.
“Tunachopaswa kufanya sasa ni kutafuta watu wa kufanya nao kazi. Wiki chache zijazo, nitakuwa nimetengeneza timu ya kazi na kuanza fujo ndani ya jiji hili la Dar es Salaam.”
“Hebu niambie juu ya hiyo timu unayotarajia kuitumia.” Mzungumzaji wa upande wa pili, akazidi kuhoji.
“Poka, Naomi, Misanya, Nyoso na Mheshimiwa, wataongoza timu hiyo katika mazingira na nyakati tofauti.” Ngongoseke akabainisha mpango wake.
“Mh! Mbona sioni mchanganyiko mzuri kati ya Poka Kingu na yule mrembo Naomi?” Mzungu akatia shaka kwa mara nyingine.
“Hawa viumbe wawili, ni kama pande mbili za sarafu. Hazifanani lakini zinafanya thamani ya pesa. Ni kama jua linavyotawala mchana, na mbalamwezi unavyoangaza usiku, vyote huangaza dunia. Naomi na Poka wanaunganishwa na hewa iliyopo pande zote, yaani, mchana na usiku. Uwanja wa Poka Kingu ni sehemu ya jua kali na misukosuko. Sehemu yenye upole na mwanga hafifu wa mbalamwezi, yenye hamasa za mahaba, ni ya Naomi Nanalungu. Wote wapo kwenye sayari moja ya matukio ya kutisha, wakiishi kwa kuvuta hewa moja, mchana na usiku.” Ngongoseke akafafanua nadharia yake kwa ujivuni.
“Kwa hivyo Poka unamfananisha na Jua, anafanya kazi mchana kwenye mazingira magumu. Naomi kama mwezi, anafanya kazi usiku kwenye mazingira laini yenye mahaba. Umesema wanaunganishwa na hewa ambayo iko mchana na usiku. Sasa hewa ndiyo nani kwenye nadharia yako?” Mzungu akahoji.
“Hiyo sehemu ya hewa ndiyo mimi. Sionekani lakini nitawaunganisha vyema.” Ngongoseke akaongea kwa utulivu na kuweka kituo. Baada ya ukimya mfupi wa tafakuri, mtu wa upande wa pili akasema.
“Lo! Nimevutiwa sana na mkakati wako. Nadhani mpango wetu utafanikiwa bila shaka.” Kauli hiyo ikafuatiwa na kimya kifupi.
“Nataka Tanzania ichafuliwe, nataka kusiwe na ripoti yoyote kuhusiana na gesi ya Mtwara. Sijui nikueleze vipi ili uelewe namna wakubwa watakavyofurahi, baada ya kufanikiwa kwa tukio hili. Makampuni takribani kumi na tano ya nchi za ulaya na Marekani, yatasaini mkataba wa kuendelea kununua gesi kutoka PAW & Company. Mpango huu ukishindwa, makampuni yote yatakimbilia kwenye gesi ya Mtwara. Ambayo itakuwa rahisi kwao kununua, na upatikanaji wake ni endelevu wa muda mrefu, kutokana na siasa tulivu za Tanzania”
“Hivi sasa kampuni zote zimeshaweka angalizo kuwa hazina hakika kama zitaongeza mkataba wa kununua gesi kwetu. Baada ya kutathimini angalizo lao hilo, tumejiridhisha kuwa zinasubiri hiyo ripoti ambayo inaandaliwa sasa kuhusu gesi ya Mtwara. Ni wazi kuwa tukiharibu utaratibu mzima wa ripoti hiyo katika kiwango ambacho kitaifanya Tanzania itake siyo chini ya mwaka mmoja kuandaa ripoti nyingine. Tutakuwa tumefanikiwa kuyalazimisha makampuni hayo kuendeleza mkataba wa kibiashara baina yetu. Nasi tutawabana walau mkataba mpya uwe wa miaka kumi, ili hata kama Tanzania ikijipanga upya, ikute tumeshatawala soko. Hivyo kazi hii ni muhimu sana kwako na kwetu, bwana Ngongoseke.”
“Ondoa shaka! Japokuwa inaonekana ni kazi ngumu, lakini itafanyika tu. Nikimaliza hii kazi, nitakuja Washington kununua zile nyumba, ulizoniambia habari yake. Nifanyie mpango.” Ngongoseke akaongea kwa hakika, huku akisimama.
“Bila shaka. Kesho nitakutumia picha za nyumba unazoweza kununua, zilizopo maeneo mazuri.” Mzungu akaongea kwa matumaini, upande wa pili wa simu.
“Nitashukuru sana. Basi tutawasiliana wiki ijayo baada ya mambo kuanza.” Ngongoseke akasisitiza.
“Sawa! Natarajia kusikia kasheshe huko. Nimetuma malipo ya awali, malipo ya pili yatafanyika nitakapopata kiboksi cheusi cha kurekodi safari ya ndege. Malipo ya mwisho yatafanyika pale itakapothibitika, kuwa timu yako imefanikiwa kuondoa na kuharibu nakala zote za ripoti ya gesi ya Mtwara.” Mzungu akafafanua.
“Mtathibitishaje kuwa nakala zote zimefutwa?” Ngongoseke akahoji.
“Ni rahisi sana.”
“Kwa vipi?”
“Tanzania itakapoanza upya mchakato wa kupima na kuandika ripoti mpya kuhusu; mchanganuo, aina, ubora na thamani halisi ya gesi ya Mtwara. Jambo ambalo litawachukua takribani mwaka mzima kulifanya. Hapo tutajua kuwa mpango wetu ulifanikiwa na kampuni yetu itakuwa imefanikisha azma yake. . Na ndiyo hapo tutajua kuwa ulifanya vema kazi yako.”
“Nashangaa unatia hofu wakati unajua rekodi yangu ya kazi.”
Njoo tena saa 12:00 jioni.
Like au Comment ili nijue kuna watu wanafuatilia.
Sent using Jamii Forums mobile app