Tupo pamojaShukrani sana poti
PamojaSafi sana kaka!
Kitu kitamu saňa hiki I see.- 17 -
Riwaya: MSAKO
Mtunzi: Japhet Nyang’oro
Frank Misanya yeye akasema ahesabu kila kitu kimeshakamilika. Akapiga simu nyingine mbili kwa vigogo. Halafu akapiga masafa marefu huko ughaibuni. Alipomaliza, alijuhusudu yeye mwenyewe; hakuna ambaye angeweza msifia kwa vile wachache waliokuwa wanajua alichokuwa anafanya. Na mbinu yake ni moja, kila aliyempa kazi alimpa kipande cha kazi, kazi kamili alikuwa akiijua yeye mwenyewe. Huyo ndiyo Ngongoseke Amos Nkwija.
*****Kitabu cha riwaya hii sasa kinachapwa kwa idadi ya wale walioweka ODA tu, kinatoka tarehe 15/6/2020. Weka ODA yako sasa 0762204166********
BAADA ya kutoka yalipo majengo ya Ofisi Fukuzi, mpelelezi Jacob Matata aliazimia kuanzia nyumbani kwa Afande Lucas. Kufutwafutwa kwa faili alilokuwa ameandaa kisha kuuawa ilikuwa dalili tosha kuwa kuna hatua alikuwa amepiga katika uchunguzi wake. Hivyo kwenda msibani na kuonana na mjane aliona kuwa lingekuwa wazo zuri. Afande Lucas alikuwa akiishi uraiani, Mwananyamala Komakoma jirani na Mwinjuma road.
Hakupata shida kuiona nyumba yenyewe, wamama wenye khanga tatu-tatu walionekana kufanya hili na lile. Upande wa kulia wa nyumba hiyo kulikuwa na turubai lililowekwa ili kuwapa watu kivuli. Aliangalia saa yake ya mkononi ilikuwa saa tano na dakika arobaini asubuhi. Kama utakumbuka wakati huu ndiyo Bi. Anita na yeye alikuwa ofisini kwake. Jacob Matata aliendesha taratibu kuliendea eneo lile. Hakukuwa na sehemu ya kuegesha gari hivyo alipitiliza kwa mwendo mdogo huku akijitahidi kutafuta sehemu ya kuegesha. Mbanano wa nyumba na ujenzi usio na mpangilio katika eneo hili ulifanya uzuri wa nyumba ambayo watu walikuwa wamejaa usionekane.
Aliiangalia ile nyumba ambayo aliamini kuwa ndiyo yalipo makazi ya marehemu Inspekta Lucas. Ilikuwa nyumba nzuri ya kisasa na thamani kubwa. Alishangaa kuona nyumba kama ile kujengwa eneo kama lile, maana nyumba kama hizo huonekana yale maeneo ya watu wazito. Kingine alichoshangaa ni kwa namna gani Askari Polisi alifanikiwa kujenga nyumba ya kifahari kama ile, ila alipokumbuka kuwa kwenye nchi yake mtu anaweza pata pesa kwa njia nyingi, alinyamaza. Kutafuta sehemu ya kuegesha kulimpeleka hadi mtaa wa nyuma ambapo kulikuwana kiwanja ambacho hakijajengwa. Hapo alikuta magari kadhaa yakiwa yameegeshwa. Kwa bahati nzuri aliona sehemu ambayo alipachika gari alilokuwa anatumia ambalo alikuwa amelikodisha. Hakuona busara kwenda nyumbani kwake baada ya yale yaliyokuwa yametokea usiku. Pia, isingekuwa akili nzuri kutumia gari lake analotumia siku zote. Hadhari lilikuwa jambo la msingi sana kwake wakati huu. Baada ya kuteremka na kufunga gari aliangaza kama anaweza pata kichochoro cha kumpeleka nyumbani kwa Afande Lucas, badala ya kuzunguka na barabara. Mara hii tena bahati ilikuwa upande wake, aliona kichochoro ambacho pia kilikuwa kikipitisha maji machafu. Haikuchukua muda alihisi yuko nyuma ya nyumba aliyokuwa akiiendea maana aliweza kusikia sauti za watu wakiongea katika hali ya kushirikiana kazi za upishi. Aliendelea mbele kidogo hadi alipokuwa usawa wa dirisha moja. Alipofika hapo alisita kidogo baada ya kusikia sauti ambayo haikustahili kusikika msibani. Alisimama kisha akajivuta ukutani jirani na lile dirishi ilikotokea ile sauti nzito ya amri.
“Kama akija mtu atakayejitambulisha kwa jina hilo tupe taarifa, maana mtu huyo ni hatari kwako na familia yako. Chukua simu hii, ukiminya tu hiki kidude utaongea na mimi moja kwa moja nami nitatuma askari wakusaidie. Pia, ukihitaji hela ziko kwenye akaunti yako ya benki.” Ilikuwa ni sehemu ya sauti hiyo nzito iliyoongea kwa amri. Jacob alitaka kuchungulia ili amwone aliyekuwa akiongea lakini kulikuwa na pazia zito hivyo hakufanikiwa. Aliharakisha kutembea ili awahi kuwaona watu hao kabla hawajatokomea. Akiwa na matumaini ya kufanikisha hilo mara uchochoro ule ukampeleka mbele ya dimbwi kubwa la maji machafu. Kwa mbele yake kulikuwa na choo ambacho kuta zake zilikuwa ni mabati na pembeni yake ambapo ndio kichochoro hiki kilipita lilichimbwa hilo shimo kubwa lililokuwa na maji machafu. Ilivyokuwa hakuwa na namna ya kuenedela na kichochoro hicho la sivyo ajitolee kutumbukia kwenye maji yale. Aliangalia kwa namna ya kukata tamaa, hii ilimaanisha asingeweza kuonana na yeyote aliyeongea kwa ile sauti. Alikata shauri kurudi na kuzunguka na barabara.
* * *
Wakati Jacob Matata akikwama kwenye kile kichochoro, Luteni Frank Misanya yeye alikuwa ndani ya gari lake akiendesha wakati simu ya Ngongoseke ilipoingia. Alipunguza mwendo wakati anakunja kushoto mbele ya Chuo cha Diplomasia akiiacha barabara ya Kilwa na kuingia Kurasini, mkono wa kushoto ulichukua simu hiyo iliyokuwa ikilia kwa fujo.
“Sema!’’ Alisema baada ya kuona namba asiyoifahamu “Ngongoseke hapa.” Alijitambulisha.
“Sema Mzee!’’ Luteni Misanya alisema.
“Nilikwambia wale vijana wamejua mengi kuhusu kazi zetu....” Ngongoseke alisema kabla hajakatizwa na Frank,
“Yaani umejuaje hapa ndio nakaribia nyumba wanayoishi, nataka nikawam...” Frank alisema lakini naye alikatishwa,“ Nilikwambia usiwaue wewe. Sasa sikiliza, sasa hivi wapeleke pale anapokaa Nanalungu, Jacob Matata, yuko hapo.” Ngongoseke alisema
“Aaaaah, aisee wewe Mzee ni kiboko!” Luteni Frank alisema, maana alishaelewa akili ya Ngongoseke.
“Ulikuwa hujui au unathibitisha tu?’’ Ngongoseke alisema kwa majivuni.
“Akili yako inafanya kazi kwa kiwango cha ajabu sana.” Frank alisema.
“Waende sasa hivi maana nimeambiwa Jacob yuko hapo muda huu. Yeye atatusaidia kuwaua.” Ngongoseke alisema.
* * *
Robo saa baada ya Ngongoseke kutoa maelekezo hayo kwa Luteni Frank Misanya, Jacob Matata yeye sasa alikuwa mbele ya mlango wa chumba alichoelekezwa kuwa mjane wa Afande Lucas alikuwemo. Kama alivyoiona kwa mbali, ilikuwa nyumba kubwa ambayo hukuhitaji elimu kubwa kuitaja kuwa ya kifahari japo ilikuwa maeneo yasiyoistahiki kuwepo. Alibisha na kukaribishwa. Aliangaza macho huku na huko. Kilikuwa chumba kilichojaa wanawake tu, ambao wengi wao macho yao yalikuwa mekundu na wengine yakiwa yamevimba. Mara alimwona msichana mmoja mrembo wa haja ambaye pembeni yake kulikuwa na kitu kama simu. Macho yake yakavutika na muundo wa ile simu, aliiangalia tena kwa makini na mara Jacob Matata akabaini kwa kilikuwa kinasa sauti. Akili ya Jacob Matata ilifanya kazi haraka, alijua yule mtu mwenye sauti ya amri ndiye aliyempatia huyo mwanamke kile kifaa akimdanganya kuwa ni simu ili aweze kurekodi mazungumzo yote ya yule Mjane wa Afande Lucas.
“Pole sana dadangu!” Jacob alisema baada ya kuwa ameinama alipokuwa ameketi yule dada. Alikuwa mwanamke, mzuri, mrembo wa umri wa kati, si mtoto si mtu mzima. Maana Jacob yeye anajua kuwa urembo na uzuri kwa manamke ni vitu viwili tofauti, lakini huyu alikuwa navyo vyote.
“Asante sana!” Alisema yule msichana kwa sauti kavu, huku akijitahidi kumwangalia Jacob Matata.
“Sijui unawe......” Kabla Jacob Matata hajamaliza alichotaka kusema, yule mwanamke haraka akaweka kidole katikati ya midomo yake kama ishara ya kumtaka Jacob Matata anyamaze. Kisha akasimama na kumwonyesha Jacob ishara kuwa amfuate.
“Bila shaka unaitwa Jacob Matata?’’ Msichana alihoji. “Kama ndiye?’’ Jacob alisema kwa mshangao.
“Ndiye wewe, maana hata jibu lako limekuwa sawa na nilivyoelekezwa na mume wangu. Naitwa Nana Lucas, marehemu mume wangu katika siku zake za mwisho alikuwa anakutafuta sana. Alijua maisha yake yako hatarini ila hakuona kama angeweza pata msaada toka kwa mtu yeyote yule mwingine zaidi yako. Juhudi zake za kukutafuta hazikuzaa matunda hadi alipouawa. Ila akawa amenielezea sifa zako akiwa na hakika kuwa kwa namna moja ama nyingine ungeingia kupeleleza kitu alichokuwa ameanza kupeleleza. Hivyo alikuwa na hakika kuwa ipo siku ungekuja kwangu. Hivyo nilivyokuona tu mara moja nikajua ndiye.” Alisema yule mwanamke huku sasa machozi yakiwa yanamtiririka. Jacob alimvuta na kuanza kumbembeleza.
“Je, unaweza kuniambia kama kuna lolote alitaka unifikishie?’’ Jacob alisema kwa sauti ya kubembeleza pia, huku akili yake ikiwa makini kabisa.
“Jumatatu wiki iliyopita ndiyo alikuja akiwa amebadilika sana. Nikamuuliza vipi, akaniambia kuna kazi amekuwa akifanya, anasema uchunguzi wake umemfikisha sehemu ambayo amegundua kuna watu wa usalama na viongozi wanahusika. Hilo halikumtisha sana, ila anasema alimtembelea Luten Frank Misanya, baada ya kuongea naye amemtishia maisha kama hatoachana na kazi hiyo. Hivyo akaniambia nikikuona nikuombe uanzie kwa Luten Frank Misanya.” Alisema yule msichana huku akilia kwa kwikwi.
“Je, kuna jingine Nana?’’ Jacob alihoji.
“Hapana Jacob, ila kuna watu walikuja wakijifanya wao ni Jacob Matata na kuniuliza kama kuna ujumbe wowote marehemu aliuacha kwa ajili yao. Lakini katika wote sikuona kama kuna mtu ana viashiria vya sifa ambazo mume wangu aliniambia. Hivyo sikusema lolote.’’
“Okay, bila shaka ndiyo waliyokupa hiyo simu ambayo pia ni kinasa sauti?’’ Jacob alihakiki.
“Ndiyo, nilipoiona niligundua. Wengi hudhani miye ni mwanamke wa kawaida tu, lakini si kweli. Ni mtu niliyepitia mafunzo mengi ya namna hiyo wafanyayo na mapenzi yangu kwa Lucas yaliyonifanya nijitulize kwake. Lakini hivi nilishapanga kama nisipokuona kesho nianze mikakati ya kisasi. Mazishi tumefanya jana, nilipanga kupumzika leo halafu kesho nianze mishe-mishe.” Nana alisema.
“Ulipanga ungeanzaje kulipa kisasi?’’ Jacob alihoji.
“Sina mpango kamili kwa sasa, ila kwa harakaharaka bila shaka ningeanza na waliokuja kunipa hii simu.” Nana alisema.
“Nadhani inaweza kuwa hatari kuliko unavyodhani.’’ Jacobo alisema kisha akamkumbatia yule Msichana ambaye sasa alianza kububujikwa na machozi.
“Nini kimekufanya uamini kuwa mimi ndiye Jacob Matata?’’ Swali hilo la Jacob lilimfanya yule msichana amsukume Jacob na kujitoa mikononi mwake. Akamwangalia kwa muda kana kwamba ndiyo kwanza anamwona. Kisha kwa sauti ya kutafakari akasema, “Wewe siyo kama askari wengine, askari ni wababe na wala siyo kama jambazi, una mvuto kwa mwanamke na ndiyo mume wangu alivyoniambia. Kitendo cha kupiga magoti pale wakati unanisalimia, muonekano wako na ulivyoitoa ile pole ilikuwa alama tosha kuwa wewe ndiye!’’ Alisema alafu akamkumbatia tena Jacob Matata huku, akilia kwa sauti na uchungu.
“Jacob, nisaidie kulipa kisasi kwa Mwenda wangu. Niko tayari kukusaidia kama ukitaka!’’ Alisema kwa uchungu, sauti yake kama iliingia kwenye masikio ya Jacob, haikuishia hapo tu bali iliingia kwenye nafsi na moyo wake. Matokeo yake akajikuta akisema,
“Tuombe uzima, Mungu atusaidie.”
"Kwa nini nisiwapigie halafu uje uwakamate Jacob?’’ Nana alihoji.
"Wazo zuri lakini sishauri ufanye hivyo. Watu hawa si wa kuwafanyia mzaha hata kidogo. Endelea kuwepo, ukiwa mtulivu na kufanikiwa kuwafanya wasijue kuwa umeonana na mimi hilo litatusaidia sana mbele ya safari tukiendelea kuwa hai. Lengo si kupata tawi bali mzizi wa mambo haya.’’ Jacob alisema huku macho yake yakiwa yametulia kifuani kwa Nanalungu. Alihusudu jinsi Afande Lucas alivyokuwa amefanikiwa kuchagua mwanamke mrembo.
Kama umesoma weka like na comment yako nijue tuko wote[emoji1488]
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Dah! Kaka hizi kazi zako ingekuwa Bibilia aisee ningekuwa na uhakika asilimia mia peponi, mana kila wakati nanusa Kama imo.
mkuu leta episode nyingineRIWAYA: MSAKO WA MWEHU
SEHEMU YA NANE
Wakazunguka nyuma ya kibanda kwenye maboksi na uchafu wa dukani na kilipo kifurushi cha mwehu "Maso Maso". Kachero Manu akakalia kiti cha mbao kichakavu huku Soni akikalia juu ya dumu tupu, lenye rangi ya manjano la lita 20 la mafuta ya kula. Mahojiano yakaanza kama ifuatavyo;
Kachero Manu: "Unamfahamu vipi Maso Maso?"
Soni: "Kumfahamu kivipi ningeomba ufafanuzi "
Kachero Manu: "Hivyo hivyo unavyomjua" alijibu Kachero Manu kwa sauti yenye hasira ila hakutaka kujijulisha.
Soni: "Maso Maso", ni mwehu ambaye amezoea kukaa hapa dukani kwangu, pembeni hapo ulipokaa ndio kikazi chake. Iwe mvua iwe jua hapo ndio maskani yake, wanasema watu kapigwa kipapai"
Kachero Manu: "Ana muda gani tokea awe anakita kambi dukani kwako hapa?"
Soni:"Sikumbuki vizuri sana ila haizidi miezi sita"
Kachero Manu: "Kuna vitu labda alikuwa anaongea ongea na wewe? "
Soni: "Hapana, mara nyingi alikuwa anautumia kuimbaimba nyimbo zake na kuandika andika kwenye kidaftari chake, mara chache ndio alikuwa anaongea lakini maongezi yasiyo na mtiririko maalumu ya kiwehuwehu"
Kachero Manu: "Unaweza kunionyesha hilo furushi lake nione hicho anachokiandika!". Soni akajibu swali kwa vitendo kwa kwenda kubeba fuko lenye vitu vya chizi "Maso Maso" akalibwaga mbele ya Kachero Manu. Kachero Manu akasitisha mahojiano kwa muda akaanza kazi ya kuchakurachakura kwenye lile fuko la mwehu. "Kweli hili fuko la chizi, mpaka chupa za mikojo zimo! " alijisemea kimoyomoyo Kachero Manu. Kulikuwa na vikorokoro vya simu mbovu, taa mbovu za kuchaji za Mchina, karatasi zilizochanika za aya za Qu'ran, viwembe vilivyotumika, mabakuli na vikombe na kila aina ya takataka zinazostahili kuwemo kwenye furushi la chizi.
Alipokuwa anakaribia kukata tamaa akashika kitu kigumu, alipokivuta akakuta ni daftari. Akashikwa na tashiwishi ya kulifungua na kujua kilichoandikwa. Ikadondoka kikaratasi chakavu cha maandishi ya Kiarabu, akakihifadhi sehemu salama. Kisha alipozidi kulifungua daftari hakuona chochote cha kumsaidia zaidi ya namba za simu kochokocho.
Kachero Manu: "Je siku ya mlipuko, Maso Maso alikuwepo au hakufika kabisa?". Akaendeleza mahojiano yake baada ya kulifunga furushi vizuri.
Soni: "Ndio alikuwepo alikaa hapo hapo, ila siku hiyo alikuwa kama mgonjwa hakuwa mchangamfu na hakula chochote tokea asubuhi, ulipotokea ule mlipuko, taharuki iliyokuwepo siku hiyo kila mtu aliingilia upande wake, na hajaonekana tena eneo hili mpaka tuna wasiwasi kama amesalimika na kifo"
Kachero Manu: "Ahsante sana kwa ushirikiano wako, nikikuhitaji tena nitakuja na samahani kwa kukuchelewesha na biashara yako"
Soni: "Hamna shida karibu tena, ngoja nifungue duka langu sitaki kula mate " aliongea kwa sauti ya hasira huku uso wake umebeba mawimbi ya ndita kuonyesha kuchukizwa kwa kuhojiwa muda wa biashara. Kachero Manu hakujali akaondoka zake huku akiwa amechukua kila kiratasi na kile kidaftari cha "Maso Maso" huku akishukuru kwa kupata majibu yaliyomkifu kifaya.
Muda sasa ulikuwa umeenda harijojo, ilikuwa imeshafika saa moja kasorobo magharibi. Akapitiliza moja kwa moja mpaka kwenye geti la Wizara ya Mambo ya Ndani kwenda kukagua namba za hiyo gari v8 PT3001 aliyotajiwa na Soni kuwa kigogo anayeitumia hiyo gari anamsaka .
Kachero Manu alikuwa tayari kasharuhusiwa na walinzi wa eneo hilo kufanya ukaguzi wake wa gari anayoitafuta. Alikuta v8 zaidi ya 18 rangi ya buluu zimejipanga. Hayo yote yalikuwa ni magari yanayotumiwa na Vigogo wa Wizara na Polisi Makao Makuu. Akaanza kufanya spenkesheni yake kwenye yale magari. Alirudia zaidi ya mara tatu halikuona lile gari alilotajiwa jina namba zake na Soni, PT3001.
Kijasho chembamba kikaanza kumvuja mpaka kwenye meno. Uso wake ukala debe akaanza kukata tamaa ya kuikosa gari hiyo. Akaamua awashe na mwangaza wa tochi ya simu yake ya mkononi kusaidia mwangaza wa eneo lile. Alipofika kwenye gari lenye namba 'PT1003' akasimama kwa muda akiikagua. "Namba hili zinafanana na zilizotajwa PT3001 tofauti ni mpangilio wa namba tu, labda zinachezewa" aliwaza Kachero Manu.
Akaanza kuchezea kile kibao namba za gari, akakikuta kibao kimeungwaungwa kiufundi mkubwa huwezi kugundua kwa haraka. Katika kupekenyua akakuta kuna nyaya zimepita kwenye namba tatu na moja. "Shabaaaashiii......kuna mchezo mchafu unafanyika, inaelekea gari ikitoka geti kuna kitufe kinabinywa kuzichezea namba za mwishoni zinapishana ndio maana mtaani linasoma PT3001, lakini humu ndani linasoma PT1003, kwisha kazi ujanja wake upo uchi" alijisemeza yeye mwenyewe.
Haraka haraka akawa anarudi pale getini kuulizia jina la kigogo anayetumia lile gari lenye namba za utata.
Alipofika wakati anaandikiwa jina la kigogo anayeitumia hiyo gari, tahamaki mtaani karibia na getini ikasikika milio ya risasi mbili zilizopigwa mtawalia, na kufuatiwa na risasi moja iliyobutuliwa juu, halafu ikasikika mseleleko mkali wa gari lenye kwenda kwa mchepuo wa kasi. Akajua mambo yameshaenda segemnege huko nje. Akafanya haraka kuchukua ile karatasi aliyopewa na kukimbilia nje ya geti huku mkononi tayari kachomoa bastola yake.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji737]
"Muuza duka Soni ameuliwa kinyama kibandani kwake"
Mamia ya watu walikuwa wamekusanyika karibia na kiduka cha Soni, huku giza lilikuwa tayari limeanza kushitadi angani katika usiku huo mbichi. Kila mmoja akijiuliza kulikoni mpaka muuza duka Soni ameuliwa kikatili namna ile. Hali ya hewa ilishachafuka kifo cha Soni kilizua tenge tahanani eneo hilo jirani na Wizara ya Mambo ya Ndani.
Maiti ya Soni ilikuwa imelala chali, damu zinamtiririka huku matundu ya risasi yakionekana dhahiri shahiri kwenye paji lake la uso na shingoni.
"Mie nimeshuhudia kila hatua ya tukio hili, walikuja watu wawili kwenye gari rangi ya kijivu aina ya "Brevis", mtu mmoja mrefu amevaa koti la kujikinga na mvua na kofia akashuka akaenda mubashara kwenye kiduka. Sikumfuatilia nikajua ni mteja wake tu anahitaji vitu vya dukani. Baadae nikaona kama kuna furushi kalibeba tokea kule anakohifadhia marehemu Soni takataka zake akalirusha ndani ya gari. Nae akaingia ndani ya gari kwa kuharakisha, lakini hawakuliondoa gari. Halafu baada ya kupita kitambo kama cha dakika 10 akashuka mmoja akakaribia tena kama meta 3 akanyanyua bastola yake na kumfyatulia risasi mbili za kichwani, ikabidi nijifiche nyuma ya kabati la fundi viatu jirani pale. Mpigaji akakimbilia kwenye gari kwa haraka. Alivyoona tumeanza kujikusanya wakadhani tunataka kuwapiga kipopo, mmoja wao akapiga risasi moja hewani, kisha wakatimka na gari lao wakala matu kwa umahiri mkubwa. Wakaingilia hiyo barabara ya mtaa wa Ohio na gari lao na kutokomea kusikojulikana" alielezea tukio hilo kwa ufasaha mkubwa mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo.
Kachero Manu alivyoona umati wa watu umejikusanya akaamua kuirudisha silaha yake kwenye ala yake, akasogea karibu na eneo la tukio. Alikuwa ni mmoja wa wale waliosikiliza kwa umakini kabisa maelezo ya yule shuhuda. Baada ya hapo akaisogelea maiti ya Soni, akaona tayari kashaaga dunia, ameshaelekea jongomeo zamani.
Akajiona ni mtu mwenye bahati ya mtende kuwahi kuzungumza nae Soni muda mchache kabla hajapoteza maisha yake na kupata maelezo yaliyompa mwangaza wa upelelezi wake. Akatumia fursa ya watu kushuhudia mwili wa marehemu kuzunguka kule nyuma ya kiduka kwenye matakataka kuangalia kama furushi la chizi "Maso Maso" lipo au ndio limebebwa na wauaji!. Alipopiga jicho, akaona hamna kitu limepotea. "Kumbe furushi la mwehu, ni dili kama dhahabu linasakwa kwa udi na uvumba" alijiwazia peke yake Kachero Manu huku anatabasamu. Alishaanza kuunganisha matukio mbalimbali yatakayofanikisha upelelezi wake na hatimaye kuwatia mbaroni wahusika wa matukio ya ugaidi uliotekelezwa kwenye jengo la Wizara ya Mambo ya Ndani, Ijumaa iliyopita.
Askari kanzu wakawa wameshafika na kuanza kutawanya watu huku wakizungushia uzio eneo la tukio. Kachero Manu akaona isiwe tabu akaanza kuondoka mdogo mdogo kwa miguu kurejea ofisini, kufungasha vitu vyake arejee nyumbani kwake, tayari kwa safari ya Dodoma kesho kutwa yake.
Alipanga kwenda kumuongezea nguvu Kachero Yasmine. Lakini tukio la kuuliwa kwa kijana Soni kulimpa msongo wa mawazo wa kutaka kufahamu "je kuna uhusiano kati ya mauaji ya Soni na msako wa walipuaji wa jengo la Wizara? "
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji737]
ITAENDELEA
KUPATA HARDCOPY NICHEKI
0625920847
Hiki chenyenyewe kabisa yaani kimenoga balaa.RIWAYA: MSAKO WA MWEHU
SEHEMU YA NANE
Wakazunguka nyuma ya kibanda kwenye maboksi na uchafu wa dukani na kilipo kifurushi cha mwehu "Maso Maso". Kachero Manu akakalia kiti cha mbao kichakavu huku Soni akikalia juu ya dumu tupu, lenye rangi ya manjano la lita 20 la mafuta ya kula. Mahojiano yakaanza kama ifuatavyo;
Kachero Manu: "Unamfahamu vipi Maso Maso?"
Soni: "Kumfahamu kivipi ningeomba ufafanuzi "
Kachero Manu: "Hivyo hivyo unavyomjua" alijibu Kachero Manu kwa sauti yenye hasira ila hakutaka kujijulisha.
Soni: "Maso Maso", ni mwehu ambaye amezoea kukaa hapa dukani kwangu, pembeni hapo ulipokaa ndio kikazi chake. Iwe mvua iwe jua hapo ndio maskani yake, wanasema watu kapigwa kipapai"
Kachero Manu: "Ana muda gani tokea awe anakita kambi dukani kwako hapa?"
Soni:"Sikumbuki vizuri sana ila haizidi miezi sita"
Kachero Manu: "Kuna vitu labda alikuwa anaongea ongea na wewe? "
Soni: "Hapana, mara nyingi alikuwa anautumia kuimbaimba nyimbo zake na kuandika andika kwenye kidaftari chake, mara chache ndio alikuwa anaongea lakini maongezi yasiyo na mtiririko maalumu ya kiwehuwehu"
Kachero Manu: "Unaweza kunionyesha hilo furushi lake nione hicho anachokiandika!". Soni akajibu swali kwa vitendo kwa kwenda kubeba fuko lenye vitu vya chizi "Maso Maso" akalibwaga mbele ya Kachero Manu. Kachero Manu akasitisha mahojiano kwa muda akaanza kazi ya kuchakurachakura kwenye lile fuko la mwehu. "Kweli hili fuko la chizi, mpaka chupa za mikojo zimo! " alijisemea kimoyomoyo Kachero Manu. Kulikuwa na vikorokoro vya simu mbovu, taa mbovu za kuchaji za Mchina, karatasi zilizochanika za aya za Qu'ran, viwembe vilivyotumika, mabakuli na vikombe na kila aina ya takataka zinazostahili kuwemo kwenye furushi la chizi.
Alipokuwa anakaribia kukata tamaa akashika kitu kigumu, alipokivuta akakuta ni daftari. Akashikwa na tashiwishi ya kulifungua na kujua kilichoandikwa. Ikadondoka kikaratasi chakavu cha maandishi ya Kiarabu, akakihifadhi sehemu salama. Kisha alipozidi kulifungua daftari hakuona chochote cha kumsaidia zaidi ya namba za simu kochokocho.
Kachero Manu: "Je siku ya mlipuko, Maso Maso alikuwepo au hakufika kabisa?". Akaendeleza mahojiano yake baada ya kulifunga furushi vizuri.
Soni: "Ndio alikuwepo alikaa hapo hapo, ila siku hiyo alikuwa kama mgonjwa hakuwa mchangamfu na hakula chochote tokea asubuhi, ulipotokea ule mlipuko, taharuki iliyokuwepo siku hiyo kila mtu aliingilia upande wake, na hajaonekana tena eneo hili mpaka tuna wasiwasi kama amesalimika na kifo"
Kachero Manu: "Ahsante sana kwa ushirikiano wako, nikikuhitaji tena nitakuja na samahani kwa kukuchelewesha na biashara yako"
Soni: "Hamna shida karibu tena, ngoja nifungue duka langu sitaki kula mate " aliongea kwa sauti ya hasira huku uso wake umebeba mawimbi ya ndita kuonyesha kuchukizwa kwa kuhojiwa muda wa biashara. Kachero Manu hakujali akaondoka zake huku akiwa amechukua kila kiratasi na kile kidaftari cha "Maso Maso" huku akishukuru kwa kupata majibu yaliyomkifu kifaya.
Muda sasa ulikuwa umeenda harijojo, ilikuwa imeshafika saa moja kasorobo magharibi. Akapitiliza moja kwa moja mpaka kwenye geti la Wizara ya Mambo ya Ndani kwenda kukagua namba za hiyo gari v8 PT3001 aliyotajiwa na Soni kuwa kigogo anayeitumia hiyo gari anamsaka .
Kachero Manu alikuwa tayari kasharuhusiwa na walinzi wa eneo hilo kufanya ukaguzi wake wa gari anayoitafuta. Alikuta v8 zaidi ya 18 rangi ya buluu zimejipanga. Hayo yote yalikuwa ni magari yanayotumiwa na Vigogo wa Wizara na Polisi Makao Makuu. Akaanza kufanya spenkesheni yake kwenye yale magari. Alirudia zaidi ya mara tatu halikuona lile gari alilotajiwa jina namba zake na Soni, PT3001.
Kijasho chembamba kikaanza kumvuja mpaka kwenye meno. Uso wake ukala debe akaanza kukata tamaa ya kuikosa gari hiyo. Akaamua awashe na mwangaza wa tochi ya simu yake ya mkononi kusaidia mwangaza wa eneo lile. Alipofika kwenye gari lenye namba 'PT1003' akasimama kwa muda akiikagua. "Namba hili zinafanana na zilizotajwa PT3001 tofauti ni mpangilio wa namba tu, labda zinachezewa" aliwaza Kachero Manu.
Akaanza kuchezea kile kibao namba za gari, akakikuta kibao kimeungwaungwa kiufundi mkubwa huwezi kugundua kwa haraka. Katika kupekenyua akakuta kuna nyaya zimepita kwenye namba tatu na moja. "Shabaaaashiii......kuna mchezo mchafu unafanyika, inaelekea gari ikitoka geti kuna kitufe kinabinywa kuzichezea namba za mwishoni zinapishana ndio maana mtaani linasoma PT3001, lakini humu ndani linasoma PT1003, kwisha kazi ujanja wake upo uchi" alijisemeza yeye mwenyewe.
Haraka haraka akawa anarudi pale getini kuulizia jina la kigogo anayetumia lile gari lenye namba za utata.
Alipofika wakati anaandikiwa jina la kigogo anayeitumia hiyo gari, tahamaki mtaani karibia na getini ikasikika milio ya risasi mbili zilizopigwa mtawalia, na kufuatiwa na risasi moja iliyobutuliwa juu, halafu ikasikika mseleleko mkali wa gari lenye kwenda kwa mchepuo wa kasi. Akajua mambo yameshaenda segemnege huko nje. Akafanya haraka kuchukua ile karatasi aliyopewa na kukimbilia nje ya geti huku mkononi tayari kachomoa bastola yake.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji737]
"Muuza duka Soni ameuliwa kinyama kibandani kwake"
Mamia ya watu walikuwa wamekusanyika karibia na kiduka cha Soni, huku giza lilikuwa tayari limeanza kushitadi angani katika usiku huo mbichi. Kila mmoja akijiuliza kulikoni mpaka muuza duka Soni ameuliwa kikatili namna ile. Hali ya hewa ilishachafuka kifo cha Soni kilizua tenge tahanani eneo hilo jirani na Wizara ya Mambo ya Ndani.
Maiti ya Soni ilikuwa imelala chali, damu zinamtiririka huku matundu ya risasi yakionekana dhahiri shahiri kwenye paji lake la uso na shingoni.
"Mie nimeshuhudia kila hatua ya tukio hili, walikuja watu wawili kwenye gari rangi ya kijivu aina ya "Brevis", mtu mmoja mrefu amevaa koti la kujikinga na mvua na kofia akashuka akaenda mubashara kwenye kiduka. Sikumfuatilia nikajua ni mteja wake tu anahitaji vitu vya dukani. Baadae nikaona kama kuna furushi kalibeba tokea kule anakohifadhia marehemu Soni takataka zake akalirusha ndani ya gari. Nae akaingia ndani ya gari kwa kuharakisha, lakini hawakuliondoa gari. Halafu baada ya kupita kitambo kama cha dakika 10 akashuka mmoja akakaribia tena kama meta 3 akanyanyua bastola yake na kumfyatulia risasi mbili za kichwani, ikabidi nijifiche nyuma ya kabati la fundi viatu jirani pale. Mpigaji akakimbilia kwenye gari kwa haraka. Alivyoona tumeanza kujikusanya wakadhani tunataka kuwapiga kipopo, mmoja wao akapiga risasi moja hewani, kisha wakatimka na gari lao wakala matu kwa umahiri mkubwa. Wakaingilia hiyo barabara ya mtaa wa Ohio na gari lao na kutokomea kusikojulikana" alielezea tukio hilo kwa ufasaha mkubwa mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo.
Kachero Manu alivyoona umati wa watu umejikusanya akaamua kuirudisha silaha yake kwenye ala yake, akasogea karibu na eneo la tukio. Alikuwa ni mmoja wa wale waliosikiliza kwa umakini kabisa maelezo ya yule shuhuda. Baada ya hapo akaisogelea maiti ya Soni, akaona tayari kashaaga dunia, ameshaelekea jongomeo zamani.
Akajiona ni mtu mwenye bahati ya mtende kuwahi kuzungumza nae Soni muda mchache kabla hajapoteza maisha yake na kupata maelezo yaliyompa mwangaza wa upelelezi wake. Akatumia fursa ya watu kushuhudia mwili wa marehemu kuzunguka kule nyuma ya kiduka kwenye matakataka kuangalia kama furushi la chizi "Maso Maso" lipo au ndio limebebwa na wauaji!. Alipopiga jicho, akaona hamna kitu limepotea. "Kumbe furushi la mwehu, ni dili kama dhahabu linasakwa kwa udi na uvumba" alijiwazia peke yake Kachero Manu huku anatabasamu. Alishaanza kuunganisha matukio mbalimbali yatakayofanikisha upelelezi wake na hatimaye kuwatia mbaroni wahusika wa matukio ya ugaidi uliotekelezwa kwenye jengo la Wizara ya Mambo ya Ndani, Ijumaa iliyopita.
Askari kanzu wakawa wameshafika na kuanza kutawanya watu huku wakizungushia uzio eneo la tukio. Kachero Manu akaona isiwe tabu akaanza kuondoka mdogo mdogo kwa miguu kurejea ofisini, kufungasha vitu vyake arejee nyumbani kwake, tayari kwa safari ya Dodoma kesho kutwa yake.
Alipanga kwenda kumuongezea nguvu Kachero Yasmine. Lakini tukio la kuuliwa kwa kijana Soni kulimpa msongo wa mawazo wa kutaka kufahamu "je kuna uhusiano kati ya mauaji ya Soni na msako wa walipuaji wa jengo la Wizara? "
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji737]
ITAENDELEA
KUPATA HARDCOPY NICHEKI
0625920847